Siri ya Meya Kinondoni kugombana na Mkurugenzi

Kwakuwa tayari Mkuu wa Mkoa mpya wa Dar es Salaam Amos Makalla ( Mzee wa Masebene ya Congo DR ) ameshawapatanisha inatosha na hizi Ngojera zako za Majungu na Umbea wala hatuzitaki na baki nazo tu Rohoni Kwako na Moyoni Mwako pia sawa?
SUKUMA-GANG roho inawauma, mfuateni mwendazake alipo kama hamuopendi Tanganyika.
 
Maelezo yako yamenyooka na nimeyapenda, hata kama ni majungu basi ni majungu yaliyokwenda skuli. Sipora Liana!!
Mama anayependa kusikika kwa Mabifu kama Shilole. Mwanamke mwenye mawazo mgando kwamba ili uonekane Mkurugenzi mzuri basi waumize wapinzani au wanaoonekana watenda haki.
Sipira Liana;
Mwanamke kiburi anayeamini hakuna wa kumfanya chochote kwa vile yuko upande wa system.
Safari hii hatimaye ameonekana udhaifu wake baada ya kukosa mpinzani wa kuonea ameamua kuwarudi aliowabeba. Anafanya hivyo akiwa anajua wazi hakuna wa kumgusa maana yeye ndiye aliyewaweka hapo kwa kura za wizi. Watamwambia nini wakati ushindi wao haramu akiyeuhalalisha ni yeye?
 
Hao waliowachagua hao madiwani wakomba pesa ndio waliona wanawafaa.
HAKUNA UCHAGUZI, kura ziliibwa nchi nzima acha kuhalalisha damu isiyo na hatia wewe.
Unaweza kwenda kanisani kumshukuru Mungu kwa ushindi kweli ? acheni dhihaka kwa Mungu
 
Magufuli aliharibu kila kitu.Haya hayakuwepo, Wacha Mungu atende kazi yake. Tungelikuwa wapi kama Mungu asingelite da kazi yake. Liana aliwatesa sana wapinzani. Sukuma gang, naye atapigwa chinni, tusubiri uteuzi
Una umri gani?
 
Wenyewe kwa wenyewe wanapalulana sisi kimyaa si wapinzani wanachelewesha maendeleo
 
Kale kamama inaonekana hata kutoa unyumba kwa mume wake ni ka tata sana
 
Mkuu tatizo lililopo ni serikali kuu kuingilia mamlaka ya serikali za mitaa kwa kujua au kutokujua, kimsingi, kama serikali za mitaa zingekuwa na mamlaka yake kamili zingekuwa zinaajiri kila mtumishi kuanzia mkurugenzi kwenye maeneo yao. Inavyoonekana sasa serikali kuu imechukua vyanzo vingi vya mapato vya halmashauri na kuna halmashauri zinaweza zisijiendeshe endapo serikali isingetoa ruzuku kugharamia shughuli mbalimbali......sasa mkurugenzi anajikuta anawajibika kwa rais aliyemteua, ina maana serikali kuu na hapo hapo anawajibika kwa baraza la madiwani. Je, ni wapi mizania inatakiwa iwekwe ili mkurugenzi asionekane analiburuza baraza la madiwani, kwa mamlaka aliyonayo kutokana na nafasi yake ya uteuzi kutokea ndani ya serikali kuu....
 
Mkurugenzi wa halmashauri anatakiwa aajiriwe na halmashauri.Kuteuliwa wakurugenzi na mamlaka nyingine ni dosari kubwa sana ya katiba tuliyo nayo.
Hivi vyeo vingine Rais wampunguzie uteuzi...viwe watu wanaapply na vyombo vilivyo safi na umakini vitumike kuwapata na kwa transparency,na kuhakikisha due deligency na vetting kama nchi zingine zilizo serious kwenye mambo ya uongozi.....kazi iendelee.
 
Nakubaliana na ushauri wako. Kwani hakuna Job description ya ded? Au kwa vile wanateuliwa na raisi ndiyo wanakuwa na kiburi kiasi hicho? Kazi zingine wawe wanatupa sisi tuwafundishe kazi.
 
Nakubaliana na ushauri wako. Kwani hakuna Job description ya ded? Au kwa vile wanateuliwa na raisi ndiyo wanakuwa na kiburi kiasi hicho? Kazi zingine wawe wanatupa sisi tuwafundishe kazi.
Tanzania Mtu akiteuliwa tu na Rais,Basi na yeye hujiona kama nae ni Rais,tena anakuwa mbabe sana kuliko hata Rais mwenyewe!!
 
SIYO MAJUNGU, hizi ni habari za ndani kabisa ambazo akina paschal mayala walipaswa kuziibua, hii nchi imeoza sana na huyu mama alikuwa kiongozi mkuu wa kufundisha genge la wakurugenzi namna ya kuhujumu chaguzi, Msimtetee.
 
Hii makala umeiandika kama Boniface Jacob!
 
Kwa ule uongeaji atakuwa ni single mother. Hakuna mwanaume ataishi na mwanamke jeuri vile maana kila siku atakuwa ana kushawishi kumbutua makofi na kumpa kichapo.
 
Mkurugenzi wa halmashauri anatakiwa aajiriwe na halmashauri.Kuteuliwa wakurugenzi na mamlaka nyingine ni dosari kubwa sana ya katiba tuliyo nayo.

Halmashauri ya Kinondoni iajiri Mkurugenzi? Wataajiri muuza madawa ya kulevya mwenzao!!! Utaratibu huu ni mzuri ili mradi madiwani wachaguliwe kwa haki na wananchi!! Matatizo yanakuja pale madiwani wote ni waccm na wanajuana wizi wao hivyo wanashindana!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…