Sayansi inahangaika kuthibitisha iliyoyakuta yameumbwa na kwasababu hiyo kila siku tafiti zinafanyika ikiwa na maana bado haijafikia kikomobchabkuthibitisha kuankitu hiki kipo hivi kwasababu ya hivi.
Ujinga ni kubaki na elimu usiyohitaji kuithibitisha kwa akili zako mwenyewe, kumbuka AKILI ninkile kinachobaki pindi ukiyatoa yooote uliyofundishwa. Je Mtoto ambaye hajaanza kufundishwa Sayansi, ukimuuliza Jua linatembea au limesimama atakujibu vipi? Au ukimuuliza Mwezi unatembea au Umesimamabatakujibu vipi?
Ujanja sio kupinga usiyoyajua, bali ujanja ni kutetea yale uliyo na uhakika nayo. Hivi unadhani kuna kuna mtu ambaye hajafundishwa kua Dunia ni kama tufe? Je kuhoji uhakika wa hilo somo ni Ujinga.
Turudi katika Imani. Je yaliyopo katika Sayansi kwenye Imani hayapo? Nipe mfano hatabmmoja kipinkipo katika Sayansi ila katika Imani za Dini hakipo.
Biblia katika kitabu cha Mwanzo tuu, Unapata habari za uumbwaji wa Dunia na Shape yake. Je imeelezea ipo katika umbo gani? Je Jua au Mwezi vimetofautishwaje kiimani kuankimoja kimesimama kingine kinatembea. Na ndio nikauliza, Ni nini Utofauti wa Jua na Mwezi pondi tuviangaliapo kwa Macho vikiwa vinahama position yake yaani kutembea. Au nikubariki na Swali hili, kwanini unaamini Mwezi haujasimamansehemu moja kama unavyoamini kwa Jua?
Kiimani au Kiroho kuna Vita ya Shetani na Mungu kila mmoja akitaka Mwanadamu Amtumikie, Mungu kaleta Masharti yake kupitia Imani na shetani kaleta Masharti yake kupitia Sayansi, so Uamuzi ni wako maana hakuna linalowezekana Kisayansinkiimani likashindikana vivyo hivyo Sayansi Inahangaika kuyawezesha ya Kiimani yawezekane Kisayansi. Narudia upande wa kiimani au Kiroho ni Somo lingine pana zaidi ili uweze kuielewa Sayansi na Malengo yake.
Hapa kwakua unabishania kitu ulichofundishwa dhidi ya uhalisia wa milangonyako ya fahamu namna unavyoona kuhisi nk, ni ngumu kutoka katika kifungo ulichofungwa kwa zaidi ya miaka saba dhidi ya Uhuru unaooneshwa kwa Sekunde kadhaa za kusoma hojabzinazopingana na uliyomezeshwa, maana naamini haujawahi kuthibitisha kwa hisia zako kua Dunia inazunguka ila kwa Macho yako huwa unaliona Jua likitembea.