Siri Ya Hati Ya Muungano Na Njama Za Kuuficha

Siri Ya Hati Ya Muungano Na Njama Za Kuuficha

Mchambuzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2007
Posts
4,850
Reaction score
9,434
Mjadala huu utakuwa na sehemu kuu NNE.


SEHEMU YA KWANZA: Msingi Wa Mkataba Ulikiukwa, Woga Wa CCM Serikali Tatu.

Mchakato wa Katiba Mpya ulitoa fursa pekee kwa CCM kurekebisha kasoro zilizojitokeza huko nyuma ambazo ndio zimezaa "kero sugu" za muungano. Iwapo CCM ingekiri makosa hayo huku ikitoa sababu mbalimbali za kihistoria na mazingira ya dunia ya wakati ule kwa ujumla, wananchi wengi wangesema "Yaliyopita Si Ndwele, Tuyagange Yaliyopo na Yajayo". CCM ingepata fursa ya kuaminiwa na sehemu kubwa ya umma na kushirikiana na chama hiki katika uzinduzi wa Tanganyika.

Hii ilikuwa ni fursa adimu ya chama (CCM) kuhakikisha kwamba: (1) inarithisha vijana wake Chama ambacho kimemaliza kazi ya kulimaliza ‘jinamizi' lililosumbua chama na taifa kwa miaka zaidi ya 30; (2) Chama kinajenga mazingira ya kukomesha "Suala la muungano" kuwa ni "suala la vyama vya siasa" bali suala la "kitaifa"; (3) Chama kinalinda na kuboresha muungano kwa kufuata mapendekezo ya tume ya mabadiliko ya Katiba. Hatua ya chama kuendelea kutetea serikali mbili katika mchakato wa Katiba, ni sawa na kuamua kuendelea kulea Kero za Muungano, na sio kuzipunguza kero hizi kama chama kinavyodai [rejea kauli za CCM za hivi karibuni kupitia Katibu Mkuu Taifa (Abdurahaman Kinana), na Katibu wa CCM NEC Taifa (Itikadi na Uenezi), Nape Nnauye].

Mkataba wa Muungano (1964) ulitoa sura ya kuwepo kwa shirikisho la serikali tatu [Masuala kumi na moja ya Muungano, huku masuala nje ya haya kumi na moja yakibakia kwa serikali za nchi shiriki za muungano (Yani Serikali Ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar)]. Chini ya mfumo huu wa serikali tatu, kati ya serikali hizi mbili shiriki (Tanganyika na Zanzibar), hakuna Serikali iliyopangwa na Mkataba wa Muungano kuwa na madaraka makubwa kuliko serikali nyenzake. Kilichobadilisha yote haya ilikuwa ni chama cha TANU kuingilia suala la muungano kinyume na mkataba wa muungano (1964).

MKATABA WA MUUNGANO: Vyanzo (Sources):

1. Jumbe, A (1995): The Partner - Ship: Muungano Wa Tanganyika na Zanzibar: Miaka 30 Ya Dhoruba.
2. Shivji, I (2008): Pan-Africanism or Pragmatism? Lessons of Tanganyika and Zanzibar Union.

MKATABA WA MUUNGANO
Baina ya
JAMHURI YA TANGANYIKA
Na
JAMHURI YA WATU WA ZANZIBAR

Kwa kuwa Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar zinafahamu uhusiano wa muda mrefu watu wake na mshikamano na kukuza uhusiano huo na kuimarisha mshikamano na kukuza umoja wa watu wa Afrika, zimekutana na kutafakari Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar.

Na kwa kuwa Serikali za Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar, zinapendelea ya kwamba Jamhuri hizi mbili ziungane kuwa Jamhuri moja huru moja kwa amasharti ya makubaliano yafuatayo:

Kwa hiyo IMEKUBALIWA baina ya Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika na ya Jamhuri ya watu wa Zanzibar kama ifuatavyo:-

(i) Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar zitaungana na kuwa Jamhuri huru moja.

ii) Katika kipindi cha kuanza kwa Muungano mpaka Baraza la Kutunga katiba lililotajwa katika ibara ya (vii) litakapokutana na kupitisha katiba ya Jamhuri ya Muungano (Kuanzia hapa kitaitwa kipindi cha mpito), Jamhuri ya Muungano itaongozwa kwa masharti ya ibara ya (iii) mpaka ya (vi).

(iii) Katika kipindi cha mpito katiba ya Jamhuri ya Muungano itakuwa katiba ya Tanganyika iliyorekebishwa ili kuweka:

a) Chombo tofauti cha kutunga sheria na Serikali kwa ajili ya Zanzibar kwa mujibu wa sheria zilizopo za Zanzibar na vitakuwa na mamlaka ya mwisho katika Zanzibar kwa mambo yote isipokuwa yale tu yaliyo chini ya bunge na Serikali ya Jamhuri ya Muungano;

b) Nafasi ya makamo wawili wa Rais mmoja kati yao akiwa ni mkaazi wa Zanzibar atakuwa ndiye kiongozi wa Serikali iliyotajwa kwa ajili ya Zanzibar na atakuwa ndiye msaidizi mkuu wa rais wa Jamhuri ya Muungano katika utekelezaji wa kazi za Serikali kwa upande wa Zanzibar;

c) Uwakilishi wa Zanzibar katika bunge la Jamhuri ya Muungano;

d) Mambo mengine yatayofaa au kuhitajika ili kuipa nguvu Jamhuri ya Muungano na mkataba huu.

(iv) Mambo yafuatayo yatakuwa chini ya bunge na Serikali ya Jamhuri ya Muungano:-
a) Katiba na Serikali ya Jamhuri ya Muungano
b) Mambo ya nchi za nje
c) Ulinzi
d) Polisi
e) Mamlaka yanayohusika na hali ya hatari
f) Uraia
g) Uhamiaji
h) Mikopo na biashara ya nchi za nje
i) Utumishi katika Jamhuri ya Muungano.
j) Kodi ya mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa nchini na kusimamiwa na idara ya forodha
k) Bandari, mambo yanayohusu usafiri wa anga, Posta na Simu

v) Bunge na Serikali vilivyotajwa vitakuwa na mamlaka ya mwisho juu ya mambo yote yahusuyo Jamhuri ya Muungano na kuongezea mamlaka juu ya mambo yote yahusuyo Tanganyika.

Sheria zote zilizopo za Tanganyika na za Zanzibar zitaendelea kutumika katika maeneo yao bila kuathiri:-

a) Masharti yoyote yatakayowekwa na chombo chenye mamlaka ya kutunga sheria.

b) Masharti yatakayowekwa kwa amri ya Rais wa Zanzibar juu ya sheria yoyote inayohusu jambo lolote lililotajwa kwenye ibara ya (iv), na kufuta sheria yoyote inayolingana Zanzibar.

c) Mabadiliko yoyote kama yataonekana yanafaa au kuhitajika ili kufanikisha Muungano na mkataba huu.

(vi) (a) Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano atakuwa ni Mwalimu J. K. Nyerere na ataongoza Serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa kufuata masharti ya mkataba hu na kwa kusaidiwa na maofisa wengine atakaowateuwa toka Tanganyika na Zanzibar na watumishi wa Serikali zao.

b) Makamo wa kwanza wa Rais kutoka Zanzibar aliyeteuliwa kwa kufuata marekebisho kama yalivyoelezwa na ibara ya 3, atakuwa Sheikh Abeid Karume.

(vii) Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa kukubaliana na Makamo wa Rais ambaye ni kiongozi wa serikali ya Zanzibar
a) Atateua tume kwa ajili ya kutoa mapendekezo kwa ajili ya katiba ya Jamhuri ya Muungano.

b) Ataitisha Baraza la kutunga katiba ikiwa na wawakilishi kutoka Tanganyika na Zanzibar katika idadi itakayoamuliwa likutane katika kipindi cha mwaka mmoja tokea kuanza kwa muungano kwa madhumuni ya kutafakarimapendekezo ya tume iliyotajwa juu na kupitisha katiba ya Jamhuri ya Muungano.

(viii) Mkataba huu utahitaji kuthibitishwa kwa kutungiwa sheria na Bunge la Tanganyika na Baraza la Mapinduzi la Jamhuri ya Watu wa Zanzibar kwa kushirikiana na Baraza lake la Mawaziri, na mkataba kupitishwa na kuundwa kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano na ya Zanzibar kwa kufuata masharti yaliyokubaliwa.

KWA KUSHUHUDIA HAPA Julius K. Nyerere, Rais wa Jamhuri ya Tanganyika na abeid Karume, Rais wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, wametia saini nakala mbili za mkataba huu, hapa Zanzibar siku ya tarehe Ishirini na mbili ya mwezi Aprili, 1964.
___________________________
Umepitishwa katika Bunge siku ya tarehe Ishirini na Tano ya Aprili, 1964.
P. MSEKWA
…………………..Karani wa Bunge

Nathibitisha kwamba Muswada wa Sheria hii ulipitishwa na Bunge kwa mujibu wa ibara ya 35 ya katiba.
A.S. MKWAWA
..........………………………..Spika

25, Aprili 1964.


Inaendelea bandiko linalofuata (#2).


Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.


cc Nguruvi3, @FJM,@ tpaul, @Mag3, @JokaKuu, @Mwigulu Nchemba, @Nape Nnauye, @MwanaDiwani,@zomba, @Ritz, @ZeMarcopolo, @Gamba la Nyoka, @Mtanganyika , @Mzee Mwanakijiji, @Pasco, @Kitila Mkumbo, @EMT, @MTAZAMO, @Kobello, @Jasusi, @zumbemkuu, @Mimibaba, @Zakumi, @Invisible, Kurugenzi ya Habari, @mnyepe, @Yericko Nyerere, @FaizaFoxy, @Dingswayo, @Makusudically, @Tumaini Makene, @Nicholas, Mtu wa Pwani, jmushi1, Mwita Maranya, Ngongo, zumbemkuu, Mzawa Halisi, Barubaru, Mindi, Kiganyi, Communist
 
Inaendelea toka Bandiko #1


Tukiudadisi Mkataba wa Muungano, 1964 (Rejea bandiko #1 hapo juu), hatuoni sehemu yoyote ambayo chama/vyama vya siasa vikitajwa. Kitendo cha TANU kuingilia suala la muungano lilikuwa ni kiuko kubwa kuliko yote ya mkataba wa muungano (1964). Baadae tutaona jinsi hali hii ilivyojitokeza. Hatua ya TANU kutoa mamlaka ya Chama kushika hatamu na kuvifanya vyombo na taasisi zote kuwa chini yake ilikuwa ni kwenda kinyume na Mkataba wa Muungano (1964) na Sheria za Muungano (1964). Athari zilizopo sasa ni kwamba, mbali ya uwezekano wa muungano kuvunjika, upande wa muungano ambao umeathirika na ukiukwaji huu, unaweza kuchukua hatua katika ngazi za kimataifa, kwa mfano kwenda kufungua kesi katika mahakama ya kimataifa juu ya "Kosa la kukiukwa Mkataba wa Muungano. Mashataka haya pia yanaweza kwenda Katika Mahakama ya Katiba.

Tukizidi kuudadisi Mkataba wa Muungano (1964), tunaona kwamba NIA ilikuwa ni muundo wa wa serikali tatu au mamlaka ambazo zingeundwa kiiunganishi ambazo katika nyaraka hiyo zilitajwa kuwa ni:

· Serikali Ya Tanganyika
· Serikali Ya Zanzibar
· Serikali Ya Jamhuri ya Muungano

MKATABA WA MUUNGANO ULIDHAMIRIA SERIKALI TATU, SIO SERIKALI MBILI AU SERIKALI MOJA.

Mkataba wa Muungano (1964) ulikubaliwa uwe ndio msingi utakaopima Katiba yoyote ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ITAKAYOFUATA. Licha ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano (1977) kukiuka Mkataba wa Muungano, bado katiba hii iliundwa kutokana na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, hivyo Mkataba wa Muungano (1964) kuendelea kuwa ndio msingi wa kisheria wa Muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar. Pia Mwanazuoni maarufu na mtaalamu wa masuala ya Sheria za Katiba (Professa Issa Shivji) anahimiza jambo hili katika maandishi yake: The Legal Foundations of the Union in Tanzania's Union and Zanzibar's Constitution (OUP, DSM, 1990).]

Katika ibara ya 3 (b) ya mkataba wa Muungano (1964), ibara hii inaelekeza juu ya makamu wa Rais kama taasisi. Mkataba unatoa nafasi kwa uteuzi wa Makamu wa Rais Wawili, huku ikihimiza kwamba kila upande wa muungano utoe Makamu wa Rais mmoja, ambao kwa pamoja watamsaidia Rais wa Muungano katika utendaji wake wa kazi za kiserikali katika masuala yanayohusu muungano "Ndani ya Tanganyika na Ndani ya Zanzibar". Kifungu hiki kinachoelezea juu ya uteuzi wa Makamu wawili wa Urais kutoka Tanganyika na Zanzibar kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano, ni ushahidi wa kwanza kwamba Mkataba wa Muungano (1964) ulidhamiria Serikali TATU, na sio Serikali Mbili wala Serikali Moja.

Tukienda kwenye ibara ya (5) ya Mkataba huu, tunaona kwamba, ibara hii inalinda sheria zilizopo Tanganyika na Zanzibar kwa maana ya kwamba – sheria hizi zinatakiwa zibaki kama zilivyo na nguvu zake katika maeneo yake. Huu ni ushahidi mwingine kwamba idadi ya serikali zilizodhamiriwa na Mkataba wa Muungano (1964), zilikuwa ni serikali TATU. Ni dhahiri kwamba kilichokusudiwa na Mkataba wa Muungano (1964) kupitia ibara hii ya (5) ni kwamba – taasisi za nchi hizi zilizoungana zilitakiwa kubaki kama zilivyo isipokuwa kwenye maeneo yaliyotajwa (rejea orodha ya masuala kumi na moja ya muungano).

Tunaweza kusema pia kwamba, kupitia ibara hii ya (5), taasisi nyingine zote za Serikali ya Tanganyika na serikali ya Zanzibar zilihakikishiwa na Mkataba huu kwamba zitafanya kazi bega kwa bega na taasisi mpya za serikali ya Muungano. Kwa mfano, kazi zilizohusiana na utumishi wa umma wa Tanganyika na Zanzibar zilihakikishwa kuendelea kuwepo kama awali.Tukitazama ibara ya 6(a) ya mkataba huu, tunaona mkataba ukitamka kwamba – Rais wa Jamhuri ya Muungano ataendeleza kazi zake za Jamhuri ya Muungano kwa msaada wa maafisa ambao atawateua kutoka pande zote mbili – za Tanganyika na Zanzibar na hiyo iendane na taasisi husika za utumishi wa umma ambazo zilikubaliwa ziwe ni sehemu ya yale masuala kumi na moja ya muungano huku taasisi zote nyingine ambazo hazikuwa za muungano, hizi zibakie kwa serikali mbili husika – Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar.

Tukienda katika ibara ya (7) ya Mkataba huu, ibara hii inazungumzia juu ya kuitishwa kwa baraza la kutunga sheria. Katika hili, ibara hii inatamka waziwazi kwamba – uteuzi wa wajumbe wa baraza la kutunga sheria utafanywa na Rais wa Muungano kwa makubaliano (sio ushirikiano, bali makubaliano) na Makamu wa Rais ambae ndie kiongozi wa serikali ya Zanzibar. Pia ikaelekezwa kwamba baraza hili la kutunga sheria litaundwa na wajumbe kutoka pande zote mbili za muungano – Tanganyika na Zanzibar kwa idadi itakayoamuliwa.

Mwisho, tukitizama ibara ya (8) ya Mkataba wa Muungano, ibara hii inataka mkataba huo uthibitishwe na vyombo vya kutunga sheria vya Tanganyika na Zanzibar ili kutoa nguvu za kuanzishwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (sio Jamhuri ya Muungano wa Tanzania)!. Maana ya kifungu hiki ni kwamba: (1) Nchi za Tanganyika na Zanzibar zilichukuliwa katika hali ya "usawa"; (2) idadi ya serikali zilizohusika zilikuwa ni tatu – Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

Kama tutakavyoona baadae, vifungu vyote hivi vya Mkataba wa Muungano (1964) vilikiukwa, hasa baada ya TANU kuingilia Mkataba wa Muungano. Hatua hii ya TANU ndio imekuwa chanzo kikuu cha kero sugu za muungano hadi leo. Pamoja na mapungufu haya yote, CCM inaendelea kutetea mfumo wa Serikali Mbili, huku ikidai kwamba kero zilizopo ni "changamoto" ambazo zitarekebishwa chini ya mfumo huo huo wa serikali mbili. Hatua hii ni kinyume cha maoni ya wananchi wengi mbele ya Tume ya Katiba ambao walipendekeza mfumo wa serikali tatu baada ya kubaini kwamba kero hizi hazijapata ufumbuzi kwa miaka 50.

Tumalizie sehemu hii ya kwanza kwa nukuu za mwanazuoni Issa Shivji [Pan-Africanism or Pragmatism: Lessons of Tanganyika and Zanzibar Union (2008), page 99, Paragraph 1]:

There is no doubt that the process of the formation of the union was fraught with Legal Manipulation and Political Expediency. The Union started on rather shaky legal and political foundations. Had the constitutional and legal framework been only temporary, for the interim one – year period, as it was originally envisaged to be, perhaps, the shaky foundations of the origins of the Union would have been overcome and forgotten. But the interim period was extended and became a long, tumultuous thirteen years before a permanent constitutional framework of the Union was put in place. For reasons that we will explore in subsequent chapters, the ghosts of the origins of the Union still haunt what has often been ‘celebrated' as the first still surviving experiment of African Unity.


[Let The People Speak: Tanzania Down the Road to Liberalism (2006), page 119, paragraph 2]:

Frankly the failure to acknowledge that the two – government structure is unworkable is, in my opinion, the biggest single blind spot in Mwalimu's Vision of Unity. I need not belabor the point for it has been debated and has been shown in practice to be unworkable. In fact, to continue to insist on it is the surest way of breaking the union.

Pia Issa Shviji [Let The People Speak: Tanzania Down the Road to Liberalism (2006), page 105, paragraph 3]:

The extent to which people participate in crystallizing and determining the final shape of the new constitution, to that extent we would have created a possibility that no ruling party, whether CCM or any other, could easily flout the rights of people at their whim. People will defend only what they have created. They may, as they always do, applaud the creations of the rulers imposed on them but when the chips are down, they will not stand by other people's creation. Therefore, the way we chart the path of constitution – making is crucial.

Itaendelea sehemu ya pili ambapo tutajadili yafuatayo:

1. Ibara ya (4) ya Mkataba wa Muungano (1964), ambayo inachanganya watu wengi na kupeleka hisia kwamba Mkataba wa Muungano uliitaka Tanganyika (baadae Tanzania Bara), kuvaa koti la Muungano. Kama tutakavyojadili, tutaona kwamba mtazamo huu sio sahihi.

2. Pia tutajadili sheria na dikrii mbalimbali zilizoifuta Tanganyika pamoja na athari zilizojitokeza kwa nchi washirika na muungano kwa ujumla.


Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.
 
nimo nnapitia ukweli mchungu.

Mchambuzi unatoa dozi, sasa kama mgonjwa anataka kupona lazima anywe au aendelee na maradhi hadi mauti yamnyakue
 
Last edited by a moderator:
SEHEMU YA PILI


· TANGANYIKA ilichakachuliwa.
· Katiba Ya Jamhuri ya Muungano ilikiuka Mkataba wa Muungano (1964).
· Hakujawahi kuwapo matakwa ya kisheria kuhalalisha muungano wa Tanzania.

Katika bandiko #2 , tulijadili kwamba ibara ya (4) ya Mkataba wa Muungano (1964), imekuwa ikichanganya baadhi ya watu kwamba pengine Mkataba huu ulidhamiria Tanganyika (baadae Tanzania Bara), ivae koti la Muungano. Kama tutakavyoona, mtazamo huu sio sahihi. Sababu ya ya msingi ya watu kuchanganyikiwa juu ya suala hili ni kwamba – chini ya Mkataba wa Muungano (1964), serikali ya muungano ilipewa mamlaka ya kusimamia na kuendesha mambo yote yanayohusu Tanganyika (yasiyo ya muungano), lakini kwa kipindi cha mpito tu (mwaka mmoja).

Tukumbuke kwamba, ni kutokana na kuwepo kwa Tanganyika (Kiserikali na Kieneo/jiografia), ndipo madaraka yakatolewa kwa Rais wa Kwanza wa Muungano kusimamia na kuendesha mambo yaliyohusu Tanganyika (Yasiyokuwa ya muungano kwa upande wa Tanganyika). Na hivyo ndivyo Mkataba wa Muungano (1964) ulivyoelekeza, huku zikitajwa mamlaka tatu (1) Mamlaka ya Zanzibar, (2) Mamlaka Ya Muungano, na (3) Mamlaka ya Tanganyika. Mkataba wa Muungano ukaagiza kwamba Mamlaka ya Tanganyika iwekewe kwa muda tu (kwa mwaka moja) chini ya Rais wa kwanza wa Muungano. Kama tutakavyojadili baadae, hali ikageuzwa mwezi mmoja tu kabla ya kipindi cha mpito kumalizika.

Kwa vile tu mamlaka ya Tanganyika yaliwekwa chini ya Rais wa Serikali ya Muungano kwa muda, haina maana kwamba Mkataba wa Muungano (1964) ulitaka hali hiyo iendelee hata katika Katiba ya Kudumu, ya Jamhuri ya Muungano. Kwahiyo, ni makosa kwa baadhi ya watu kujenga hoja kwamba sababu hiyo basi sheria za Tanganyika (zilizokuwa nje ya muungano) ziliacha kufanya kazi baada ya mkataba kusainiwa. Kisheria, Serikali ya Muungano inaweza kufanya kazi zake kuhusiana na Tanganyika kwa njia ya kutumia sheria za Tanganyika pekee, kuhusiana na mambo yasio ya muungano.

Tukiutazama Mkataba wa Muungano, Mkataba huu unatoa sura ya uwepo wa serikali tatu: (1) Tanganyika, (2) Zanzibar, na (3) Muungano. Na hata katika sehemu ya utangulizi wa mkataba huu, tunaona wazi kabisa kwamba kwamba Mkataba huo ni wa JAMHURI YA TANGANYIKA NA JAMHURI YA WATU WA ZANZIBAR. Mkahata huu hausemi kwamba ni Mkataba wa JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. Pia mkataba huu unasema kwamba Marais wa Tanganyika na Zanzibar wakiwakilisha nchi zao mbili, wameamua kuziunganisha nchi hizi mbili kwa nia ya kuzaa "Jamhuri ya Mamlaka Moja".

Kufuatia muungano huo, ndio wakaunda Serikali ya Jamhuri ya Muungano. Kwa maana hii, uundwaji wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano uliongeza serikali tatu ambayo ingesimamia masuala kumi na moja tu ambayo nchi washirika (Tanganyika na Zanzibar ) waliyasalimisha kwa serikali mpya ya muungano. Kwa maana hii, mkataba ukaweka wazi kwamba serikali mbili za awali/kabla ya muungano (Serikali Za Tanganyika na Zanzibar), ziendelee kusimamia masuala mengine yote ya ndani kivyao, nje ya yale masuala kumi na moja ya muungano.
Kumekuwa na upotoshaji mkubwa juu ya hesabu za kujumlisha kuhusiana na idadi ya serikali ndani ya muungano. Kwa hesabu rahisi kabisa za darasa la kwanza, Moja (Serikali ya Muungano yenye mamlaka juu ya masuala kumi na moja tu) JUMLISHA MBILI (Yani Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar zenye mamlaka juu ya masuala mengineyo nje ya yale kumi na moja), Jibu ni TATU [1 + 2 = "3]. Jibu Sio "1", na wala sio "2". Kwa wale wanaodai kwamba jibu ni MOJA au MBILI, bandiko namba moja la mjadala huu limeweka CHETI CHA KUZALIWA cha Muungano yani Mkataba wa Muungano (1964), je:

· Ni wapi katika cheti hiki cha kuzaliwa kwa muungano kinaonyesha MOJA JUMLISHA MBILI NI MOJA AU MBILI?

Na cha kushangaza zaidi, muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar umezaa watoto waitwao "Tanzania Bara na Zanzibar". Kwa mujibu wa Mkataba wa Muungano, washiriki wa muungano walitakiwa kuendelea kuwepo – rejea ibara ya (5) ya Mkataba wa Muungano (1964) ambayo inasema kwamba:

Sheria za Tanganyika na Zanzibar zitaendelea kufanya kazi katika maeneo yahusikanayo.


UKIUKWAJI WA MKATABA WA MUUNGANO (1964).

Kama tulivyokwisha jadili, Mkataba wa Muungano (1964) uliweka kipindi cha mpito cha mwaka mmoja cha kutekeleza yale yote ambayo yalikubaliwa ndani ya mkataba huo, ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa mchakato wa katiba mpya. Ibara ya (7) ya Mkataba wa Muungano inasema kwamba:

a) Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa kukubaliana na Makamu wa kukubaliana na Makamu wa Rais ambaye ni kiongozi wa serikali ya Zanzibar.

b) Ataitisha Baraza la Kutunga Katiba likiwa na wawakilishi kutoka Tanganyika na Zanzibar katika idadi itakayoamuliwa likutane katika kipindi cha mwaka mmoja tokea kuanza kwa Muungano kwa madhumuni ya kutafakari mapendekezo ya tume iliyotajwa juu ya kupitisha mkataba wa Jamhuri ya Muungano.

Lakini kinyume cha makubaliano ya mkataba huu, mwezi mmoja kabla ya kumalizika kwa kipindi cha mpito, ikatungwa Sheria ya Baraza la Kutunga Katiba (Namba 18) ya mwaka 1965. Sheria hii ikasambaratisha Mkataba wa Muungano (1964). Hili ndio likawa pigo takatifu lililobadilisha mwelekeo wa Muungano KIKATIBA, na kuwa ndio mwanzo wa maamuzi mengi yasiyo ya kikatiba ambayo hadi leo yanaupeleka muungano kaburini. Mwanazuoni na mtaalamu wa Sheria ya Katiba, Issa Shivji katika kitabu chake cha [Pan-Africanism or Pragmatism: Lessons of Tanganyika and Zanzibar Union (2008), page 99, Paragraph 1], analijadili suala hili kama ifuatavyo:

There is no doubt that the process of the formation of the union was fraught with Legal Manipulation and Political Expediency. The Union started on rather shaky legal and political foundations. Had the constitutional and legal framework been only temporary, for the interim one – year period, as it was originally envisaged to be, perhaps, the shaky foundations of the origins of the Union would have been overcome and forgotten. But the interim period was extended and became a long, tumultuous thirteen years before a permanent constitutional framework of the Union was put in place. For reasons that we will explore in subsequent chapters, the ghosts of the origins of the Union still haunt what has often been ‘celebrated' as the first still surviving experiment of African Unity.

Vile vile, Issa Shivji [Let The People Speak: Tanzania Down the Road to Liberalism (2006), page 94 (paragraph6, & page 95, paragraph 1], anasema kwamba:

If one was to judge by the standards of constitutionality, which are proclaimed today, our union and country had hardly had a constitutional government for the last thirty years. There were so many breaches – including surreptitious manipulations of the constitution – that in reality we did not live by our constitution. We even forgot to swear by it. We, at the HILL, stopped teaching constitutional Law in 1971 or 1972.

Kama yupo Mtanganyika mmoja aliye hai ambae anaweza kututhibitishia jinsi gani Tanganyika ilichakachuliwa, basi huyo ni Pius Msekwa. Mzee huyu ndiye mtendaji mkuu wa kwanza wa TANU (CCM), na pia alikuwa ni karani wa Bunge wakati mkataba wa muungano ulipokuwa unatia saini na waasisi wa Muungano. Umuhimu wa Mzee Msekwa ni kwamba – hata saini yake ipo katika hati halisi ya muungano. Lakini kama tunavyoelewa, saini yake na ya Mwalimu Nyerere zimechakachuliwa kwa maana ya kwamba, hati za muungano zilizowasilishwa kwa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba Dodoma, sio Hati halisi za Muungano bali ni ni "Magumashi", yenye jitihada za kuendeleza mazingaombwe ya CCM. Inasekemana kwamba hata Pius Msekwa mwenyewe amesema wazi kwamba alichokiona Dodoma (nyaraka ya muungano), hakina saini yake halisi bali ya kuchakachuliwa.

Katika Kitabu chake kipya kiitwacho: 50 Years of Independence: A Concise Political History of Tanzania, Mwandishi wake - Pius Msekwa anasema kwamba hakujawahi kuwapo matakwa ya kisheria kuhalalisha muungano wa Tanzania. Mzee Msekwa anasema kwamba – kilichofanyika ni kwa Mwalimu Julius Nyerere kutunga sheria iitwayo "Amri ya Masharti ya Mpito ya Mwaka 1964 (The Transitional Provisions Decree 1964), baada ya kusaini hati ya Makubaliano ya Muungano (Articles of the Union, 1964).

Kwa mujibu wa maelezo ya Pius Msekwa ambayo yamo katika waraka wa marekebisho ya Rasimu ya Katiba ya Wananchi (UKAWA), Msweka anaeleza kwamba:

Amri ile ilichapishwa katika gazeti la serikali la siku hiyo. Kupitia amri hiyo, watumishi wa serikali ya Tanganyika walibadilishwa na kufanywa watumishi wa Serikali ya Muungano.
Mahakama Kuu ya Tanganyika iligeuzwa kuwa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano; Na Nembo ya Taifa ya Jamhuri ya Tanganyika iligeuzwa kuwa nembo ya taifa ya Jamhuri ya Muungano.

Tarehe Hiyohiyo, Rais Nyerere alitunga Amri nyingine ya Rais iliyoitwa Amri ya Katiba ya Muda ya Mwaka (1964) – The Interim Constitution Decree 1964. Amri hii iliitanganza katiba ya Tanganyika kuwa ndiyo katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kifungu cha (4) cha amri hii ndicho kilichoipa serikali ya Muungano majukumu kuhusu mambo yote ya muungano katika jamhuri ya muungano na vilevile kwa mambo yasiyokuwa ya Muungano kwa upande wa Tanganyika.

15 Juni 1964, Mwalimu Nyerere alitunga amri nyingine tena iliyoitwa The Transitional Provisions (No.2) Decree, 1964, yani Amri ya Masharti ya Mpito (Na.2) ya mwaka 1964. Amri hii ilielekeza kwamba mahali popote ambapo sheria zilizpo zimetaja jina la "Tanganyika", basi jina hilo lifutwe na badala yake lina la "Jamhuri ya Muungano", liwekwe.

Vilevile, Amri hiyo ilielekeza mahali popote ambapo Seriklai ya "Tanganyika" imetajwa, au kwenye jambo au kitu chochote ambacho kwa namna yoyote kinmilikiwa au kinahusishwa na serikali hiyo, basi itachukuliwa kuwa ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano ndiyo iliyotajwa.

Uhai wa Tanganyika ulitolewa kwa njia ya "Amri". Athari za jumla za hizi ni kwamba eneo la kisiasa ambalo ndio ilikuwa Tanganyika lilitolewa uhai wake moja kwa moja kwa "Amri".

Hii ndio sababu hata jina la eneo la kijiografia lililojulikana zamani kama Tanganyika ilibidi libadilishwe na kuwa Tanzania Bara.


Inaendelea bandiko linalofuata ambapo tutajadili hoja za Msekwa kwa undani, huku tukichambua nyaraka anazozijadili.
 
''Uhai wa Tanganyika ulitoweka kwa njia ya amri'' haya ni maneno mazito sana
Shivji naye alisema katiba ilivunjwa , leo anajenga hoja kwa kutumia katiba ile ile aliyoiona mbaya.

Pius Msewka saini yake imechakachuliwa, kuna nini hapo.

Endelea kutoa dozi, Mchambuzi
 
Mchambuzi,

Ahsantum kwa darsa zako ingawa sasa zimekuwa nyingi sana kiasi cha kuanza kujirudia rudia. NAFIKIRI SASA USIWE WAKTI WA KUZIDI KULALAMA NA KUANGALIA HISTORIA BALI UWE WAKTI WENU KUPITIA WABUNGE WENU KATIKA BUNGE LA KATIBA WALIONE HILO NA KUCHUKUA MAAMUZI MAGUMU kama wanavyofanya waZnz kukwamisha kupatikana kwa 2/3 ya maamuzi hayo

Kinyume cha hapo mtabaki tu kulalama ndani ya JF bila kupata suluhisho.

Nakupongeza kwa darsa zako.

HONGERA SANA
 
Mkuu Mchambuzi ahsante kwa nondo hizi

.....

Katika drama zote huwa najiuliza swali moja....."Kwa faida ya nani".....na huyu "nani" ni nani?
 
Last edited by a moderator:
Inaendelea bandiko linalofuata ambapo tutajadili hoja za Msekwa kwa undani, huku tukichambua nyaraka anazozijadili.
Na iendelee ukimaliza tutapitia mstari mmoja hadi mwingine.
Watetezi wa serikali 2 nadhani wapo njiani. Nao tutawasoma kwa utulivu tu. Tutaweka mchele katika gunia tofauti na chuya. Watetezi wa 2 sijui wanasemaje kuhusu serikali kughushi mkataba!!!
 
Mchambuzi,

Ahsantum kwa darsa zako ingawa sasa zimekuwa nyingi sana kiasi cha kuanza kujirudia rudia. NAFIKIRI SASA USIWE WAKTI WA KUZIDI KULALAMA NA KUANGALIA HISTORIA BALI UWE WAKTI WENU KUPITIA WABUNGE WENU KATIKA BUNGE LA KATIBA WALIONE HILO NA KUCHUKUA MAAMUZI MAGUMU kama wanavyofanya waZnz kukwamisha kupatikana kwa 2/3 ya maamuzi hayo

Kinyume cha hapo mtabaki tu kulalama ndani ya JF bila kupata suluhisho.

Nakupongeza kwa darsa zako.HONGERA SANA
Kama kawaida yako ya kuvuruga mtitiriko wa mada kwa kuingiza yasiyohusika. Jiridhishe kabla ya kuandika http://habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/23786-dk-shein-asisitiza-serikali-2-mwafaka

Msikie huyu mzanzibar http://www.mwananchi.co.tz/Katiba/-/1625946/2270956/-/yww8t8z/-/index.html
 
Mchambuzi, ktk nyuzi zilizowahi kunipa mwanga wa muungano hii ni mojawapo. Asante sana.

Kingine, hivi majuzi alinukuliwa Shivji akisema haijui Tanganyika lakini kupitia uzi huu, baada ya kusoma paragraph za machapisho yake nimegundua kua Shivji, kama siyo kujikomba kwa watawala basi kala matapishi yake tena kwa hiari yake mwenyewe.

Endelea kutuelimisha mkuu.
 

Nguruvi3,

Tatizo lako ahali yangu ni kukurupuka bila kutafajari kabla kuamua.

Kumbuka nilichobainisha hapo ni mawazo yangu na ushauri wangu kwa MCHAMBUZI, Na nafikiri umeona hata mwenyewe Mchambuzi kanitumia LIKE pale.

Kumbuka kuwa ili mnakasha uwe mzuri lazima kuwe na mawazo mgongano (mbadala) kwa faida ya wengi na sio watu wote kukubali kila kitu hata kama unakioba wazi kuwa kina mushkira ndanimwe.

Lakin kumbuka ilmu hiyo imetolewa sana Znz walianza CUF kwa wanachama wao kudai Znz huru na ikaendelea mpaka kwa akina Mzee Moyo, Akina Jusa, Mansour Himid na kikundi cha UAMSHO wakalisemea zaidi kiasi cha waZnz kujitambua na kujua haki zao zinazofichwa na hivyo wote kuja na ZNZ KWANZA.

Kuandika makala pekee hakusaidii hata kidogo lazima watu wapande kwenye viriri na kupambanua mambo.

Nakupa pole sana.

 
Mchambuzi, ktk nyuzi zilizowahi kunipa mwanga wa muungano hii ni mojawapo. Asante sana.

Kingine, hivi majuzi alinukuliwa Shivji akisema haijui Tanganyika lakini kupitia uzi huu, baada ya kusoma paragraph za machapisho yake nimegundua kua Shivji, kama siyo kujikomba kwa watawala basi kala matapishi yake tena kwa hiari yake mwenyewe.

Endelea kutuelimisha mkuu.
Skype,

Nadhani uliona bandiko langu katika ule uzi ambao Shivji anasema kwamba haijui na haitaji Tanganyika. Nilishauri watu wa karibu na mzee wetu huyu wamshauri aache kutoa matamka na badala yake apumzike katika maisha yake ya ustaafu kwani anazidi kujivunjia heshima mbele ya jamii iliyomweshimu sana kwa mchango wake. Iwapo haukunisoma, niliwasilisha bandiko hilo hivi:
-----
ISSA SHIVJI (2006): Let the people speak: Tanzania Down the road to neoliberalism, page 117, Paragraph 6:

...Whatever form the new unity takes it ought to observe scrupulously the basic democratic principle of the right of people to self determination. This premise has two sides to it.

A) That between Zanziba and Tanganyika, as a people and nations, we would have to respect the principle of equality on the one hand, and be sensitive to the legitimate culture, history and sentiments of both parts, on the other. This means that THOSE OF US who come from the bigger nation, Tanganyika, and consider OURSELVES progressive and democrats, should be extra responsible and cautious in guiding against big nation Chauvism.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Skype,

Nadhani uliona bandiko langu katika ule uzi ambao Shivji anasema kwamba haijui na haitaji Tanganyika. Nilishauri watu wa karibu na mzee wetu huyu wamshauri aache kutoa matamka na badala yake apumzike katika maisha yake ya ustaafu kwani anazidi kujivunjia heshima mbele ya jamii iliyomweshimu sana kwa mchango wake. Iwapo haukunisoma, niliwasilisha bandiko hilo hivi:
-----
ISSA SHIVJI (2006): Let the people speak: Tanzania Down the road to neoliberalism, page 117, Paragraph 6:





Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Nimekusoma mkuu.
 
Last edited by a moderator:
SEHEMU YA TATU

Awali tuliona kwamba ibara ya (7) ya Mkataba wa Muungano (1964) ilitoa nguvu za kuchaguliwa Tume ambayo ingekuja na mapendekezo ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano. Ibara hii pia ikaamrisha kuwa Rais wa Muungano (Kiongozi wa Tanganyika huru), kwa makubaliano na Makamu wa rais wa muungano (Kiongozi wa Zanzibar huru) wataitisha:
Baraza la kutunga katiba ambalo litakuwa na wajumbe kutoka Tanganyika na Zanzibar katika idadi itakayoamuliwa ndani ya kipindi cha Mwaka Mmoja wa Muungano kwa ajili ya kukaa na kujadili mapendekezo ya Tume iliyotanguliwa kutajwa na kuipitisha katiba hiyo kwa Jamhuri ya Muungano.


HATUA ZA AWALI UCHAKACHUAJI WA MKATABA WA MUUNGANO (1964)

Maelekezo haya ibara ya (7) ya mkataba muungano (1964) hayakutekelezwa kama ilivyokubaliwa, na hali hii ni moja ya sababu kwanini muungano hadi leo umekumbwa na migogoro isiyokwisha. Issa Shivji anajadili hili kama ifuatavyo: Issa Shivji [Pan-Africanism or Pragmatism: Lessons of Tanganyika and Zanzibar Union (2008), page 99, Paragraph 1]:

There is no doubt that the process of the formation of the union was fraught with Legal Manipulation and Political Expediency. The Union started on rather shaky legal and political foundations. Had the constitutional and legal framework been only temporary, for the interim one – year period, as it was originally envisaged to be, perhaps, the shaky foundations of the origins of the Union would have been overcome and forgotten. But the interim period was extended and became a long, tumultuous thirteen years before a permanent constitutional framework of the Union was put in place. For reasons that we will explore in subsequent chapters, the ghosts of the origins of the Union still haunt what has often been ‘celebrated' as the first still surviving experiment of African Unity.

UCHAKACHUAJI WA MKATABA WA MUUNGANO (1964) NA PATASHIKA LA NYARAKA ZA MUUNGANO BUNGE LA KATIBA DODOMA

Patashika la nyaraka za muungano hivi karibuni bungeni Dodoma lilitokana na kifungu kifuatacho ndani ya rasimu ya Katiba:

SEHEMU YA KWANZA: Jina, Mipaka, Alama, Lugha na Tunu Za Taifa.
(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi na shirikisho lenye mamlaka kamili ambalo limetokana na muungano wa nchi mbili za Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar, ambazo kabla ya hati ya makubaliano ya muungano, 1964, zilikuwa nchi huru.

(3) HATI YA MAKUBALIANO YA MUUNGANO iliyorejewa katika ibara ndogo ya (1), ndio msingi mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania na katiba hii, kwa kadri itakavyo rekebishwa, itakuwa ni muendelezo wa makubaliano hayo.


NYARAKA ZILIZOWASILISHWA DODOMA NA SIRI INAYOFICHWA
· Nyaraka zilizowasilishwa Dodoma hazina umuhimu kwa Rasimu iliyopo

Pamoja na kwamba Rasimu ya Katiba inataja "MKATABA/HATI WA MUUNGANO" kama ndio cheti cha kuzaliwa cha muungano, nyaraka hii haikuwasilishwa Dodoma. Kilichowasilishwa Dodoma ilikuwa ni Sheria mbili za mwaka 1964 na 1965 ambazo kimsingi, zililenga kuudhoofisha Mkataba wa Muungano (1964). Kwa maana hii, Wajumbe wa UKAWA Dodoma "Are Barking at the Wrong Tree". Hata kama nyaraka zilizowasilishwa zingekuwa hazina matatizo na saini zake, bado zisingetatua tatizo. Rasimu ya Katiba katika Sura Ya Kwanza (1&3) inataja HATI au MKATABA WA MUUNGANO (1964) kama ndio msingi wa Muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar. Rasimu ya Katiba haina muda na Sheria za Muungano zilizofuatia baada ya Mkataba wa Muungano (1964) kusainiwa kwani sheria hizi zilichakachua makubaliano ndani ya mkataba wa muungano (1964). Tutajadili.

Hii ni SIRI muhimu sana ambayo bado imejificha. Kinachohitajika ni Cheti Cha Kuzaliwa kwa muungano (Mkataba wa Muungano, 1964), kama inavyoelekezwa na Rasimu ya Katiba. Nyaraka zilizowasilishwa Dodoma hazina maana kwani zililenga kufunika Hati/Mkataba wa Muungano, ili Sheria hizi ndio ziwe nguzo kuu ya Muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar. Kwa maana nyingine, ni muhimu kwa UKAWA na wananchi kwa ujumla wakaelewa kwamba - tatizo la msingi la nyaraka zilizowasilishwa Dodoma halipo katika kugushiwa kwa saini za Mwalimu Nyerere na Pius Msekwa, bali:

· Tatizo lipo kwenye Yaliyomo Katika Nyaraka zenyewe, ambazo zinapingana na Mkataba wa Muungano (1964), lakini pia kupingana na kinachotajwa Ndani ya Rasimu ya Katiba (2014) kama msingi wa Muungano uliopo.


UNDANI WA NYARAKA ZILIZOWASILISHWA

Nyaraka mbili zimewasilishwa Dodoma.

1. Nyaraka ya KWANZA ni - Sheria Namba 22, Aprili 25, mwaka 1964. Sheria hii ilipitishwa SIKU MOJA TU tu baada ya mkataba wa muungano kusainiwa. Ingawa dhumuni la msingi la sheria hii ilikuwa ni kuhalalisha Mkataba wa Muungano (1964), kilichotokea ndani ya nyaraka hii haikuwa kuuthibitisha muungano bali kuuchakachua muungano kwa nia ya kuutokomeza. Kwa maana hii, Sheria Namba 22 ya mwaka 1964 ni batili na ni kinyume cha "mkataba wa muungano (1964)." Hii ni sehemu ya siri inayofichwa. Tutafafanua.

2. Nyaraka ya PILI ni - Sheria Namba.18 ya Mwaka 1965. Sheria hii ilipitishwa MWEZI MMOJA TU kabla ya kipindi cha mpito kumalizika. Tukumbuke kwamba Mkataba wa Muungano (1964) ulielekeza juu ya kipindi cha mpito cha mwaka mmoja ambapo pamoja na mengineyo, ibara ya (7) ya Mkataba wa muungano (rejea bandiko #1 ) ilitarajiwa iwe imeanza kutekelezwa. Kama ilivyo kwa sheria namba 22 ya mwaka 1964 hapo juu, Sheria hii (namba 18, 1965), pia ililenga kupunguza makali ya Mkataba wa Muungano (1964), hasa kuchakachua ibara ya (7) ya Mkataba wa Muungano (1964. Hii nayo ni sehemu ya siri inayofichwa. Tutafafanua.


Inaendelea katika bandiko linalofuatia...


Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla
 
Inatoka bandiko #15


JE NI SIRI GANI INAYOFICHWA?


Tuanze na Sheria Namba 22 Ya Mwaka 1964 (Aprili 25, 1964). Sheria hii ni ndefu (kurasa karibia tano). Muda ukipatikana tutaiwasilisha.

Vinginevyo, Muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar ulianza kwa Mkataba/Hati ya makubaliano (rejea bandiko #1 ). Hata tukitizama kwenye utangulizi wa sheria yenyewe, inasema wazi kwamba madhumuni ya Sheria ya Muungano (Sheria Namba 22 Ya 1964):
Kuthibitisha Mkataba wa Muungano baina ya Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.
.

Tukiangalia ibara ya (5) ya mkataba wa muungano (1964) – rejea bandiko #1 , ibara hiyo inasema kwamba:

SHERIA ZILIZOPO TANGANYIKA NA ZANZIBAR ZIENDELEE KUWEPO NA ZITUMIKE NDANI YA MAENEO YA NCHI HIZO.


Lakini kinyume na Mkataba wa Muungano (1964), sheria ya muungano (Sheria Namba 22 ya mwaka 1964), katika kifungu cha pili kinakuja na tafsiri yake kuhusu "sheria zilizopo" na kusema:

SHERIA ZILIZOPO VITABUNI NA ZISIZOANDIKWA WAKATI WA MUUNGANO HUO UKIANZISHWA, LAKINI HAZIJUMUISHI KATIBA YA TANGANYIKA KATIKA KULE KUITHIBITISHA KWAKE KUWEPO KWA SERIKALI YA TANGANYIKA AU SHERIA NYINGINE AU TAMSHI AMBALO LITAPOTEZA NGUVU ZAKE KUTOKANA NA KUANZA KUTUMIKA KATIBA YA MUDA.

Hii ni kinyume kabisa na mkataba wa muungano (1964), kwa sababu - Katiba ya Tanganyika ndio ilikuwa ni SHERIA MAMA YA TANGANYIKA, hivyo kuwa juu ya sheria zote zilizopo na zilizotajwa chini ya ibara ya (5) ya mkataba wa muungano (1964). Sheria Namba 22 ya
Muungano ilitakiwa tu kuthibitisha Mkataba wa Muungano, sio zaidi ya hapo. Lakini tofauti na matarajio kwamba Sheria ile ingefuata makubaliano yaliyomo ndani ya Mkataba wa Muungano (1964), uchakachuaji wa Mkataba wa Muungano ukafuatia na sheria hii namba 22 ya mwaka 1964. Ilikuwa ni kinyume kabisa cha Mkataba wa Muungano (1964) kwa Sheria Ya muungano/Sheria namba 22 ya Mwaka 1964, kutamka kwamba:
Sheria zilizopo hazihusiani na katiba ya Tanganyika
.

Sheria Namba 22 ya 1964 pia inafanya ukiukwaji mwingine wa Mkataba wa Muungano (1964) kupitia kifungu cha (7) cha sheria hii. Kinyume na Mkataba wa Muungano, kifungu hiki kilikuwa na nia ya kutangaza "kufutwa kwa katiba ya Tanganyika", kama mwanzo wa safari ya ya Tanganyika kwenda kaburini. Ibara ya (7) ya sheria namba 22 (1964) hii inatamba kwamba:

Wakati Katiba ya Muda ya Jamhuri ya Muungano itakapoanza kutumika, katiba ya Tanganyika itakoma kuwa na nguvu kwa ajili ya Serikali ya Tanganyika kama sehemu tofauti ya Jamhuri ya Muungano.

Huu ulikuwa ni ukiukwaji wa wazi wa Mkataba wa Muungano (1964) kwani chini ya Mkataba huu, nchi shiriki (Tanganyika na Zanzibar) zilikubaliana kwamba katika kipindi cha mpito (mwaka mmoja), yani kutokea siku ya muungano hadi siku baraza la kutunga katiba litakapopitisha Katiba ya Tanzania, Serikali na Bunge la Tanzania litaifanyia kazi pia Serikali ya Tanganyika. Kulikuwa na umuhimu wa pekee wa kipengele hiki kuwepo ndani ya Mkataba wa Muungano (1964). Hii ni kwa sababu, chini ya Mkataba wa Muungano, Tanganyika ilikuwepo, Tanganyika ilikuwa na serikali yake kamili ikiwa na mamlaka juu ya eneo lote la Tanganyika katika mambo yasiyokuwa ya Muungano (nje ya orodha ya masuala kumi na moja ya muungano).

MUHIMU
Mkataba wa Muungano (1964) haukutoa ruhusa kwa katiba ya Jamhuri ya Muungano kutumika kuendesha mambo ya Tanganyika. Kilichosemwa na Mkataba wa Muungano ni kwamba – katiba iliyopo (Ya Tanganyika), ifanyiwe marekebisho ili iweze kutumika kwa ajili ya Muungano tu. Vinginevyo, ili kuongoza na kutawala Tanganyika, ilibidi kiongozi wa Tanganyika arudie, sio tu katika sheria zilizopo Tanganyika, bali katiba ya Tanganyika iliyokuwepo (ile ambayo haikuwa imefanyikwa marekebisho kwa ajili ya matumizi juu ya masuala kumi na moja ya muungano).

Pia, ni dhahiri kwamba katika kipindi cha Mpito (rejea mkataba wa muungano, 1964), Rais wa Muungano alikuwa pia na kofia ya urais wa Tanganyika. Lakini kilichotakiwa kufanyika katika kipindi cha mpito ilikuwa ni kutenganishwa kwa Kofia ya Urais wa Muungano na ile ya Urais wa Tanganyika, kama vile ilivyofanyika kwa Urais wa Zanzibar kutengwa na Urais wa Muungano. Na hii ndio ilikuwa mantiki ya Mkataba wa Muungano (1964) kuelekeza kwamba Rais wa Muungano atasaidiwa na Makamu wawili wa Urais (mmoja kutoka Tanganyika na mwingine kutoka Zanzibar).

Rais wa Muungano alikuwa na mamlaka ya kutawala juu ya masuala ya Muungano tu. Katika kipindi cha MPITO, Rais wa Muungano alikuwa na nguvu za kisheria kuongoza Tanganyika "KAMA RAIS WA MUUNGANO", sio "KAMA RAIS WA TANGANYIKA". Ibara ya 12(1) ya katiba ya muda (1965) inathibitisha suala hili inaposema kwamba:
[quote
Mamlaka ya serikali kuhusiana na mambo ya muungano kwa Jamhuri ya Muungano na kuhusiana na Tanganyika yanawekwa mikononi mwa Rais.
[/quote]


Itaendelea ambapo tutaangalia kwa undani Nyaraka nyingine iliyowasilishwa Dodoma – Sheria namba 18 ya Mwaka 1965.


Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla
 
Idumu jf, kweli kinachotokea mjengoni ni mazingaombwe tupu. Naomba watu wote walioko mjengoni wapitie uzi huu ili wapate namna ya kuendelea vzr na mchakato.
 
Mchambuzi, ktk nyuzi zilizowahi kunipa mwanga wa muungano hii ni mojawapo. Asante sana.

Kingine, hivi majuzi alinukuliwa Shivji akisema haijui Tanganyika lakini kupitia uzi huu, baada ya kusoma paragraph za machapisho yake nimegundua kua Shivji, kama siyo kujikomba kwa watawala basi kala matapishi yake tena kwa hiari yake mwenyewe.

Endelea kutuelimisha mkuu.
Jaji warioba alisha mlipua siku ileile kuwa huyu jama ni mnafiki hivi vitabu vya shiviji kwa sasa vikiingizwa sokoni vitapata soko kubwa sana jamani wasambazaji mko wapi???
 
Back
Top Bottom