Siungi mkono haya mambo yanayomfanya na Manabii, Waziri wa mambo ya ndani chukua hatua.

Siungi mkono haya mambo yanayomfanya na Manabii, Waziri wa mambo ya ndani chukua hatua.

Manyanza

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
16,464
Reaction score
35,629
WAKUU
Tusifanye masikhara huu mchezo unaofanyika pale Kawe na kule Kimara Temboni, haufai na hauna ustawi kwa afya ya Taifa letu. Na huwa ni nashangaa sana @Wizara Mambo ya ndani, wanalea na kutetea huu ujuha kwenye Taifa linalohitaji jitihada za ziada kujikwamua ili Wananchi wake waweze kujimudu kimaisha. Cha kushangaza hiyo Wizara na baadhi ya Viongozi Waandamizi ndio wamekuwa ndio kama moja ya wanaobariki haya mambo.
Kinachoumiza na kukera kwenye hili Taifa.
1. Watu wanaendelea kuwa masikini
2. Upatikanaji hata wa mahitaji ya muhimu ya Kibinadamu umekuwa na changamoto.
3. Wagonjwa wako wengi tu mahospitalini
4. Wanaohitimu elimu tena kwa kugharamiwa na Serikali wapo tu mitaani na ajira yao imekuwa ni Kubeti
5. Rasilimali za nchi hazina tena manufaa kwa Wananchi.
Badala yake Serikali imeruhusu mambo yasiyokuwa na ustawi wala manufaa kwa Wananchi watu wamezidi kuwa watumwa kwa hawa Matapeli wa miujiza na ulaghai. Watu wapewe elimu ya stadi za maisha sio kuruhusu wawe Watumwa kwa Walagai na Wanaotumia dini kujineemesha.

Nawasilisha.
 
Huo ndo mtaji wa CCM. Muendelee kuweka matumaini kwa Mungu maana wai hawawajibiki. Mambo wasiyofanya wanasema ni mpango wa Mungu.
 
WAKUU
Tusifanye masikhara huu mchezo unaofanyika pale Kawe na kule Kimara Temboni, haufai na hauna ustawi kwa afya ya Taifa letu. Na huwa ni nashangaa sana @Wizara Mambo ya ndani, wanalea na kutetea huu ujuha kwenye Taifa linalohitaji jitihada za ziada kujikwamua ili Wananchi wake waweze kujimudu kimaisha. Cha kushangaza hiyo Wizara na baadhi ya Viongozi Waandamizi ndio wamekuwa ndio kama moja ya wanaobariki haya mambo.
Kinachoumiza na kukera kwenye hili Taifa.
1. Watu wanaendelea kuwa masikini
2. Upatikanaji hata wa mahitaji ya muhimu ya Kibinadamu umekuwa na changamoto.
3. Wagonjwa wako wengi tu mahospitalini
4. Wanaohitimu elimu tena kwa kugharamiwa na Serikali wapo tu mitaani na ajira yao imekuwa ni Kubeti
5. Rasilimali za nchi hazina tena manufaa kwa Wananchi.
Badala yake Serikali imeruhusu mambo yasiyokuwa na ustawi wala manufaa kwa Wananchi watu wamezidi kuwa watumwa kwa hawa Matapeli wa miujiza na ulaghai. Watu wapewe elimu ya stadi za maisha sio kuruhusu wawe Watumwa kwa Walagai na Wanaotumia dini kujineemesha.

Nawasilisha.
Ukute na yeye anaenda kuombeewa huko ndugu we fwata imani yakoo
 
Suala la imani kwa Mungu ni la mtu binafsi ..ni fumbo, maisha yana mengi sana kila mtu anatabika kivyake..imani zinaleta ahueni ya mtu kuamini atatuliwa shida zake..and it works!!
 
Back
Top Bottom