Sitaisahau siku lift ya ghorofa ilipofail/kwama katikati ya safari nikiwa peke yangu

Sitaisahau siku lift ya ghorofa ilipofail/kwama katikati ya safari nikiwa peke yangu

Daah pale Benjamin mkapa tower, nilikuwa nnaelekea gorofa ya 10 TPDC tulivyofika ya 8 ikagoma siyo sababu ya umeme lakini...baada ya kama dakika kumi ikaanza kwenda juu kwa kasi ya ajabu, kufika juu ikashuka chini kwa kasi ya ajabu afu ikapanda tena mpaka gorofa ya 9 kwa speed ile ile, aisee nilijuta kuapanda ile lift kwa Siku hiyo,

Na pia lift za jengo la ushirika la zamani
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Mecheka sana jamani!!! Khaaaa, ilikuwaje ikasimama sasa
 
Acha kabisa lakini wakati mwingine hakuna jinsi fikiria unaenda ghorofa ya 20. Kuna moja nilisikia zile waya ambazo zinaishikilia zilikatika ikiwa na watu ndani basi ikaporomoka kufika chini kuna watu walikufa na wengine kuvunjika miguu.
Duuuh hatari acha nibaki tu na ushamba wangu teh....
Siku nlienda kujifungua nna uchungu nesi ananambia tupande lift kwenda leba, nkamwambia hapana sipandi lift mie napanda ngazi, anauliza mara mbili utaweza kupanda namwambia lift sipandi....wala sikupanda
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hahahaha ushikwe kwa nguvu. Pole mwanetu
Kuna siku hiyo hadi nilijicheka yani nipo na mtu ananivuta twende kwenye lift mie nmesimama kwenye ngazi, mkono mmoja nimeshika kingo za ngazi mkono mmoja ananivuta afu anashout twendeee nami nmekomaa siendii napanda ngazi, waliokua wanapita hawana mbavu, sikupanda lift mie
 
Kuna siku hiyo hadi nilijicheka yani nipo na mtu ananivuta twende kwenye lift mie nmesimama kwenye ngazi, mkono mmoja nimeshika kingo za ngazi mkono mmoja ananivuta afu anashout twendeee nami nmekomaa siendii napanda ngazi, waliokua wanapita hawana mbavu, sikupanda lift mie
Hahahaaaaa
 
Mh! Weye una msimamo thabiti. Mie siku hizi huzikagua kwanza kama inaelekea imechoka choka basi niko radhi nipande ngazi.

Duuuh hatari acha nibaki tu na ushamba wangu teh....
Siku nlienda kujifungua nna uchungu nesi ananambia tupande lift kwenda leba, nkamwambia hapana sipandi lift mie napanda ngazi, anauliza mara mbili utaweza kupanda namwambia lift sipandi....wala sikupanda
 
Ilikua Udsm iyo hall 5,jamaa yangu floor ya 8 ndo anakaa sasa katoka pindi/lecture anarudi room kupumzika wako kama wa5 ndani ya lift. Isizime floor ya 4 aiseeee,jamaa anantumia text mwanangu leo nakufa lift imezima,mi nikajua utani. Jamaa wamekosa hewa,kiu zimewashika kuna jamaa alikua ametoka chini kukinga maji ya kuoga na ndoo ya chooni mbona walikunywa kama wanakunywa kilimanjaro maana fundi anaeOperate kupigiwa simu yupo kigamboni. Jamaa wametoka after 2 hours wamelegea kama mlenda jasho linawatoka,mmoja uyo alianza kumlilia mamaake kwenye simu,mama akatoka kazini adi kaja eneo la tukio.Jamaa yangu hadi tunamaliza mwaka wa ule hakuwahi panda lift na akahamaga kabisa hall 5. Sasa imagine likuzimikieni alafu unaenda kwenye mtihani na simu umeacha.
Sio mambo mazuri kukutokea koz inakupima kikwelikweli,naomba mungu isije kunitokea.
 
Mimi Napenda kupanda na sijawahi kunasa
 
mm lifti siipendi maana nikipanda najihisi kudondoka afu tumbo linaniumaga sana kama linataka kudondoka vile
 
Sijawahi kukutana na kashikashi kama hizo ila mara ya kwanza naenda kupanda lift, wazee nyumbani walinielekeza kama naenda kufanya mtihani. Mama anasema lake mzee anasema hili, nilipoingia tu nikafanya utundu mmoja nahis ni hatari mno. Nliruka ruka nikaona inanesa nesa.
 
Duuuh hatari acha nibaki tu na ushamba wangu teh....
Siku nlienda kujifungua nna uchungu nesi ananambia tupande lift kwenda leba, nkamwambia hapana sipandi lift mie napanda ngazi, anauliza mara mbili utaweza kupanda namwambia lift sipandi....wala sikupanda
Duh? Wewe kiboko!
 
Back
Top Bottom