Siri ya vipaji vya kuimba ‘bafuni’ wakati wa kuoga, hasa kwa watoto na watu wazima kama wapo

Siri ya vipaji vya kuimba ‘bafuni’ wakati wa kuoga, hasa kwa watoto na watu wazima kama wapo

Siku kama sina haraka basi ntaenda bafuni na simu kabisa kwa ajili ya kuskiliza music af nikiimba huko hua nakua na sauti flani amaizing balaa.
Tatzo nikitoka huko inakua kama sio mie dk chache zilizopita
Kuna auto-tune tofauti na nje Ya bafu.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Umenikumbusha mbali sana mkuu na kunifanya nicheke. Nadhani nilikuw mahiri sana katika hili. Sikumbuki niliacha acha vipi hii tabia, na wala sielew kwanini nilianza pia. Ila ilikuw nikiingia bafuni lazima niimbe.

Sikukatazwa na mzazi, japo sister angu mmoja alikuw ananiambia ninyamaze kila akisikia natoa ma-vocal huku naoga. Msala zaidi ulikuw nikitoka na sabuni masikioni au sijatakata...!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nini kuoga mzee kuna hali ya utulivu inakujia ukiwa maeneo hayo, ni kama zile idea zinakujia ukiwa unakata ‘kubwa’.... ukitoka hapo utaona kama zinakuja zinakataa.
 
Salamu kwenu Wanyabe!

Leo nimekuja na hili suala, nimekuwa nikiliona na kusikia siku nyingi japo sikuwahi kulipa umuhimu.

Basi kijana wangu mwenye kawaida ya kuimba kiustadi kila aingiapo maliwato ‘kuoga’ sio ile shughuli nyingine, leo ametia vokali kali sana kiasi cha kumkera mgeni wangu na akashindwa kujivunga.

Sijui yeye amepokeaje, kaonesha kutofurahishwa na ‘tabia’ hiyo... na kunishauri nimkanye mtoto asiimbe eti ‘chooni sio studio’.

Ndipo nikapata wasaa kulitafakari kwa upana wake, nikakumbuka kuwa sio watoto tu wanaopenda kuimba wakiwa kuoga, wapo baadhi ya watu wazima.

Hii ina maana gani.? Ni dalili ya nini, na haya ‘makatazo’ ya wazazi huenda vipaji vingi vimezimika kwa njia hiyo.?

Hebu tushirikishane tunaoshudia hii, na pia wale ambao ni mahodari wa kuimba, au wale ambao ‘walikoma’ watatupa sababu zao.

Karibuni.
Mimi nihodari sana wa kuimba choon.na wimbo wangu mkubwa ni “fight song”wa Rechal Platten.sasa kama kunawatu nawakera watulie tu maana hii tabia siwezi iacha.ni ya miaka nenda rudi
 
Back
Top Bottom