Sisi Waafrika historia yetu iko wapo kabla ya ujio wa Wamisionari na Waarabu?

Lakini Mansa Musa, ambaye pia anajulikana kama Musa I wa Mali, alikuwa mtawala wa himaya ya Mali kuanzia mwaka wa 1312 BK hadi 1337 BK. Alikuwa maarufu kwa utajiri wake mkubwa na safari yake ya hija kwenda Mecca mwaka wa 1324 BK, ambayo ilimfanya kuwa maarufu katika ulimwengu wa Kiislamu na Ulaya. Kwa hiyo, Mansa Musa alikuwepo katika karne ya 14

Kwa maana hii ukiachana na mansa mussa lazima kuna waafrika wengine maarufu na wenye pesa Pennine ukute kupita hata Mussa, je historia zao ziko wap

Kwa vyovyote naamini Mansa mussa anazungumziwa uwepo wake kwakuwa tu alienda kuvisit mecca. So ukosema tulikuwa hatuvai nguo ntakushangaa.
 
Je huyo methiopia aliubiliwa na nani? na alibatizwa na nani?
Kwa vyovyote mzungu alimbadilisha kwenye kitu ambacho yeye na jamii yake iliamini. Swali linarudi pale pale sisi waafrika historia yetu iko wapi
Niliandika hivi kumaanisha Muethiopia aliyekuwa ameenda kuhiji Yerusalem, alihubiriwa na Filipo aliyekuwa Myahudi (middle eastern, sio mzungu). ni kweli Africa tulikuwa na dini zetu ila Ukristo haukuletwa kwa mara ya kwanza na wakoloni au wamisionari wa kizungu, zamani hizo hata Misri ilikua ya Kikristo, Uturuki ilikuwa ya Kikristo, na tarishi wa Ethiopia alihubiriwa na Filipo akabatizwa akaja na ukristo Africa miaka kenda kabla hata ukoloni haujaja africa.
 
Nashukuru kwa views zako lakini bado hata wewe ni kama mimi ni vile hujataka kujua kuwa hata ww haujui, kwanini? kwa sababu

1. Mansa mussa aliexist karne ya kumi 14 kwenye utawala wa Mali, nachotaka kujua miaka 300BC hapo mali palikuwaje? Hamna unachokijua kubali.
Mansa mussa anatajwa kuwa moja ya matajiri wakubwa kuwahi kuwepo duniani, umaarufu huu anaupata kwakuwa tu alienda kuvisit Msikiti wa Mecca hichi ndicho kinampa umaarufu. Je umewahi kujiuliza kuwa hakukuwa na matajiri na watawala wengine kama yeye? Kwanini kwenye historia hawapo?

2. Timbuktu University ni chuo kilicho kuwepo kuanzia karne ya 12 na kimepata umaarufu wake katika karne ya 15-16. Chuo hiki kilikuwa kinaunganisha misikiti mitatu katika Mji wa Timbuktu nchini mali, kilikuwa ni sehemu muhimu katika Enzi hizo. Chuo hiki kilikuwa kituo cha elimu ya utamaduni wa kiislamu na kilivutia wananzuoni wengi kutoka sehemu mbalimbali za dunia ya kiislamu.

Uislamu uliingia nchini Mali karibu na mwisho wa karne ya 9 na mwanzo wa karne ya 10. Ueneaji wa Uislamu katika eneo hilo ulikuwa ni matokeo ya biashara za trans-Sahara na mwingiliano wa kitamaduni kati ya watu wa Afrika Magharibi na wafanyabiashara Waislamu kutoka Afrika Kaskazini.

"nikurudishe nyuma karne ya 8 uislamu uliingiaje afrika kaskazini"
Uislamu uliingia Afrika Magharibi kuanzia karne ya 8. Wafanyabiashara Waislamu kutoka Bara Arab, India, na Asia walifika katika pwani ya Afrika Magharibi na kuanza kufundisha Uislamu kwa wenyeji. Kufikia karne ya 9, Uislamu ulikuwa umeenea zaidi katika eneo hilo, hasa kupitia biashara na uanzishwaji wa himaya kama vile Dola la Ghana. Uislamu ulileta pamoja na imani, muundo wa kisiasa na kisheria katika maeneo yaliyokuwa chini ya udhibiti wa Waislamu.
Swali linakuja pale kabla ya karne ya 5 au 400BC waafrika tulikuwa na maisha gani? Historia yetu iko wapi?

3. Ukisema Mwanafalsafa mkubwa duniani Mwanafunzi wa Socrates, Plato kuwa amesoma Alexandria University nakataa kwa sababu hicho chuo kimeanza miaka ya 1938 karne ya 20 na Plato alikuwepo miaka ya 300KK Huko. PLATO alitembelea misri kati ya 380kk Hii ilikuwa ni baada ya kufiwa na mwalimu wake Socrates. Plato alipenda kuzunguka sehemu mbali mbali duniani kujifunza falsafa na tamaduni za watu wengine ikiwemo Misri na Inasemekana kwamba alijifunza kutoka kwa makuhani wa Misri na alivutiwa na hekima yao na maarifa ya kijiometri na kiastronomia.

4. Ukisema wayahudi walikuwa wanaasili ya Afrika nakataa kwa sababu Wayahudi wanahistoria yao na walikuwa na Dini yao ambayo iliitwa Yahwism.
Yahwism
ilikuwa ni dini ya waislaeli wa zamani hasa katika maeneo ya Seir, Edom, Paran, na Teman, na baadaye na Kanaani ambapo kwa sasa ni eneo la Islael na Palestine.
Yahwism ilikuwa dini ya Waisraeli wa zamani na ilikuwa hasa polytheistic kwa asili, ikiwa na pantheon ya miungu mbalimbali. Yahweh alikuwa mungu mkuu katika pantheon hii na aliheshimiwa kama mungu wa kitaifa wa ufalme wa Israeli na Yuda 1-3 BC.
Kwa mujibu wa wataalamu, Yahwism ilipitia mabadiliko kadhaa na kujikita zaidi katika monolatry ya Yahweh, ambapo Yahweh alitambuliwa kama mungu mkuu na mwingine yeyote alipunguzwa hadhi. Mabadiliko haya ya kidini yalianza kujitokeza kwa kiasi kikubwa wakati wa Ufalme wa Muungano wa Israeli na Yuda na yaliendelea kusambaa kwa watu wengi wakati wa machafuko ya kisiasa ya karne ya 7 na 6 BC. Kufikia mwisho wa kufungwa kwa Babeli, Yahwism ilianza kugeuka kutoka kwenye polytheism na kuelekea monotheism, ambapo Yahweh alitangazwa kama mungu muumbaji na pekee anayestahili kuabudiwa. Baada ya mwisho wa kufungwa kwa Babeli na kuanzishwa kwa Yehud Medinata katika karne ya 4 BC, Yahwism ilijikusanya na kuwa Uyahudi wa Hekalu la Pili, ambao kutoka hapo dini za kisasa za Kiyahudi na Usamaria, pamoja na dini za Abrahamu za Ukristo na Uislamu, zilijitokeza.
Utafiti wa DNA ya kale umebaini kwamba kulikuwa na mchanganyiko wa watu katika eneo la Levanti, ambapo watu wenye asili kutoka maeneo kama Anatolia na Iran walichangia kwa kiasi kikubwa katika muundo wa kijenetiki wa watu wa eneo hilo.
Kwa maana hii inaonesha Wahweh ( Mungu mmoja) alikuwa mungu wa Wayahudi, tangu kipindi cha Zama za kati na before christ.
Mungu wa waafrika yuko wapi?, aliitwaje?
JE UNATHUBUTUJE KUSEMA WAYAHUDI WALIKUWA WEUSI na wanahistoria yao? Nipe ushahidi unaoonesha Myahudi alikuwa Mweusi?

5. Kama yesu na wahusika wengine kwenye Bible walikuwa weusi je kwanini Dini ya kikristo ilianza kusambazwa na wazungu?

Kwanini waafrika wao wenyewe wasingepambana kusambaza ukristo wao?

Binadamu wa kwanza alitoka afrika ndio je Mzungu alitokea wapi? Vipi kuhusu wahindi wajapani, Korea China?

Kama adamu na Hawa walikuwa waafrika je spishi ya hizo race nyingine walitokea wapi?
Inawezekana Mwafrika kumzaa Mchina?

Mimi na elimu yangu ndogo hujanishawishi, njoo tena
 
Sisi ndio wazawa halisi wa hapa na kila kitu tulikifanya kwa ukubwa wafanyavyo n kopi ya marudio ya tulivyovifanya.

Wanafanya kila hila tusijielewe ila uongo haudumu muda utasema.
 
Putin ameshatangazia umma kwamba yesu alikua mweusi...baada ya kupata nakala kwenye sanduku la kale lenye picha za mitume na manabii wa kale weusi.

Hii kwangu pia sio ishu kubwa sababu hii ameitangaza kwenye hili vuguvugu la vita yake na miamba ya dunia( wameshajua sisi hatuna misimamo linapokuja suala la imani) Na kitu muhimu katika kutawala jamii nyingine zinazopokea pokea ( Africans).

Kuhusu dini kusambazwa na mzungu hasa huku kwetu ni lengo la kututawala,kutudumaza kifikra Ili iwe rahisi kufanya mambo yao.( Un equal exchange, slavery, colonialism,neo colonialism na sasa globalization ( papa kashatoa baraka kwa wapenzi wa jinsia moja).

Binadamu ( haijalishi race gani)ana level ya maendeleo kwa wakati fulani na eneo fulani.
1.Zama za kale.
2.Zama za Kati.
3.Zama za mwisho.

Kila zama zina vipengele vyake nimeandika kwa kifuni nikimaanisha ya kwamba mpaka karne ya 14( nakubali kusahihishwa )jamii zote tulikua sawa kwenye maendeleo ila mabadiliko yalitokea kwa jamii ya wazungu kufanya mapinduzi ya kila sector ya maisha ya mwanadamu.Hivyo kuwalazimu kutafuta maeneo mapya ya kuweza kukidhi haja zao.
Ndio mbinu mbalimbali zikatumika kutushawishi sisi dhaifu mathalani kutumia(dini) na azikupokelewa kama tunavyojadili hapa babu zetu waliuawa,walikatwa mikono,miguu,walihasiwa,viwanda vyao vya kufua vyuma vilichakazwa.

Nimalizie kwa kusema kwamba kama wasingetuvamia tungeendelea kuishi bila kuingiliwa na wazungu/waarabu na sisi tungekua na uchumi imara, technology kubwa,utawala bora,elimu nzuri,sanaa bora,urembo na mengine mengi.
 
Kuna kitabu cha ramani za kale(atlas) za wazungu kinaitwa Peruplus of the ethrean sea. Kinatambua nchi nyingi. Hata Tanzania walisafiri na kuukuta mji unaitwa Raphta na Azania
Unacho mkuu ushare nasi hapa.
 
Haya mambo ya Yesu yalisukwa tu, hakuna Mungu anaetoa kafara. Walitumia mbinu za kimaendeleo ili tukubali na kututishia na moto wa milele.
 
Kuna kitabu cha ramani za kale(atlas) za wazungu kinaitwa Peruplus of the ethrean sea. Kinatambua nchi nyingi. Hata Tanzania walisafiri na kuukuta mji unaitwa Raphta na Azania
hiyo rapta si ndo ipo kwenye maji now days
 
Jina tuu unalotumia linasadifu namna ulivyo so lazima umtetee huyo bwana wako wa kiyahudi
 
Kuna sababu nyingi sana kwanini baadhi ya maeneo ya maeneo Duniani ikiwemo Afrika hayana historia za simulizi za kale kama mengine

Kwanza kabisa ni MAANDISHI
Maandishi hutunza historia kwa muda mrefu zaidi kuliko hadithi za kusimuliana kizazi hadi kizazi
Waafrika ukiondoa Misri tulichelewa sana kujua kuhifadhi kumbukumbu kwenye maandishi hadi miaka ya hivi karibuni wazungu na waarabu walipokuja
 
The Real...
Napenda kwanza kusahihisha kichwa cha uzi huu.
The Real...
Kwanza napenda kusahihisha kichwa cha uzi huu: ''Sisi Waafrika historia yetu iko wapi kabla ya ujia wa Wamisionari na Waarabu?''

Ilitakiwa iwe ''kabla ya ujio wa Uislam na Ukristo?''

Hii inafuata ''sequence'' yaani kilichotangulia kinakuwa mwanzo kisha kilichofuatia.

Lakini kichwa cha habari kingeweza pia kuwa, ''Kabla ujia wa Waarabu na Wamishionari.''

Umetaja Wamishionari ambao ni Wakristo kisha ukataja Waarabu.
Ilitakiwa iwe, ''Kabla ya Uislam na Ukristo.''

NImeandika kitabu, ''Rajabu Ibrahim Kirama Jemedari wa Vita Kuwa Jemedari wa Uislam.''

Kitabu hiki nimeandika kutokana na kuhadithiwa historia ya Wachagga na Bi, Hawa bint Rajabu, mtoto wa Rajabu Ibrahim Kirama na mjukuu wa Mangi Abdieli Shangali wa Machame.

Bi Hawa kanifahamisha kuwa historia hii aliyokuwa ananieleza imekuwa katika ukoo wao kwa takriban miaka 200 ikitoka kutoka kizazi kimoja kwenda kingine kwa kusomeshana kwa kuhadithia hadi walipoingia Wamishionari na kufungua shule.

Wamishionari wakaanza utafiti wa kutaka kujua historia ya Wachagga.

Wachagga toka zama hizo walijihisi na kujiona ni taifa na ardhi yao yote ni nchi kamili.
Nchi yenye mipaka yake ya kueleweka. Wenye lugha moja lau kama makabila yao ni mengi na yakiishi sehemu mbalimbali chini ya Mlima Kilimanjaro.

Historia ya Wachagga imeandikwa kwenye upeo wa hali ya juu na Charles Dundas kiasi mimi nilistaajabu.

Nilijiuliza huyu Mzungu kajuaje yote haya?

Jibu lilikuwa jepesi sana.

Mwandishi Charles Dundas kayajua yote haya kwa kusomeshwa na Wachagga wenyewe.

Wachagga hawakuwa wameandika popote historia hii.

Historia hii ilikuwa imehifadhiwa kwenye vichwa vyao.

Kizazi hadi kizazi hadi kumfikia Charles Dundas, Ukristo na ukoloni ulipoingia Uchaggani.

Kwa kumpenda Charles Dundas Wachagga wakampa jina Wasaoye-o-Wachagga, yaani Mzee wa Kichagga.

Historia ya Muro Mboyo aliyeishi Machame katika miaka ya katikati ya karne ya 19 imeishi katika simulizi za ukoo wake unaofahamika kama ukoo wa Nkya, ikipokelewa kutoka kizazi kimoja hadi kizazi kingine kwa miaka inayofikia 200.

Historia hii haikupata kuandikwa popote kwa nia ya kuwa historia hiyo inaandikwa ili ije kusomwa.

Hata hivyo mtoto wake, Kirama Mboyo ameacha utajiri mkubwa wa nyaraka zilizoandikwa kwa hati ya mkono na nyingine zimepigwa chapa zinozoeleza historia ya babu zake waliomtangulia kiasi cha miaka 100 nyuma na kueleza pia historia yake mwenyewe pale ilipoingia karne ya 20.

Baadhi ya nyaraka hizi ziko katika mfano wa barua, taarifa na maelezo ya kawaida zina tarehe na zipo nyingine hazina tarehe wala jina la mwandishi.

Muhimu ni kuwa kumbukumbu hizi zinaeleza historia muhimu sana ya takriban miaka 200 nyuma ya Wachagga wa Machame na sehemu nyingine za jirani ambao walikuja kuwa Waislamu wa kwanza Kilimanjaro.

Msikiti wa kwanza Moshi Mjini Masjid Riyadha ulijengwa mwaka wa 1899.

Nahitimisha kwa kusema kuwa Waarabu na Uislam ulikuwapo Pwani ya Afrika ya Mashariki kwa zaidi ya miaka 1000 na Pwani ya Afrika ya Mashariki ina historia kubwa inayogusa mataifa mengi.


 
Andiko lenye matumizi mazuri ya akili!! Hongera sana Ndugu!!

Nimependa uandishi wako wenye aina ya pekee kabisa, mizaha na buruduni Lakini dhamiri Yako imetufikia.


1-Dunia imezalisha wajinga wenye ujinga wa Hiyari, wao hawataki kujua matukio halisi ya ulimwengu huu,tangu mwaka 1 AD mpka leo Hii 2024, Lakini hata kabla ya mwaka moja kulikuwa na maisha mengine.

2-Hivi vitabu wiwili vinavyoaminiwa na watu wengi, vyenyewe siyo vitabu vya historia Bali ni vitabu vya fasihi simulizi, kwa udogo wa maarifa yetu tumevibadili vitabu hivyo kama vitabu vya historia ya ulimwengu..(none sense) tunaendelea kubuluzwa.

3-Historia ya Dini HIZI,imepotoshwa makusudi tu Ili wafuasi wawe wengi waziendee, wazitii, wazitumikie, lengo lao kubwa ni kushikilia UCHUMI and they won this battle, waarabu na wazungu wachache wao they real know wanachofanya, ila mazuzu wengi hawajui, haya mazuzu ni ya RANGI zote, kabila zote, na mataifa yote. Wapo tu.

4-Dini zote Tatu kubwa. Christianity, Muslim, Judaism, Asili ya mafundisho Yao ni Afrika ya Leo na baadhi ya maeneo ya Asia, ambayo kale eneo lote Hilo lilikaliwa na MTU mweusi, MTU pekee aliyeleta mchuzi juu ni mgiriki, kazi ya kwanza ilikuwa ni kubadilisha majina ya maeneo na vitu, Ili kumbukumbu zipotee,Lakini wanasahau kwamba Ardhi na baadhi ya kumbukumbu kamwe haziwezi kufutika ,Zipo na zinaendelea kuwepo,uamzi ni wako na akili Yako.

5-40,000 yrs back kulikuwa hakuna MTU mweupe duniani,...anzia hapo. Soma piramid za kemet (Misri ya leo) hapa juu sudani, michoro ya kondoa, isimila na kwingine kwingi ,utaona kwamba this guy trying to play us.

6- Vitabu vyao vyote fasihi zao hazilandani na maeneo Yao, hadithi zinaoana kimazingira na Afrika na ndiyo hasa ilipaswa kuwa,lkn wandishi wa hizi fasihi walitumia miaka mingi sana kuaminisha watu kwa nguvu fasihi zao.

NIMALIZE HIVI::: Naamini MUNGU Lakini siamini Mungu huyu mwenye itikadi tofauti, Naamini MUNGU aliyopo ndani yangu na yule aishiye Katika Asili, maana sheria za Asili zinatulinda sote kwa utu wetu kwa usawa na UPENDO.
 
Kutokana na ujinga au kutokufahamu walikuwa wakiabudu mizimu ..na hao wajinga bado wapo mpaka sasa
 
Mkuu kuna msemo unasema "Kila amlipaye mpiga zumari hutaka kuchezewa wimbo wake", kwa maana hiyo huwezi kukuta simulizi za mashujaa wa Afrika katika vitabu vilivyoandikwa kusimulia tamaduni za wazungu.
Tunazo historia za Mashujaa wa Afrika sema ni vile tu hazipati muda wa kutosha kuzungumziwa katika majukwaa ya sasa, pia kuna changamoto ya kupata historia ya pamoja ya mashujaa hawa kwa wakati mmoja kutokana na ukweli kwamba kila nchi na jamii huwaelezea watu wao pekee kutokana na kukosekana kwa taarifa za ndani za mashujaa wa upande mwingine.
Kwa mfano, ukifika makumbusho ya Mtemi Mirambo utapata historia ya Mtemi Mirambo pekee na kabila lake kwa ujumla na sio rahisi kukuta katika makumbusho hayo kupata historia ya ushujaa wa Mtwa Mkwa mpaka pengine ukatembelee makumbusho ya Kalenga.
Ila angalau kwasasa hata mitaala inaboreshwa watoto wanajikita kusoma historia ya Tanzania kwa namna ya pekee tofauti na hapo awali inaweza saidia kuwa na uelewa wa kutosha kwa vijana wetu kulifahamu vyema Taifa lao pamoja na mashujaa na wakombozi wa Taifa hili
 
Labda tumelogwa, tulishangilia kama mazuzu, tukapuuza jadi yetu na kutukuza yao. Mababu zetu wamekasirika ndio maana maafa ni mengi Africa. Katika Ukristu angalia tunavyowatukuza watakatifu wa kizungu.
 
Africa Tradition was wiped away and Africans were taught to believe that anything tradition means Evil.

Biblia na Quran ni takataka tu.

Waafrika wanapaswa kuachana na hekaya hizi zisizo na kichwa wala miguu.

Ni muda wa waafrika kuamka.
waamke wapi acha uongo.
 
Wafrika hatukuwa na historiabyeyote ya maana..
Tulikuwa hatujengi, hatuna technology yeyotebya maana kwa mtu mwenye akili timamu kuadopt.

Jamii znyingi za kiafrika tulikuwa tunaishi kama unavyoona baadhi ya makabila ambayo hata sisi yunaona hawajastalabika kama wamasai wale wa ndani ndani kabisa , wahadizabe, wamang'ati na jamii zingine kama hizo.

Wafrika walikuwa wanaishi porini, mapangoni, kwenye majabari wakiwinda na wanyama , atakaye muwahi mwenzake anageuzwa chakula.

Ndiomaan bhata idadi ya watu ilikuwa ndogo, wengi walikufa wa changamoto za kimaisha kuchanyanyikana na wanyama..
Hicho ndio kulipelekea kutokuwa na historia yeyote ya maana kwa jamii nyingi za kiafrika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…