Sitasahau niliposimama kwenye treni kutoka Kigoma hadi Singida

Sitasahau niliposimama kwenye treni kutoka Kigoma hadi Singida

LA7

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2019
Posts
655
Reaction score
2,369
Ndugu zangu huu usafiri ni mzuri Ila usipande ile treni yetu ya wanyonge japo gharama zimepishana kidogo, mfano kutoka Tabora mpaka Kigoma ya wanyonge ni 12500 na ile express ni 16100 kwa wakati huo ila sijajua kwa sasa.

Ilikuwa hivi; wakati nasafari kutoka Kigoma kwenda Singida nilikuta train ndio linakaribia kuondoka sasa nikaingia tu nikiamini nitakatia tu tiketi ndani ya tren.

Jamaa wakaja wakanikatia tiketi ila hawakuniandikia siti, japo siti zilikuwepo. Sasa baadae si nikanyanyuliwa na wenye siti ikabidi nisimame tu tiketi yangu ilikuwa nishukie Manyoni ila ikanibidi tu nishukie Tabora maana sio kwa mateso hayo.

Ushauri wangu kwa TRC; waongeze usalama kwenye treni maana mule kuna askari na bunduki kabisa lakini abiria wanaibiwa tu tena kwa kukwapuliwa na vibaka. Jambo hilo huwezi likuta kwenye express, usafiri huo haueleweki kabisa saa ya kuondoka na saa ya kufika unakokwenda.

Watu kukaa njiani na mizigo ndani ya mabehewa, kila kituo kiwe na wakatisha tiketi kuepuka kuwapiga watu faini wakati wamepandia kituoni ila kituo hakiuzi tiketi.

Nimemaliza ya kwangu, ni hayo tu.
 
Umenikumbusha mwaka jana nilisimama kutoka njombe (makambako) mpaka Dar es Salaam....daah aseee sisahau miguu kidogo itself maji daaah
 
Kidogo miguu ikatemoto nyieee bongo ni hovyo sana tren zake...
 
Umenikumbusha nishawahi kusimama kutoka Tabora mpaka mpanda. Treni ilitoka Tabora saa sita usiku, tulikuwa tumebanana vibaya ukisimama huwezi hata kusogeza mguu, nilisinzia nimesimama sababu siwezi anguka, hakuna nafasi ya kuanguka. Wakati wa kupanda vibaka wanasimama mlangoni, wanabana nafasi basi watu wanaibiwa vibaya mno. Mara huyu aingie mfuko umechanwa na wembe na pesa imeenda.

Huu usafiri huwa wanatumia watu wa hali ya chini na kipindi hicho hapakuwa na lami Tabora - Mpanda. Ile safari tulikuwa wawili na jamaa yangu tukiwa wadogo, tulikuwa tunalala kwa kupokezana ili tusiibiwe. Kama ulivyosema, halina muda maalumu wa kuondoka wala kufika. Huo siyo usafiri bora lori.
 
Nimepanda treni sana mpaka mwaka 2013, aisee nilikuja kufahamu treni hapa bongo ni kwa walala hoi. Yaani siwezi panda treni hata kwa bahati mbaya.

Kuna ile watu kujaa mlangoni, sasa usiombe mlango ukiwa unafunguliwa ni kama daladala maana mtabanana mpaka mlango ufunguke.
 
Bwana Mughabho Pole Sana Ulibeba Ugali Wa Loe Ambao Unakaa Wiki Bila Kuharibika
 
Back
Top Bottom