Goo morning wana Jf!
Watanzania huwa tunatabia ya kuwaongezea ugonjwa wagonjwa..Yaani mtu anaweza akawa anaugua kabisa na dalili zote tunaziona lakini ndio kwanza tunaendelea kumgeuza kiburudisho au kivutio..
Huyu Mama anaye jiita Sister Fei ni mgonjwa kabisa na ana hitaji msaada kabisa na kinacho shangaza badala ya kumsaidia watu wana mgeuza kivutio au kituko...Bado najiuliza watoto wa huyu Mama wako wapi kumsaidia Mama yao hata kumpeleka hospitali?
Ndugu wa huyu Mama wako wapi kumsaidia ndugu yao anaugua kabisa?
Ndugu wa huyu kijana anayeonekana na mgonjwa wako wapi kumshauri wampeleke hospitali?
Wazazi wa huyu kijana wako wapi?
Huyu Mama anahitaji msaada asaidiwe haraka.
Muda huongea lakini ukweli ni kwamba huyu Mama anaumwa kabisa ni muda utathibitisha...
View attachment 847756View attachment 847757View attachment 847758
Sent using
Jamii Forums mobile app