Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
MAJI SHINGONI, 'MKATABA' WAPELEKWA DODOMA
NI BAADA YA UDANGANYIFU, HAKUNA AJUAYE NI UDANGANYIFU PART II?
NGUVU YA UMMA HAIJWAHI KUSHINDWA. CCM HAIONI MAONYO 10 YALIYOPITA.
Sehemu ya I
Bandiko la Mchambuzi limetukokota kuanzia safari ya Tanganyika hadi Tanzania na leo 'Tanzania mkanganyiko'
Ktibu mkuu kiongozi na waziri wameahidi kuufikisha 'unaoitwa mkataba wa muungano bungeni'. Pamoja na yote hayo ukweli unabaki kuwa 'uhuni wa mwanzo' hautoi nafasi kuaminika tena.
Sote tunafahamu mkataba feki umekanushwa na wahusika akina Msekwa na wazee wengine.
Balozi Sefue ametoa maelezo akililia lia kuhusu wananchi kushindwa kuwaelewa wanaohoji mkataba. Balozi Sefue na serikali ni kama wamechanganyikiwa.
Hoja za Lissu, Tundu hazijajibiwa, kilichofanyika ni kulia lia.
Wananchi kwa miaka mingi wamedai hati ya mkataba kwa kilio, leo wapi serikali ya CCM inapata ushujaa na mshipa wa kuwasemea eti wamefedheheshwa
Maswali yanayobaki kutojibiwa ni haya yafuatayo
1. Kwanini kwa miaka mingi serikali iligoma kuutoa na leo unapelekwa Dodoma kirahisi?
2. Kwanini serikali ilipeleka mkataba feki ikijua mkataba halisi upo na unatakiwa ?
3. Je, ni kweli kuwa UN iliwahi kuleta telex za kuomba mkataba, na majibu yake yalikuwa ni nini?
4. Je, mkataba umesajiliwa UN kwa mujibu wa taratibu kama ulivyombwa na maafisa wa UN?
Maswali hayo ndiyo yataka kiu ya wananchi na wala si kupeleka mkataba.
Tayari serikali imeshaonyesha udanganyifu nani wa kuamini tena karatasi kutoka Ikulu.
Hili si tatizo la wananchi ni tatizo la Ikulu.
Nafasi ya kuongelea mkataba alikuwa nayo Rais. Suala la mkataba si la leo au jana.
Rais akachagua njia ya kumshambulia Warioba ili kujenga uhalali wa anachOkitaka na si kile wananchi wanachotaka.
Leo Warioba amesimama akizungukwa na nyota zinazo ng'aa, giza nene likimgubika Rais wetu.
Swali lianalogonga vichwa vya watu ni hili, je, kuna nini kimefanya CCM iachie mkataba hata pale ilipogoma baada ya amri ya mahakama? Je, kweli ni mkataba halali au ni part II ya feki lingine?
Kwamba hili laweza kuwa ni mkataba feki, hilo halina shaka.
Kama waliweza kughushi wiki moja iliyopita, 'wahuni' hawawezi kubadili tabia siku 7 baadaye. Huu ni uhuni wa miaka 50 hivyo unahitaji rehabilitation nzito si program ya siku 7
Kwanini CCM wameamua kuutoa?
Kuna sababu kadha wa kadha
1. Kwamba, hoja walioijenga ya rasimu feki ya CCM ya serikali 2 itakufa kama mkataba hautoki.
Hoja ya CCM ni kuwa, msingi wa mkataba ni serikali 2.
Ingawa hoja halisi ni serikali 3 kama tulivyoonyeshwa na Mchambuzi hapo juu, kwa ulaghai wa kughushi maneno, wanakamati wa kamati za CCM bungeni wamelishwa maneno ya msingi wa mkataba ni serikali 2.
Kama CCM hawatoa mkataba uwe halali au feki, hoja yao itakosa mashiko.
Hoja itakayokuwa mbele ni moja, tuanze upya au jahazi livunjwe tugawane mbao.
Sisi wameshikwa kunako, na hakika wanatamani maliwato.Tumbo limevurugika.
2. CCM wasipotoa mkataba uwe halali au feki, hii itaanzisha mtinange (cascade of reactions) na hivyo kupelekea umoja wa mataifa kuhoji kuhusu uhalali wa muungano.
Hapo kunaweza kuibuka yasiyotarajiwa. CCM wanaepusha shari.
3. Nguvu ya umma: CCM imeshindwa kukabliana na nguvu ya umma.
Umma unaamini kuwa kinachosemwa na watu wengine ni ukweli vinginevyo hakukuwa na sababu za kupeleka mkataba feki.
Umma unaamini kuwa Makamu wa Rais na waziri mkuu mstaafu Warioba, Waziri mkuu mstaafu na katibu mkuu wa OAU Salim, Katibu myeka wa Nyerere mzee Butiku, Maprofesa na tume, wana sababu za msingi na za maana kuutaja mkataba katika rasimu.
Wana nia njema na walitaka jambo hilo likamilike kwa kupitia rasimu ya serikali 3 ambayo leo kungekuwa hakuna hoja hiyo.
CCM kwa kutotambua nguvu ya umma na kwa uzoefu wa udanganyifu wakajua kila jambo litapita kama upepo.
Tumeandika mara saba sabini kuwa hakuna mahali popote duniani dola iliwahi kushinda nguvu ya umma.
Kinachotokea sasa hivi ni nguvu ya umma kuanza kujidhihiri.
CCM kwa kuto ona maonyo bado wanaendelea na kiburi chao. Licha ya binu zao kufeli huko nyuma, CCM hawaonekani kujifunza lolote.
Hebu tuangalie dalili za nguvu ya umma, sehemu ya II
Inaendelea....
NI BAADA YA UDANGANYIFU, HAKUNA AJUAYE NI UDANGANYIFU PART II?
NGUVU YA UMMA HAIJWAHI KUSHINDWA. CCM HAIONI MAONYO 10 YALIYOPITA.
Sehemu ya I
Bandiko la Mchambuzi limetukokota kuanzia safari ya Tanganyika hadi Tanzania na leo 'Tanzania mkanganyiko'
Ktibu mkuu kiongozi na waziri wameahidi kuufikisha 'unaoitwa mkataba wa muungano bungeni'. Pamoja na yote hayo ukweli unabaki kuwa 'uhuni wa mwanzo' hautoi nafasi kuaminika tena.
Sote tunafahamu mkataba feki umekanushwa na wahusika akina Msekwa na wazee wengine.
Balozi Sefue ametoa maelezo akililia lia kuhusu wananchi kushindwa kuwaelewa wanaohoji mkataba. Balozi Sefue na serikali ni kama wamechanganyikiwa.
Hoja za Lissu, Tundu hazijajibiwa, kilichofanyika ni kulia lia.
Wananchi kwa miaka mingi wamedai hati ya mkataba kwa kilio, leo wapi serikali ya CCM inapata ushujaa na mshipa wa kuwasemea eti wamefedheheshwa
Maswali yanayobaki kutojibiwa ni haya yafuatayo
1. Kwanini kwa miaka mingi serikali iligoma kuutoa na leo unapelekwa Dodoma kirahisi?
2. Kwanini serikali ilipeleka mkataba feki ikijua mkataba halisi upo na unatakiwa ?
3. Je, ni kweli kuwa UN iliwahi kuleta telex za kuomba mkataba, na majibu yake yalikuwa ni nini?
4. Je, mkataba umesajiliwa UN kwa mujibu wa taratibu kama ulivyombwa na maafisa wa UN?
Maswali hayo ndiyo yataka kiu ya wananchi na wala si kupeleka mkataba.
Tayari serikali imeshaonyesha udanganyifu nani wa kuamini tena karatasi kutoka Ikulu.
Hili si tatizo la wananchi ni tatizo la Ikulu.
Nafasi ya kuongelea mkataba alikuwa nayo Rais. Suala la mkataba si la leo au jana.
Rais akachagua njia ya kumshambulia Warioba ili kujenga uhalali wa anachOkitaka na si kile wananchi wanachotaka.
Leo Warioba amesimama akizungukwa na nyota zinazo ng'aa, giza nene likimgubika Rais wetu.
Swali lianalogonga vichwa vya watu ni hili, je, kuna nini kimefanya CCM iachie mkataba hata pale ilipogoma baada ya amri ya mahakama? Je, kweli ni mkataba halali au ni part II ya feki lingine?
Kwamba hili laweza kuwa ni mkataba feki, hilo halina shaka.
Kama waliweza kughushi wiki moja iliyopita, 'wahuni' hawawezi kubadili tabia siku 7 baadaye. Huu ni uhuni wa miaka 50 hivyo unahitaji rehabilitation nzito si program ya siku 7
Kwanini CCM wameamua kuutoa?
Kuna sababu kadha wa kadha
1. Kwamba, hoja walioijenga ya rasimu feki ya CCM ya serikali 2 itakufa kama mkataba hautoki.
Hoja ya CCM ni kuwa, msingi wa mkataba ni serikali 2.
Ingawa hoja halisi ni serikali 3 kama tulivyoonyeshwa na Mchambuzi hapo juu, kwa ulaghai wa kughushi maneno, wanakamati wa kamati za CCM bungeni wamelishwa maneno ya msingi wa mkataba ni serikali 2.
Kama CCM hawatoa mkataba uwe halali au feki, hoja yao itakosa mashiko.
Hoja itakayokuwa mbele ni moja, tuanze upya au jahazi livunjwe tugawane mbao.
Sisi wameshikwa kunako, na hakika wanatamani maliwato.Tumbo limevurugika.
2. CCM wasipotoa mkataba uwe halali au feki, hii itaanzisha mtinange (cascade of reactions) na hivyo kupelekea umoja wa mataifa kuhoji kuhusu uhalali wa muungano.
Hapo kunaweza kuibuka yasiyotarajiwa. CCM wanaepusha shari.
3. Nguvu ya umma: CCM imeshindwa kukabliana na nguvu ya umma.
Umma unaamini kuwa kinachosemwa na watu wengine ni ukweli vinginevyo hakukuwa na sababu za kupeleka mkataba feki.
Umma unaamini kuwa Makamu wa Rais na waziri mkuu mstaafu Warioba, Waziri mkuu mstaafu na katibu mkuu wa OAU Salim, Katibu myeka wa Nyerere mzee Butiku, Maprofesa na tume, wana sababu za msingi na za maana kuutaja mkataba katika rasimu.
Wana nia njema na walitaka jambo hilo likamilike kwa kupitia rasimu ya serikali 3 ambayo leo kungekuwa hakuna hoja hiyo.
CCM kwa kutotambua nguvu ya umma na kwa uzoefu wa udanganyifu wakajua kila jambo litapita kama upepo.
Tumeandika mara saba sabini kuwa hakuna mahali popote duniani dola iliwahi kushinda nguvu ya umma.
Kinachotokea sasa hivi ni nguvu ya umma kuanza kujidhihiri.
CCM kwa kuto ona maonyo bado wanaendelea na kiburi chao. Licha ya binu zao kufeli huko nyuma, CCM hawaonekani kujifunza lolote.
Hebu tuangalie dalili za nguvu ya umma, sehemu ya II
Inaendelea....
Last edited by a moderator: