Siridhiki na utendaji wa Baraza la mitihani la Taifa, NECTA

Siridhiki na utendaji wa Baraza la mitihani la Taifa, NECTA

Huna pakusemea hata wawe wazembe kiasi gani...
Tumaini langu halijawahi kuwa ktk kelele za wabunge hata siku moja. Mbunge aliyeamua kuacha shule baada ya kujua kusoma na kuandika anisaidie nini bungeni? Hata upinzani wawe 50% kwa ubora ule na maneno yale ya uongo kesho yake wanahama, what a shame!
 
Mwanao ameibuka na division FOUR basi unataka azingatiwe, ruksa kujitekenya mkuu!
 
Watoto mathematics katika masomo yote si kweye phy,chem,hata geogr, vihesabu vidogo vinawapiga Sana siku hizi .
Nafikiri ni lishe na ubovu wa walimu na mtazamo wa walimu hasa ngazi ya secondary.
Unakuta mtoto primary alikua vizuri namba badae anakua bomu la F
 
Mtihani wa mwisho uwekewe only 30 % yaani mwanafunzi akipata yote 100 % then it means ana 30 %. The remaining 70 % iwe ni mixture of assignments, presentations, group works, kazi za mikono, usomaji wa vitabu etc.... Kiufupi kutegemea sana mitihani ya mwisho kunaongeza tatizo la kukariri na wizi wa mitihani.
system yetu ya elimu ni ya waingereza/wamarekani ie western style education... huko huko kwenye system hii ndiko elimu bora iliko, discvoveries zote za dunia hii zinatoka huko, sasa utasemaje kuwa system hiyo haifai? sema sisi kuna mahali tunakosea......
 
Education sector is relative my friend

Wait and see the comments around here; as we keep on waiting, I have to take you in several concepts concerning what is so called Education;..
Huyu naye alipata division one
 
Kazi ya baraza ni kufanya post mortem tu. Then wanatoa ripoti mada walizoshindwa wanafunzi ni hizi, wizara ya elimu ndiyo inapaswa kuweka mikakati kuboresha. TAMISEMI wao wanahakikisha miundombinu iko sawa
 
Duniani kote huo ni utaratibu wa kawaida lazima uwatambua wanafunzi bora pamoja na shule zilizofanya vizuri zaidi
 
Kwanza kabisa nadhani NECTA na wizara wangeacha huu mtindo wa ku rank shule kwa ufaulu. Shule iliyofaulisha watoto wengi mara nyingi inakuwa regarded kama shule bora. Lakini ukweli ni kwamba ubora wa shule ni zaidi ya kufaulu wanafunzi. Ufaulu wa wanafunzi ni kigezo moja wapo tu..

Inawezekana ukawa sahihi lakini kazi ya NECTA ni kufanya tathmini kwa kuangalia kigezo cha mitihani na ndio maaana wanaitwa 'BARAZA LA MITIHANI TANZANIA'. Sasa kama unashauri zifanyike rank za shule kwa kuangalia vigezo vingine kama vile Usafi, michezo na nidhamu wanaweza kufanya watu wengine lakini acha NECTA wafanye kazi inayofanana na jina lao.
 
Mtihani wa mwisho uwekewe only 30 % yaani mwanafunzi akipata yote 100 % then it means ana 30 %. The remaining 70 % iwe ni mixture of assignments, presentations, group works, kazi za mikono, usomaji wa vitabu etc.... Kiufupi kutegemea sana mitihani ya mwisho kunaongeza tatizo la kukariri na wizi wa mitihani.
Kwa sasa mtihani wa mwisho una 70% na ni course work. Tatizo ninaloliona kwenye pendekezo lako ni pale ambapo shule X itafundisha topic moja na shule Y ikafundishwa topic 10 alafu wote wakatungiwa mitihani na walimu wao kwa kuzingatia topic walizosoma na ndio ziamue hiyo 70% na mtihani huo unasahihishwa na mwalimu huyo huyo!!!
 
Duniani kote huo ni utaratibu wa kawaida lazima uwatambua wanafunzi bora pamoja na shule zilizofanya vizuri zaidi
Sehemu nyingi duniani wamesha achana na utaratibu wa kushindanisha mashule. Finland wameondoa kabisa mitihani na ma test
 
Hakuna kitu kibaya Kama Uhuru wa maoni.
Kwa makusudi Mtu kwa makusudi hataki mitihani iwe kipimo Cha ufaulu/kujua
Kwa makusudi Mtu hataki shule zinazoogoza zitangazwe
......f..ck...Uhuru wa maonj
 
Nimeangalia matokeo ya kidato cha 4. Kwa ujumla wake wanafunzi wameshindwa hesabu. Je, Baarza limeleza sababu yake? Hapana! Wako bize kutueleza shule fulani imeongoza.

Baraza hili linalojiita NECTA ni shemu ya wizara ya Elimu. Miaka nenda rudi limeheshimika kwa kusimamia ubora wa mitihani na matokeo yake. Kwa maana nyingine, wanakagua kuona kama wizara mama, imetimiza wajibu wake wa kuwaelimisha watoto wetu. Tunachotaka ni elimu na siyo division 1,2,3,4. Hizo divisions ziwepo lakini kweli tunapozunguma na mtu wa division tuone hiyo division.

Hali haiko hivyo. Hao wote unaowaona division 1, baada ya miaka miwili ya form 5 na 6 unawakuta division 3, 4 na wengine sifuri! Inakuwaje? Hii ni kwa sababu NECTA wameweka sana suala la division kama kipimo cha ufahamu. Hata shule bora sasa ni ile yenye division 1 nyingi jambo ambalo naliona ni upuuzi tu!

Mtendaji mkuu wa NECTA tunaamini kisha sikia maoni kama haya, kwamba aache mtindo wa kututangazia shule ya kwanza, ya pili, nk. Kwa sababu haina maana yoyote zaidi ya kutangaza bishara za watu. Biashara hizi zinakuzwa na NECTA kwa kuzifanya divisions ndo elimu.

Imefikia hatua waalimi wanaiba mitihani ili tu wapate division 1 nyingi. Ubunifu umekuwa ni kujibu maswali madarasani ili wanafunzi wapate division 1. Huu ni upuuzi tuachieni hata division 4 ambaye anaonesha ukomavu na uwezo wa sekondari kuliko division 1 asiyeweza hata kuzungumza mbele za watu.
Kuna. M-NECTA mmoja alijenga Kijiji cha Maghorofa hapa Dar kwa Kuuza mitihani
 
Matangazo mengi Sasa hivi kwenye TV na Redio yanayohimiza kujiunga na form one hasa hizi English St somebody utasikia shule ilikuwa ya kwanza ki mkoa na ya Tatu kitaifa
 
Kuna. M-NECTA mmoja alijenga Kijiji cha Maghorofa hapa Dar kwa Kuuza mitihani
Bado biashara hizo zinaendelea. Kila mwaka wanajidai mitihani imeibiwa, hakuna kuibiwa, wanaigawa wenyewe kwa malipo.
 
Back
Top Bottom