Sitosahau yaliyonipata kijijini Kwamsisi

Sitosahau yaliyonipata kijijini Kwamsisi

SEHEMU YA 7

Niliporudi kutoka kwenye kuupumzisha mwili sikumkuta Sitti pale alipokuwa amekaa. Nilijaribu kumuulizia ila kila niliyemuuliza alisema hajawahi kuona mtu kama huyo, kwani niliwalezea kwa jinsi alivyokuwa amevaa na kwa jinsi alivyokuwa akionekana, walibaki kunishangaa tu niliogopa kurudi nyumbani bila yeye nilikaa pale msibani mpaka watu wote wakamalizika kuondoka. Nami nikakata shauri la kuondoka eneo lile la tukio nilipokuwa nikiondoka nilisikia sauti ya mtu akiniita kwa jina langu ilikuwa ni sauti ya wana Kingalu. "Mwanangu Soka!" niligeuka nikamfuata.

Nilimtazama mwanamama huyu aliyekuwa amesha zeeka haswa ngozi yake iliyokunjamana na sura yake kukosa nuru. "Bila shaka unamtafuta rafiki yako Sitti?" aliniuliza. "Umejuaje mama, ni kweli namtafuta kwa maana ninajua asingeweza kuondoka bila ya kuniaga." "Unaikumbuka hii?" ananionyesha khanga aliyokuwa amejitanda. "Imeokotwa huko mtoni walipokwenda kuteka maji." (ni kawaida kwa wanawake kushiriki kazi kwenye eneo la msiba), "Kuna watu wameiokota," kisha alinikabidhi niliichukua ile khanga kuna fundo lilifungwa nikalifungua nikakutana na kikaratasi chakavu kimeandikwa.

"Kwako Mwalimu Soka, ukipokea barua hii utambue kuwa rafiki yako Sitti yupo kwenye mikono salama, lakini uhai wake uko mikononi mwako, endapo tu utatuletea ile hirizi ya Simba, tuna kupa sikumbili za kusubiri, ukishindwa kufanya hivyo uhai wa huyu binti utakuwa mashakani, ni mimi Mbwana." ilimaliza sehemu ya barua hiyo.

Yule kijana alikuwa na dawa ya kupumbaza wasichana awatakao, dawa huitwa ndele. Humsogelea msichana akiwa amepaka mafuta yake ya mvuto usoni, humpiga na kifimbo chake kidogo utosini na yule msichana humfuata mwenyewe popote aendapo, nahisi alitumia mbinu hii kumuiba Sitti.

"Hirizi ya Simba?!" nilishtuka nikaingiza mkono mfukoni kujipapasa na kuitoa kile kitu nilichokitoa kwenye mwili wa marehemu wakati wa kumuosha na kisha nikakitazama kwa sekunde kadhaa, bado kilikuwa kina pumua. "Bila shaka hii ndio yenyewe na kwanini hasa wanaitaka?" Nilikuja kugundua kwamba hirizi ya Simba ni moja kati ya mazindiko makubwa sana ya wachawi pia hutumika na viongozi wakubwa wa serikalini ili kuwafanya waogopwe na kila mtu, pia ukiwa nayo hii ni kinga dhidi ya wachawi.

Kumbe ndio maana mzee Kingalu alikuwa akiogopwa na kuheshimiwa na kila mtu na ndio maana kwenye msiba wake ilipigwa ngoma, sikila mtu akifa hupigwa ngoma ni kwa watu wachache wenye hadhi fulani na heshima fulani mbele ya jamii. Kwahiyo Mzee Kingalu alikuwa na kauli ya mwisho juu ya maamuzi yoyote pale Kijijini, labda hii ilitokana na kumiliki hirizi hii ya simba. Niliondoka kuelekea nyumbani kwangu huku macho yakiwa yanatazama chini niliichukua ile khanga ya Sitti nikaizungusha shingoni, ile barua niliifunga palepale ilipokuwa.

Nilifika nyumbani saa moja kasorobo hivi usiku niliwakuta walimu wenzangu wakinisubiri kwa hofu, nilivyo waona wamekaa pale nje kibarazani nilikaza mwendo kuwawahi kwani niliona kama nachelewa kuwafikia, nilifika nikaanza kulia niliwaeleza yote yaliyotokea na jinsi Sitti alivyopotea kimiujiza tulijadiliana kila mtu alitoa wazo lake, wapo waliosema kwamba tupige simu wilayani ili watume polisi kuja kuwakamata wahusika wote lakini wazo hili lilipingwa vikali na mwalimu mkuu.

Inaonekana kama aliogopa kibarua chake kuota nyasi ama labda aliwaogopa wazee wa Kwamsisi, kufanya jambo lolote bila kuwahusisha wao ni kujihatarishia maisha yako nilimwachia mwalimu mkuu ile khanga yenye ile barua mimi nikaingia ndani ili kujipumzisha kwakuwa nilikuwa nimechoka sana sikutaka hata kula kwani hamu ya kula sikuwa nayo kwa usiku ule, pia mchana nilikula msibani. Nilisali kabla ya kulala na kumuombea Sitti awe mzima huko aliko.

Nilipitiwa na usingizi nikiwa bado nimepiga magoti pale kitandani, nilishtuliwa na sauti ya mtu aliyekuwa akigonga mlango wangu, baadaye akahamia dirishani dirisha lilikuwa na wavu na pazia tu. "Soka Soka..!" sauti ya mtetemo ilisikika nilifungua pazia kutazama nje mbalamwezi ilikuwa ikiangaza kila upande sauti ilisikika tena, "Soka Soka, kwanini mliuzika mwili wangu mapema?" Nilifikicha macho kutazama mzimu wa Mzee Kingalu ulikuwa ukinitazama kutoka dirishani sura ni yakwake lakini macho yalikuwa yaking'aa sana kama yale ya paka.

"Kwani we' walikupeleka wapi?" nilimhoji. "Walinipeleka nyumbani kwa mzee Samasimba wanataka kunifanya msukule." ulijibu ule mzimu wa Mzee Kingalu. "Umewezaje kufika hapa?" "Nimetoroka." niliogopa nikawa nikitetemeka mwili mzima jasho likiwa linanitoka nikashtuka usingizini na kutazama pazia lilikuwa limefunguliwa na wala sikuona kitu chochote pale dirishani inamaana nilikuwa naota? Niliamka pale nilipokuwa nimepiga magoti nikalala vizuri na kujinyoosha kitandani.

ITAENDELEA...
Chai
 
SEHEMU YA 7

Niliporudi kutoka kwenye kuupumzisha mwili sikumkuta Sitti pale alipokuwa amekaa. Nilijaribu kumuulizia ila kila niliyemuuliza alisema hajawahi kuona mtu kama huyo, kwani niliwalezea kwa jinsi alivyokuwa amevaa na kwa jinsi alivyokuwa akionekana, walibaki kunishangaa tu niliogopa kurudi nyumbani bila yeye nilikaa pale msibani mpaka watu wote wakamalizika kuondoka. Nami nikakata shauri la kuondoka eneo lile la tukio nilipokuwa nikiondoka nilisikia sauti ya mtu akiniita kwa jina langu ilikuwa ni sauti ya wana Kingalu. "Mwanangu Soka!" niligeuka nikamfuata.

Nilimtazama mwanamama huyu aliyekuwa amesha zeeka haswa ngozi yake iliyokunjamana na sura yake kukosa nuru. "Bila shaka unamtafuta rafiki yako Sitti?" aliniuliza. "Umejuaje mama, ni kweli namtafuta kwa maana ninajua asingeweza kuondoka bila ya kuniaga." "Unaikumbuka hii?" ananionyesha khanga aliyokuwa amejitanda. "Imeokotwa huko mtoni walipokwenda kuteka maji." (ni kawaida kwa wanawake kushiriki kazi kwenye eneo la msiba), "Kuna watu wameiokota," kisha alinikabidhi niliichukua ile khanga kuna fundo lilifungwa nikalifungua nikakutana na kikaratasi chakavu kimeandikwa.

"Kwako Mwalimu Soka, ukipokea barua hii utambue kuwa rafiki yako Sitti yupo kwenye mikono salama, lakini uhai wake uko mikononi mwako, endapo tu utatuletea ile hirizi ya Simba, tuna kupa sikumbili za kusubiri, ukishindwa kufanya hivyo uhai wa huyu binti utakuwa mashakani, ni mimi Mbwana." ilimaliza sehemu ya barua hiyo.

Yule kijana alikuwa na dawa ya kupumbaza wasichana awatakao, dawa huitwa ndele. Humsogelea msichana akiwa amepaka mafuta yake ya mvuto usoni, humpiga na kifimbo chake kidogo utosini na yule msichana humfuata mwenyewe popote aendapo, nahisi alitumia mbinu hii kumuiba Sitti.

"Hirizi ya Simba?!" nilishtuka nikaingiza mkono mfukoni kujipapasa na kuitoa kile kitu nilichokitoa kwenye mwili wa marehemu wakati wa kumuosha na kisha nikakitazama kwa sekunde kadhaa, bado kilikuwa kina pumua. "Bila shaka hii ndio yenyewe na kwanini hasa wanaitaka?" Nilikuja kugundua kwamba hirizi ya Simba ni moja kati ya mazindiko makubwa sana ya wachawi pia hutumika na viongozi wakubwa wa serikalini ili kuwafanya waogopwe na kila mtu, pia ukiwa nayo hii ni kinga dhidi ya wachawi.

Kumbe ndio maana mzee Kingalu alikuwa akiogopwa na kuheshimiwa na kila mtu na ndio maana kwenye msiba wake ilipigwa ngoma, sikila mtu akifa hupigwa ngoma ni kwa watu wachache wenye hadhi fulani na heshima fulani mbele ya jamii. Kwahiyo Mzee Kingalu alikuwa na kauli ya mwisho juu ya maamuzi yoyote pale Kijijini, labda hii ilitokana na kumiliki hirizi hii ya simba. Niliondoka kuelekea nyumbani kwangu huku macho yakiwa yanatazama chini niliichukua ile khanga ya Sitti nikaizungusha shingoni, ile barua niliifunga palepale ilipokuwa.

Nilifika nyumbani saa moja kasorobo hivi usiku niliwakuta walimu wenzangu wakinisubiri kwa hofu, nilivyo waona wamekaa pale nje kibarazani nilikaza mwendo kuwawahi kwani niliona kama nachelewa kuwafikia, nilifika nikaanza kulia niliwaeleza yote yaliyotokea na jinsi Sitti alivyopotea kimiujiza tulijadiliana kila mtu alitoa wazo lake, wapo waliosema kwamba tupige simu wilayani ili watume polisi kuja kuwakamata wahusika wote lakini wazo hili lilipingwa vikali na mwalimu mkuu.

Inaonekana kama aliogopa kibarua chake kuota nyasi ama labda aliwaogopa wazee wa Kwamsisi, kufanya jambo lolote bila kuwahusisha wao ni kujihatarishia maisha yako nilimwachia mwalimu mkuu ile khanga yenye ile barua mimi nikaingia ndani ili kujipumzisha kwakuwa nilikuwa nimechoka sana sikutaka hata kula kwani hamu ya kula sikuwa nayo kwa usiku ule, pia mchana nilikula msibani. Nilisali kabla ya kulala na kumuombea Sitti awe mzima huko aliko.

Nilipitiwa na usingizi nikiwa bado nimepiga magoti pale kitandani, nilishtuliwa na sauti ya mtu aliyekuwa akigonga mlango wangu, baadaye akahamia dirishani dirisha lilikuwa na wavu na pazia tu. "Soka Soka..!" sauti ya mtetemo ilisikika nilifungua pazia kutazama nje mbalamwezi ilikuwa ikiangaza kila upande sauti ilisikika tena, "Soka Soka, kwanini mliuzika mwili wangu mapema?" Nilifikicha macho kutazama mzimu wa Mzee Kingalu ulikuwa ukinitazama kutoka dirishani sura ni yakwake lakini macho yalikuwa yaking'aa sana kama yale ya paka.

"Kwani we' walikupeleka wapi?" nilimhoji. "Walinipeleka nyumbani kwa mzee Samasimba wanataka kunifanya msukule." ulijibu ule mzimu wa Mzee Kingalu. "Umewezaje kufika hapa?" "Nimetoroka." niliogopa nikawa nikitetemeka mwili mzima jasho likiwa linanitoka nikashtuka usingizini na kutazama pazia lilikuwa limefunguliwa na wala sikuona kitu chochote pale dirishani inamaana nilikuwa naota? Niliamka pale nilipokuwa nimepiga magoti nikalala vizuri na kujinyoosha kitandani.

ITAENDELEA...
Kuna dem nlikutana naye kwenye basi akasema kwao ni kwa msisi ..... sasa basi kwa stori hii simtaki tena
 
Ulivua ile bangili yenye nguvu ya kukusaidia kuona vitu visivyoonekana kwa macho ya kawaida…

Then akaingia Mzee kimiujiza ukafanikiwa kumuona na ukapambana nae asichukue kitu kilichokuwa kinapumua mithili ya moyo….

Make the story clear Chief[emoji3166][emoji3166]
Hapa mwandishi kateleza na mi nimeliona
 
Safi sana dogo. Lete stories watu waburudike. Kesho hakikisha unaleta episodes za kutosha. Umeshamaliza kuandaa lesson plan? Na scheme of work? Piga kazi dogo ila usisahau kutuletea visa mbalimbali vya kichawi.
Wahaya mbona mko hivi? Si utulie!!
 
Bado tunasubiri umalizie hiyo iliyobaki mkuu

Ili kuondosha maneno
Tunakuomba unganisha yoote safari hii sio roborobo tena
 
Back
Top Bottom