Sitasahau tulivyonunua TV na deki mwaka 1989, hakuna kuigusa na inalala chumbani

1989 rambo, remote, dishi hata tv hazikuwa zinauzwa tz, japo nlikuwa mdogo sana ila hivi vitu sikuwahi kuviona dar. Waliokuwa na tv ni wale waliokuwa wanaenda kusoma nje wanarudi na tv. Pia zilikuwa kama redio unanyonga kutafuta stesheni
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha

Najua ulikuwa hutarajiwi kuja katika ulimwengu huu.

Watoto wa miaka ya 2000 mmekuta kila kitu shwari.

Enzi zetu mambo yalikuwa ni mbombo ngafu [emoji14] [emoji14]

Karma pita uku pia
Afu acha masihara ujue, 89 wazazi walikua wanaazimisha anniversary ya 20 yrs of marriage and I'm their firstborn so jiulize nilikua na umri gani[emoji3][emoji3]. Watu tumekula chumvi mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu Uzi umenichekesha sana dah,
Cha kujifunza, "Bibi wa leo alikua bint wa Jana"
[emoji85]Nilikua nna mwaka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh umenikumbusha mbali sana....nyie mlikuwa wa kishua sana....miaka hiyo mi nakumbuka mzee wangu (RIP) alikuwa anarudi na ile mashine ya picha za mgando kama projector flani alikuwa anaiazima ofisini kwao....lakini alikuwa mkali sana...yaani mtu haruhusiwi kuisogelea ....kwa hiyo akipress inatokea picha ukutani mara picha ya mnyama amesimama , mara mgambo anaruka,mara mtu kapanda farasi..hapo tunakuwa tumetulia kimya sana na madirisha yamefungwa..kila picha ikitokea anasubiri kama dk 3 halafu anauliza tayari nitoe?..nakumbuka watu wallikuwa wanajaa kichizi home wakishajua mshua amerudi na alikuwa anaifungia chumbani kwake...baada ya muda wa siku kadhaa alikuwa anairudisha ofisini kwake aliko i azima....hapo tulikuwa tuna mind kichizi.....kipindi hicho nakumbuka ukitaka kuona video chogo lazima uende ukumbi wa CCM na ilikuwa lazima ulipie...hapo ndipo palikuwa pagumu....zamani raha sana
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ hapo kwenye kula mkofi tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…