Siungi mkono Serikali kuwatafutia maeneo wamachinga. Hawa ni wahalifu walipaswa kuchukuliwa hatua

Siungi mkono Serikali kuwatafutia maeneo wamachinga. Hawa ni wahalifu walipaswa kuchukuliwa hatua

Sexless

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2017
Posts
23,683
Reaction score
55,898
Kwanni serikali imeamua kubeba mzigo wa kuwatafutia maeneo wamachinga? Hawa wanaojiita wamachinga ni wahalifu maana wamekiuka Sheria na taratibu mbalimbali za nchi kwa kuamua kujenga mabanda barabarani ama kupanga bidhaa mbele ya maduka ya wafanyabiashara.


Nilitegemea watu hawa, mmoja mmoja ama kwa umoja wao wachukuliwe hatua kali za kisheria.

Ama kwa kuhurumiwa wafurushwe bila huruma kutoka ktk maeneo hayo haramu halafu wao wenyewe watafute mahala sahihi pa kwenda.

Kama serikali inaona ni sahihi kuwatafutia wahalifu (wamachinga) maeneo mbadala, basi ifanye hivyo pia ktk makundi mengine ya wahalifu kama ifuatavyo:-

1. Waliovamia na kujenga kwenye hifadhi ya barabara, open spaces na taasisi za serikali wapewe viwanja.
2. Wafugaji wanaochungia maeneo ya hifadhi wahamishiwe maeneo yenye malisho.
3. Iwajengee nyumba ombaomba wote nchi nzima.
4. Wapiga debe wote wanunuliwe mabasi na serikali.
5. Wavuvi wanaotumia nyavu haramu (makokoro) serikali iwapatie nyavu halali. Siyo kama ilivyo sasa amabapo wavuvi huchomewa nyavu zao na kuachwa masikini kabisa

Watu wote ktk makundi yote haya wamekiuka Sheria na taratibu ndiyo maana huwa wanatiwa nguvuni wakikamatwa. Iweje hawa wahalifu (wamachinga) ambao wamevunja Sheria za nchi machana kweupe wananyenyekewa??

N.B. Wamachinga waondolewe kwa nguvu maeneo yasiyoruhusiwa. Wasibembelezwe.

NIMEJENGA HOJA, NAOMBA NIJIBIWE KWA HOJA. NISIBEZWE.
 
Acha roho mbaya.. Sasa unataka wakale wapi?

Binadamu kusaidiana.. usifurahie anguko la mwenzako. We unadhani hao machinga wasipo settle, utaishi kwa raha?
 
Mbona hayo makundi mengine hayasaidiwi ili ya-settle?
We umesema wafurushwe bila huruma.. sio jambo zuri.. nao wana haki kwenye hii nchi.

Ni kweli hawakufanya shughuli zao kwa utaratibu ila sababu haswa ni hao hao serikali kukosa mipango ya mapema.

Kwahiyo sioni haja ya kuanza kuwaumiza hawa machinga
 
Ukiwasikiliza wanaojiuza, wapiga debe na wezi nao pia wailaumu serikali.
Wewe huoni kwamba kuna mstari mwembamba sana unaotenganisha machinga na hayo makundi mengine ya wanaojiuza, wapiga debe na wezi.

Jaribu kufikiri mkuu... Ndo mana kwenye social welfare ya jamanii.. mistreatment ya wamachinga itakuwa na impact ambayo mpaka sasa kuna indicators zinaanza kuwa dhahiri..

Think
 
Wachukulie hatua halafu uone jinsi watakavyoanza kuchoma moto maduka ya watu Kariakoo na kuwatia watu hasara.
 
Duhh...kweli wew ni bwanyenye.
Yupo sahihi machinga walitakiwa kabla ya kuamishwa wapitiwe mmojammoja biashara mitaji yao isngaliwe. Wameikosesha serikali mapato kwa mda mrefu.

Wengi walishakuwa na mitaji mikubwa. Mtu anauza soda,juisi na maji ya jumla banda lipo juu ya mitaro. Vipodozi,mitungi ya gesi,wengine walikuwa wanauza mpaka simu je ni kweli walikuwa machinga hawa?

Kuhusu ishu ya kutafutiwa maeneo vipi sisi wakulima na wavuvi ns makundi mengine nani alitutafutia? Haya ndo matokeo ya siasa za kupenda sifa za mwendazake.
 
Usijali serikali itafanya hivyo,subiri kwanza tu sort wamachinga first and then tutafuata hayo makundi mengine 😊😊😊😊
 
Serikali itumie mabavu kuwatimua afu baadae wamachinga hawa hawa waje watumiwe na wapinzani uchwara kama daraja la kutafutia kura, kwa kujifanya wanawatetea na kutengeneza sera za uongo za kujifanya wana njia mbadala ya kuwasaidia wamachinga wote walionyanyaswa na kukandamizwa na serikali iliyopo sasa. Lengo na dhumuni la kuandika uzi huu lishajulikana tayari, na kamwe haliwezi kufanikiwa kwa namna yoyote ile.
 
Kuhusu ishu ya kutafutiwa maeneo vipi sisi wakulima na wavuvi ns makundi mengine nani alitutafutia? Haya ndo matokeo ya siasa za kupenda sifa za mwendazake.
Tena umenikumbusha mkuu. Walionunua nyavu zisizoruhusiwa walichomewa nyavu zao na hawakugawiwa nyavu sahihi
 
Back
Top Bottom