Siri za utajiri ambazo hamna mtu anayeweza kukwambia

Siri za utajiri ambazo hamna mtu anayeweza kukwambia

Jamaa amepuyanga tu mwanzo mpaka mwisho Hakuna lolote la maana la kujifunza,hovyo kbsa
 
Imebidi ni log in
Mtoa mada naomba nikukashfu HUJIELEWI pumbavu wahed kabisa.
Ndugu zangu watanzania wengi ni wajinga sana na hili linajidhihirisha kila siku.
 
Huu ujumbe ni special kwa ndugu Deborah9007 , maana nilikuwa kwenye mfungo, na Mungu akaniambia niongee na wana JamiiForums juu ya jambo hili.

Ili uwe tajiri na udumu katika utajiri wako, eidha wa nuruni au wa gizani ni lazima uwe na vitu viwili vikubwa.

1. MADHABAHU
2. AGANO.

Madhabahu ni sehemu ambayo unakutana na nguvu yako ya utajiri. Kama niguvu yako ni uchawi, basi hapa huwa ndipo unapatenga kwa ajili ya mambo yako, ila sisi ambao utajiri wetu umetoka kwa Mungu, MADHABAHU ni sehemu ambayo huwa nakutana na Mungu wangu, na huwa ninamtengea muda maalum. Muda huo na simu nazima kabisa, najikabidhi kikamilifu.

Namwita Mungu wangu, na huwa muda wetu wa kukutana madhabahuni ni saa tisa usiku hadi kumi na moja na nusu alfajiri kila siku.

Ninampa Mungu hesababu zangu za mapato na matumizi. Vitabu vyangu vya hesabu vinalala madhabahuni.

Namkabidhi Mungu mipango na ratiba zangu za asubuhi na siku nzima inayofuata.

MADHABAHU peke yake ndio inayoweza kukushindia vita zako zote. Kila vita yako ikabidhi madhabahu nayo vita itaisha.

2. AGANO
AGANO ni patano ambalo limebeba ahadi na sheria. Hamna tajiri ambaye hana AGANO. AGANO linakupa standing orders, do's and dont's. Ufanye nini na usifanye nini.

Kwenye agano hapa ndio kwenye masharti ya utajiri. Wengine wana majeraha yasiyopona. Hilo jeraha ndilo agano lenyewe, kwamba jeraha likipona tu utajiri umekwisha, hivyo ili uendelee kuwa tajiri ni lazima uhakikishe kidonda hakiponi.

Wengine wanaambiwa wasile vyakula fulani fulani, wengine wanaambiwa wasilale vitandani, walale kwenye sakafu mbichi iliyolowa maji.

Sisi wa nuruni pia tuna maagano yetu na aliyetutajirisha. Binafsi agano langu linatoka kitabu cha Yakobo 1:27 na Ufunuo wa Yohana 22:2.

Utajiri ni siri, siwezi kumwaga hapakila kitu kwani kwenye agano langu sitakiwi kuropoka hadi nipate ruhusa.
NB:-

CHAKULA CHA MADHABAHU NI SADAKA AMBAYO INAPATIKANA KWENYE AGANO.

KWENYE AGANO KAMA MLIKUBALIANA KILA IJUMAA YA MWANZO WA MWEZI UTATOA SADAKA YA NG'OMBE MZIMA, BASI USITOE MBUZI AU KUKU, KWANI UTAJIRI WAKO UTAPUKUTIKA.

SADAKA INA NGUVU SANA
Deborah9007 naamini kuna kitu umenasa.

hilo agano unafanyia chumbani kwako au kanisani??
Pia madhabahu unayomaanisha ni ile ya kanisani au ni ile unayojitengenezea ww
 
hilo agano unafanyia chumbani kwako au kanisani??
Pia madhabahu unayomaanisha ni ile ya kanisani au ni ile unayojitengenezea ww
Madhabahu ya kanisani sio madhabahu yako, wala huwezi kukuhanika pale
 
Biblia haijaandikwa kwa mafumbo imeandikwa kwa lugha nyepesi ya picha ili hata watoto wadogo waweze kuelewa. Biblia inatumia sana vielelezo vya picha (pictorial language) kuelezea ukweli flani na sio lugha ya kufumba. Kwanini wewe hutaki watu waelewe namna zako za kupata fedha kama njia zako sio za kishirikina?
Acha ubishi ujifunze. Biblia hasa Ufunuo ni mafumbo tupu.
 
Hizi

mambo ni assumption tu..
Ni wenye iman hizi ndio masikini kwelikweli africa na asia.. huko europe na america the more you work hard the more u earned..na wakija hapa kwetu kutalii tunawaona wote ni matajiri...

Siri ya utajiri ni nidhamu ya fedha + fanya kazi kwa bidii/kazi kwa maarifa hizo nyingine ni viini macho tu..
Baki na unachoamini.
 
Tunadanganyana tu,Utajiri wa mtu ni km kifo,kila mtu ana kifo chake inawezekana ukiwauliza wafu namna walivyokufa wanaweza wasieleze kiundani,ndivyo ilivyo hata kwenye ishu za utajiri.
 
Hiyo Madhabahu inapatikana kanisani ama wapi?
 
Skupingi kijana ata mie iyo Ratiba ndo nnayoifuata ila siku ya makutano ni alhamiss ,hua natenga muda nakutana Na yule wa sirini
 
Unakuta mtu ana kidonda kisichopona na kichafu, uwezo wa kukitibu anao ila anakubali kuteseka tu! Hayo ni maagano.
 
Nikikwambia utafaidika nini? Si bora uombe connection kama kuna sehemu unakwama nikusaidie wàtu watakaoweza kukuvusha
Chaka la Mamba utajiri ungekua hivyo watanzania wote wangekua matajiri, cha kusikitisha Nchi tajiri Ila wanaoikalia ni masikini
 
ulipo anza

"Siri za utajiri ambazo hamna mtu anayeweza kukwambia"​

nikamkumbuka ontario aka sir JEFF wa forex ili neno alilipenda sana sema yeye alikazania na vikolombwezo vya benki
 
Back
Top Bottom