kwahiyo ulitaka amruke baba yake kuelezea historia? wakati alikuwepo kwanye hilo eneo,
tatizo ni wewe wala sio mohamed said, yeye ameeleza historia hizi kwenye medani tofauti na kwa upana,lete na wewe machapisho yako tusome,tukujue na weweTulia kijana wacha kuruka ruka kama bata bukini tangu lini historia ya Kariakoo ndio ikawa historia ya Tanganyika.Mtu akija kukwambia mimi ni Baba yako utamkubalia kwasababu anajua kucheza na lugha au kwasababu una maaba na paukwa pakawa.Ikiwa akili yako ni ndogo kiasi hichi unakubali jambo kirahisi rahisi kwasababu una swalii na Mohamed Said msikiti moja sitashangaa akija na story nyingine sizizo na kichwa wala miguu lakini bado utakubali.
tatizo ni wewe wala sio mohamed said, yeye ameeleza historia hizi kwenye medani tofauti na kwa upana,lete na wewe machapisho yako tusome,tukujue na wewe
Tulia kijana wacha kuruka ruka kama bata bukini tangu lini historia ya Kariakoo ndio ikawa historia ya Tanganyika.Mtu akija kukwambia mimi ni Baba yako utamkubalia kwasababu anajua kucheza na lugha au kwasababu una maaba na paukwa pakawa.Ikiwa akili yako ni ndogo kiasi hichi unakubali jambo kirahisi rahisi kwasababu una swalii na Mohamed Said msikiti moja sitashangaa akija na story nyingine sizizo na kichwa wala miguu lakini bado utakubali.
tatizo ni wewe wala sio mohamed said, yeye ameeleza historia hizi kwenye medani tofauti na kwa upana,lete na wewe machapisho yako tusome,tukujue na wewe
Ha haaa haaa Mohamed Said kumbe unasomesha historia ya Babu yako haya endelea wengine tukidhani hii ndio historia ya Tanganyika kumbe tulikuwa tunakusuka suka bure samahani sana Ustadhi wa Gerezani.
Al akhy Muhammad Saidi, wasikusumbue hawa, ukweli umeshajulikana wanachofanya ni kushindwa kuupinga kwa hoja badala yake wanaleta kebehi tuu.
Ukweli upi mkuu wakati tumeukanusha kwamaandishi kabisa?
Wanamajlis,
Waswahili tuna msemo.
Bubu alisema kwa uchungu wa mwanae:
7:24pm, 8 May - Mohamed Said: Edmund,
"There is more to the freedom struggle which some of us do not seem to have the inclination to talk or write about. For example, did you know that Abdul Sykes and the name you read in this Mtemvu story, Ali Mwinyi Tambwe went to Ukerewe Island where Hamza Mwapachu was 'exiled' by Governor Twining in March 1953 to discuss the candidacy of Julius Nyerere as new President of Tanganyika African Association as a prelude to the re-constitution of TAA into TANU in July 1954? I still recall the visit vividly. I was a standard three pupil then and together with my brother Bakari had to sleep in the sitting room leaving our bedroom to the two guests. Abdul Sykes was then President of TAA and the TAA leadership plus Dar-based political activists who were predominantly Moslems wanted Abdul Sykes to retain the Presidency. Abdul was eager to secure Hamza's position on the matter given the fact that it was Hamza who introduced Nyerere to the TAA leadership in Dar back in 1949 before Nyerere left for Edinburgh University. Since 1945 Hamza was firmly committed to the view that Nyerere was the best person to lead Tanganyika to independence. For two reasons: First, he knew Nyerere as a very close friend from Makerere between 1943 and 1945 and was seized of his intellectual capacity. Second, because after his two years stint in Wales as a mature student at the University of South Wales, Cardiff, and coming close to Fabian Society British friends, Hamza was of the firm belief that the Colonialists would be more amiable to dealing with a Christian leader than a Muslim one. Abdul agreed with Hamza and whilst he had to stand in opposition to Nyerere because of Party electoral rules, he voted for Nyerere to be President of TAA in July 1953.
So here is another piece of history that some of you are unaware of."
JV.
Kwanza uelewe,Abdul Sykes hakuwahi kuwa "rais" wa AA,TAA wala TANU.
Yeye aliongoza mapinduzi yakupiga ngumi wazee wa chama cha AA ambao ni katibu Klest Sykes baba yake mzazi, na Mtunza fedha bwana Ally Ramadhan
Kipindi Mwalimu anajiunga na TAA, Abdul Sykes alikuwa amekaimu tu kiti cha urais wa TAA baada ya rais halali Dr Vedastu Kyaruzi akiwa kahamishwa kituo chake cha kazi kwenda Sengerema
Yericko Nyerere,
Wanamajlis wengi wameniomba mara kadhaa kuwa nisijibishane
na wewe.
Kisa ni kuwa huna adab za mnakasha.
Jifunze kuandika kistaarabu.
Uandikapo ukiwa na ghadhabu fikra hazitengemai.
Hatuna haja ya kurejea njia ile ile ambayo tushaipita mimi na wewe
na wengine mara nyingi kwa kuwa inachosha.
Hii "note" niliyokuwekea hapa nimeiweka hapa jamvini ili ijazie
katika kuijua historia ya uhuru wa Tanganyika na historia ya Nyerere
na TANU.
Hapakuwa na zaidi ya hilo.
PS: Jina kamili ni Vedasto Kyaruzi na uhamisho ulikuwa kwanza
Kingolwira Prison, Morogoro kisha Nzega.
Mzee ukipewa heshima ni jukumu lako kuilinda,
Umepoteza hilo, umebaki kuilazimisha hesha.
Hoja yamsingi niliyokujibu hapo nikuwa Abdul Sykes hakuwahi "kuchaguliwa" kuwa rais wa Chama chochote duniani tangu azaliwe mpaka kufariki kwake.
Yericko,
Ikiwa unataka tumjadili Abdul Sykes na nafasi ya urais katika TAA sawa.
Abdul Sykes hakupata kuchaguliwa kuwa rais wa TAA na wala hili sikutegemea
kuwa ni jambo la kutaka kujadiliwa.
Baba yake Abdul Mzee Kleist Sykes hakupata kuwa rais wa African Associatio.
Hakuchaguliwa kuwa rais kwa sababu nafasi iliyomwenea ni ukatibu kwa sababu
ya kipaji chake cha kuoganaizi watu na mambo.
Pili hakuwa rais kwa sababu ya kipaji alichokuwanacho katika uandishi
na lugha.
Abdul Sykes kama baba yake na yeye alikuwa na kipaji kikubwa katika kuoganaizi
na alikuwa na ulimi mzuri sana wa kuzunguza Kiingereza.
Licha ya hayo alikuwa anajua kupiga taipu na kuandika hati mkato.
Hizi ndizo sifa zilizomfanya yeye siku zote achaguliwe nafasi ya ukatibu kuanzia
Dar es Salaam Dockworkers Union 1947 hadi TAA 1950.
Kleist akizungumza Kiingereza na Kijerumani.
Yericko,
Huijui historia ya TANU.
TAA haikuasisiwa 1927 bali 1929 na wakati ule nafasi za uongozi
hazigombewi.
Msome Iliffe "Modern Tanzanians" Kleist Sykes the Townsman
(Daisy Sykes) (1973) historia nzima ya AA imeandikwa mle.
Nimekuwekea "note" ya JV kwa Edmund akieleza mkakati wa
Nansio kati ya Hamza Mwapachu na Abdul Sykes vipi wabadili
uongozi 1953.
Kuhusu uchaguzi wa 1950 uliowatia madarakani Abdul na Kyaruzi
msome Listowel (1965) "The Making of Tanganyika," utajifunza
mengi na utajua kuwa juhudi kubwa ya kuwaingiza vijana hawa
madarakani ilitoka kwa Schneider Abdillah Plantan na huyu
alikuwa mmoja wa baba zake Abdul na aliyekuwa ametolewa
madarakani alikuwa Mwl. Thomas Plantan kaka yake Schneider
kwa hiyo ni baba yake mkubwa Abdul.
Hebu soma hiki kipande na mtafute Dr. Kyaruzi katika uongozi wa
TAA mwaka 1953 kabla TANU haijaasisiwa:
Hayo hapo chini ni kutoka kitabu changu: "The Life and Times of
Abdulwahid Sykes..." (1998):
In June, TAA headquarters announced its executive committee with
J.K. Nyerere, President; Abdulwahid Sykes, Vice-President; J.P.
Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias and
Waziri Dossa Aziz, Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer
and Ally K. Sykes as Assistant Treasurer.
Committee members were Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani,
Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo
and Patrick Aoko.[1]
Yuko Kyaruzi hapo?
Sasa ikiwa viongozi ndiyo hao 1953 mwaka mmoja kabla ya TANU
kuasisiwa Kyaruzi katoa mchango kutoka chama kipi na katika
mwakaupi?
Mwisho tunarudi palepale tulipoanzia na mimi kupata sababu ya
kuandika kitabu ambacho kwa miaka sasa kila uchao tunakizungumza
hapa jamvini.
Ikiwa historia ya uhuru wa Tanganyika ndiyo hii na historia ya TANU
chama cha uhuru ndiyo hii...
Imekuwaje historia ya TANU ikaja kuandikwa na ikawaacha nje wengi
wa wazalendo hawa?
Inawezekana Yericko Nyerere akaja na jibu.
Ningependa kumweleza Yericko kuwa Abdul alikuwa Kaimu
Rais TAA baada ya Dr. Kyaruzi kupewa uhamisho kwenda Kingolwira
(ingawa Yericko anasema uhamisho ulikuwa Sengerema) na alikaimu
nafasi hiyo toka 1951 - 1953.
Baada ya uchaguzi wa 1953 uliomuingiza Nyerere madarakani kama
rais wa TAA Abdul akawa makamu wa rais.
Unapoandika historia ya TANU na ukaanza na Nyerere na kumtoa nje
Abdul Sykes hapo mtafiti anakuwa kajipalia makaa.
Historia hiyo haiwezi kusimama kwani mtafiti anakuwa si kama kajipunja
yeye mwenyewe bali pia kaipunja historia ya uhuru wa Tanganyika.
Jambo la kushangaza ni kuwa Dr. Kyaruzi alipatapo kueleza kuhusu
historia yake ya siasa na akasema kuwa ilikuwa yeye ndiye aliyemwachia
Nyerere chama.
Katika makala nzima hakupata kumtaja Abdul Sykes wala uchaguzi wa
1950 wala hakumtaja Schneider Plantan.
Ilikuwa yeye Kyaruzi na Nyerere peke yao katika historia ya TANU.
Hizi ndizo historia zetu.
Wanamajlis,
Anaetaka kumjua vizuri Dr. Kyaruzi aingie hapa:
Mohamed Said: DK. VEDASTO KYARUZI DAKTARI MWANAHARAKATI WA TAA
[1] Tanganyika Standard, 19 th June 1953.
Yericko,
Kuna watu wamejaaliwa uelewa wa juu kabisa na kuna wengine
uelewa wa chini.
Narejea na kuongeza maelezo ili yule mzito wa akili na yeye apate
kuelimika.
Ndiyo kila nitoapo darsa huunganisha na darsa lingine kumuongezea
msomaji maarifa.
Ndipo hapo nimeweka kiungo cha Dr. Kyaruzi nikukumbushe kuwa
uhamisho wake haukuwa Sengerema bali Kingolwira kisha Nzega.
Nimekuwekea na gazeti la Tanganyika Standard la 19 June 1953
kukuonyesha kuwa Abdul Sykes alikuwa Makamu wa Rais TAA chini
ya Nyerere yote haya kuwaonyesha watu kuwa naijua vizuri sana
historia ya TANU kwa ushahidi wa rejea za uhakika.
Yote kukuhakikishia kuwa haikamiliki si historia ya TANU au ile ya
Nyerere mwenyewe katika uuuru wa Tanganyika bila kumtaja Abdul
Sykes.
Kwa hakika napokea salaam nyingi sana za shukurani ya kuiokoa
historia ya uhuru wa Tanganyika.
Huna lolote la kusema kuhusu taarifa ya JV kwa Edmund kuhusu
uchaguzi wa TAA 1953 uliomuingiza Nyerere madarakani?