Naby Keita
JF-Expert Member
- Oct 20, 2011
- 12,893
- 20,089
Halafu wanaoapishwa CCM workdone = 0Come 28 Oktoba
Chagua
Rais Chadema
Mbunge Chadema au ACT
Diwani Chadema au ACT
Usifanye makosa tena ya kuchagua matapeli.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Halafu wanaoapishwa CCM workdone = 0Come 28 Oktoba
Chagua
Rais Chadema
Mbunge Chadema au ACT
Diwani Chadema au ACT
Usifanye makosa tena ya kuchagua matapeli.
Wewe ndio humpendiNdiyo maana Jiwe ni Rais wa double standards, hili ndiyo tatizo kuu la kwanini hapendwi na watu timamu.
Majibu yote, Oct 28.Pumba na mahindi vitajulikana.SISI SIO WAJINGA
Ulipochukua tu madaraka ukaanza na kubomoa nyumba zetu katika bonde la Msimbazi. Bila huruma ukatuacha tumelala nje na watoto wetu. Ulidhani tutahama mjini lakini sisi bado tupo.
SISI SIO WAJINGA
Ulipokuwa unapanua barabara ya Ubungo - Kibaha ukabomoa nyumba zetu. Mbunge wetu Mnyika aliomba utulipe fidia ukampinga mbele yetu. Lengo lako tufe masikini lakini kwetu sisi maisha yanaendelea.
SISI SIO WAJINGA
Hukutaka tuwaone wawakirishi wetu, wakiwakirisha matatizo yetu Bungeni. Ulisema gharama za kurusha matangazo Live ni kubwa. Lakini leo hii unatuomba tufungue TBC tukuangalie ukikata mitaa kuomba kura.
SISI SIO WAJINGA
Baada ya kuwa tumefanya kazi kwa miaka 40 na tumebakiza miezi 3 tustaafu ukatufukuza kazi kwa kisingizio cha vyeti feki. Ulidhani tutakufa kwa njaa lakini Mungu anatupigani bado tunaishi.
SISI SIO WAJINGA
Tulipopata tetemeko la ardhi Watanzania wenzetu walituchangia pesa nyingi lakini wajanja wakatafuna. Ulipokuja Bukoba tulidhani utatutetea wanyonge badala yake ukatusimanga na kutukumbusha majanga ya Ukimwi, MV Bukoba kwamba yote yanatupiga sisi. Sasa nasikia unakuja kuomba kura kwetu! Je, ni kweli wewe utakanyaga Bukoba?
SISI SIO WAJINGA
Tulipokuwa tuna njaa. Njaa iliyotokana na ukame. Tukakuomba msahada wa chakula. Hii sio kwako tu, hata Serikali zilizopita zilitusaidia tulipokumbwa na ukame. Lakini ulitujibu kwa kejeli na kiburi cha hali ya juu. Eti tusikuombe chakula, Serikali haina shamba. Leo hii unakuja tena kuomba kura?
SISI SIO WAJINGA
Tukaenda Mtwara kulima korosho. Ukatuma askari wako wakatunyang'anya korosho halafu wakadai tuwaonyeshe mashamba yetu. Mbona wanaolima Mahindi, Pamba, Mpunga, n.k. hamuwaulizi mashamba yao? Ukasema hao askari watabangua korosho kwa meno ili kila Mtanzania atapata kilo 2, lakini hatujapata mgao. Sasa nasikia unakuja kuomba kura! Labda uishie Nangurukuru kwa sababu.
SISI SIO WAJINGA
Tumeitumikia nchi yetu kwa bidii kubwa. Tumefanya kazi kwa uzalendo mkubwa, huku tukipokea mishahara kidogo. Leo hii tumestaafu, tupo nyumbani miaka ikikatika. Lakini hutaki kutulipa mafao yetu. Bila aibu unakuja kutuomba kura tena?
#SISI_SIO_WAJINGA.
JPM aliposema "Watanzania sio wajinga",hakukuhesabu na wewe kwa kuwa wewe si Mtanzania na ni zaidi ya mjinga.Nyiee (mimi nitoe humo kwenye sisi) sipo kabisa
Nyiee (mimi nitoe humo kwenye sisi) sipo kabisa
Ni SISI sio NINYI.Ungesema wewe siyo mjinga. Badala ya kuongelea nafsi ya mtu.
Mimi sipo hapo kwenye “Sisi”