SKONGA: Kipindi 'kinachovua nguo' wanafunzi


Na hili mbona limekwenda mbali mpaka kwa kaka zao vyuo vikuu?Kuna kile kipindi kilichokuwa kinaitwa Zain Africa Challenge...wanafunzi wa vyuo vikuu vyetu walikuwa hawafiki kokote wakikutana na Waganda.Wakenya na Wanaigeria.Tatizo letu kubwa ni kwamba HATUSOMI.
 
Huyo ndiye usiseme kabisa, badala ya watoto kulala na kutuliza bongo zao, saa 9 za usiku tukiamshwa kuwahi foleni ya unga. Usinikumbushe mateso aliyotupa nchi nzima.

Mzee yule, Mungu amlaze anapostahiki.

sasa wewe ulizaliwa enzi zipi? Majanga haya
 
vyakula vinachangia tutoto kukua haraka na kujiglobolaizi kwenye sosho faktazi nyingi,
hensi;
kukua mwili ....kulemaa akili

mkuu hii pepa yako ni ya kuchukulia phd kabisa. Naomba nakala yake niweke kwenye library yangu
 
Dah, naona sasa unauhamishia mjadala kwenye dini! samahani sana sina mood ya kwenda huko kwa sasa na nnakuomba, koma.
Iwapo utamkoma Nyerere usidhani dini yako ni bora kuliko wengine hata wapagani imani yao ni bora zaidi pia. Koma kabisa.
 
Iwapo utamkoma Nyerere usidhani dini yako ni bora kuliko wengine hata wapagani imani yao ni bora zaidi pia. Koma kabisa.

Kinachokukasirisha nini? na mambo niliyoyaandika ndivyo yalivyokuwa wakati wa Nyerere? ni nani asiyejuwa kuwa tulikuwa tukiamshwa saa 9 za usiku kwenda kuwahi foleni ya unga?

Naona hilo limekuuma sana, labda ungewauliza wazee wako kama walikuwapo wakati huo watakueleza. Naona wewe ni mtoto mdogo sana na umejazwa ujinga kiasi hata ya ukweli yaliyokuwapo wakati wa Nyerere wewe unaona anaonewa tu.

Unaendelea kulazimisha kuufanya huu mjadala uwe wa kidini. Nakwambia tena, sipo kwenye mood ya kuingiza dini kwa sasa, kama unahamu sana ya kuongelea dini, usiharibu hii nyuzi ya watu, funguwa yako niite ntakuja. Narudia, koma.

Nyerere Mungu amlaze anapostahili.
 
Here we go, kwamba unakanusha Mwamed siyo Marehemu na anasubiri hukumu siku ya hukumu? koma kabisa ujinga wako huu peleka huko huko kwa kina Mohamed Said. Fuseki.
 

hahaha! Haya ni majanga kwa kweli. Umenikumbusha siku moja lecturer wa udom alisikika akilalamika kwamba wanafunzi wake wa sheria wanaandika paragraph nzima bila kuweka panctuation mark hata moja. Elimu ye2 imekuwa majanga tangu kindergarten mpaka chuo kikuu. Yanahitajika mapinduzi ya kufa m2 ili kuirejesha elimu yetu kwenye mstari. Na ilianza kuharibika tangu zamani, sio leo. Wanafunz wanamaliza chuo kikuu hawawez kuongea wala kuandika kiingereza kwa ufasaha!!! MAJANGA!¿?!
 
Here we go, kwamba unakanusha Mwamed siyo Marehemu na anasubiri hukumu siku ya hukumu? koma kabisa ujinga wako huu peleka huko huko kwa kina Mohamed Said. Fuseki.

Nimekwambia, hata ukikasirika huo ndio ukweli na kuna watu wazima kuliko wewe waliokuwepo wakati wa Nyerere, wanaomtetea na wasio mtetea, wanajuwa huo ndio ukweli. Na si huo tu kijana, kuna mengi sana tuliyapitia wakati wa Nyerere ambayo leo hii neema tuliyonayo tukiyawaza roho zinatuuma.

Tulikuwa wafungwa ndani ya nchi yetu. Tukipimiwa reshen ya kula kwa wiki ambayo hata wafungwa wa leo hawapimiwi hivyo. Jee, unafahamu kwamba ilifikia wakati tukipiwa sukari kilo moja kwa wiki nzima kwa kaya moja? na ilhali Nyerere huyo huyo alipokabidhiwa hii nchi Tanzania ilikuwa nchi ya kwanza katika Afrika kusafirisha mazao ya chakula?

Sasa kaa ufikiri, mtoto ambae hana lishe bora hiyo elimu itamuingia kweli?

Fikiri tena, usiingize dini katika hii mada ya watu, watakuona ni mjinga. Koma.

Nyerere Mungu amlaze anapostahiki.
 
Mada za kijinga kama hizi tafuta mapunguwani wenzako wa Kariakoo mkae barazani ndio mjazane ujinga huu huku mkila tende na kusikiliza ngano za Mohamed Said. Jingas kabisa.
 
Mimi nilizaliwa wakati hii nchi iko chini ya Umoja wa Mataifa na ulinzi wa Waingereza.

Matokeo ya vyuo vya ualimu yatoka, watahiniwa washindwa vibaya mitihani yao nchini ilioandaliwa na serikali yenye mafanikio ya rais Jakaya Kikwete!!
 
Mada za kijinga kama hizi tafuta mapunguwani wenzako wa Kariakoo mkae barazani ndio mjazane ujinga huu huku mkila tende na kusikiliza ngano za Mohamed Said. Jingas kabisa.

Hapa ni mada ya elimu, na sisi tuliokuwepo siku hizo tunajuwa chanzo cha kushuka elimu ya Tanzania. Sababu kubwa ya kushuka elimu Tanzania ni Nyerere na siasa zake zilizokuwa hazina muono.

Nakumbuka shule niliyokuwa nikisomaa mimi wakati naanza shule kulikuwa kuna "Janitor" wa shule. Huyu kazi yake ilikuwa kuhakikisha shule iko safi wakati wote, vyoo visafi, madarasa masafi, uwanja msafi na kweli shule ilikuwa inang'aa.

Naam, baada ya Mwaka 1967 wakati huo nipo darsa la nne, tukawa tunaanz akufagilishwa sisi shule na yule "Janitor" tukaambiwa tusimwite tena "Janitor" na tumuite "Mwalim wa usafi". Tulikuwa wadogo na hatukuwa na hili wala lile, lakini leo hii nikikumbuka nasema ule ndio ulikuwa mwanzo wa kuporomoka kwa elimu.

Yule Mzee alikuwa hana alijuwalo zaidi ya kujuwa kuongea. Utendaji na Falsafa zake zote ziliharibu kila kitu mpaka kuwa ZERO. yes Sifuri.

Mwenyeezi Mungu amlaze Nyerere anapostahiki.
 

Baba yangu mzazi, Mzee Mikidadi, aliharibikiwa baada tu ya KUSILIMU akiwa mtu mzima (mwaka 1970)!! Kitu cha kwanza alichofanya ni kuanza kuoa/kuongeza wanawake wengine kwa kasi ya ajabu! Kufumba na kufumbua ana wake watatu! Kitu cha pili na cha ajabu alichofanya ni kutaka kutuzuia kusoma elimu dunia bali tujikite kusoma MADRASA!! Hapo ndiyo MTAFARUKU ulipoanzia katika familia yetu na hatimaye mama yangu akafukuzwa kwa TALAKA TATU,na watoto wote, tulikuwa 10 tukafukuzwa na mama!! Baba yangu akaoa mke mwingine ku-cover nafasi iliyoachwa na mama!! Sasa basi kilichomtokea baba na watoto wake wengine aliowazaa kwa wake zake wengine hakuna aliyevuka darasa la saba!! Lakini wakiwa wamejaza JUZUU kibao vichwani mwao na ROHO MBAYA kama ya kwako!!

Thanks to GOD and Mwl JK Nyerere, mama yetu, akiwa mwanakijiji tu asiye na chochote alifanikiwa kutusomesha watoto wote and now I AM PROUD as both a CIVIL ENGINEER and an ACCOUTANT! MY STEP SISTERS wana roho mbaya kama wewe! Walichezea nafasi za bure za kusoma enzi za Mwalimu kwa kudanganyana kama mnavyofanya hadi leo!! Kipindi cha utawala wa JK elimu imeshuka sana lakini bado mnalia na Nyerere! Shame on You!!!
 
Matokeo ya vyuo vya ualimu yatoka, watahiniwa washindwa vibaya mitihani yao chini ilioandaliwa na serikali yenye mafanikio ya rais Jakaya Kikwete!!

Safi sana, hapo ndio ujuwe wakati huu wa Kikwete habebwi mtu, aidha wafanye vizuri au kufeli tu. Hakuna kuchekeana, viwango lazima vipande.

Hapo inafaa pasifiwe sana inaonesha kuwa zile rushwa za kupeana vyeti huko na kupasishana hata waliofeli sasa inadhibitiwa.
 

Umeangalia jambo hili kwa jicho lisilo la kawaida, vyombo vyetu vya habari kiukweli vina mchango mkubwa wa kuharibu au kutokuharibu jamii, mbaya zaidi vipindi vinaendeshwa kwa matakwa ya watangazaji na kuna kipindi watangazaji wanaonyesha mitazamo binafsi wakati anatakiwa awe neutral aache wasikilizaji wamalize.

Back to the point, kuna haja ya mamlaka zinazohusika kusimamia hili suala hasa ukizingatia ni ngumu kwa mzazi kumsimamia kila kitu mtoto wakati 24 hrs vipindi vinavyorushwa ni vya aina hiyo hiyo ya kujirusha. Nilichojifunza hawa jamaa wanatumia ule msemo wa kufa kufaana maana ukiangalia kwa jicho la kawaida utaona kwamba vifo vya Ngwea na Kanumba walivyokuwa wamejitolea kutangaza live ni kwa sababu walijua wengi wataangalia na matangazio yao ya biashara watauza kwa style nyingine (si ya udhamini wa vipindi kama ilivyozoeleka) ila kwa walio wengi wataona hawa jamaa ni waungwana kweli lakini ajabu kuna wengine yakitokea ya kutokea mbona hakuna kuweka live.

Miaka ya nyuma nilikuwa naona serikali wanoko walivyokuwa wanatoa leseni kwa mikoa michache kwanza alafu baadae ndio wanaruhusu mikoa mingine (nimegundua ilikuwa inasaidia sana)
 

Samahani lakini inaonesha baba'ko alikuwa ana matatizo ya akili, anaoa mpaka Mkwe? poleni sana. Na inaonesha matatizo yake umeyarithi wewe.
 

Inawezekana kwa kipengele hiki ilikuwa mnapata practical orientation ya namna ya kufanya usafi ili mkirudi nyumbani muwe mna-support kazi ndogo ndogo za nyumbani
 
Nadhani kuanza maswali unayoyaweza(mepesi)ni starategy ya kuscore marks uweze kutoka,cuz kuna swala la muda pia kwenye mtihani,sasa haiyumkiniki ukang'ang'ania swali ambalo linahitaji muda wa kufikiri zaidi wakati yako maswali ambayo kwako ni kutiririka tu mwanzo mwisho na sometimes yana marks sawa na maswali yanayohitaji muda wa kufikiri,unatakiwa kuwa mjanja wa mtihani kwa kuwa elimu yetu ndio iko hivyo,tunasoma ili tufaulu mitihani!
 
Ni kweli FaizaFoxy kuwa vipindi vya burudani vimezidi. Hakuna ubunifu kwenye vipindi vya kuelimisha kwenye tv na redio zetu.

Tangopori huyo alikuwa kidato gani?

ni kweli vipindi vya miziki ya mapenzi inayochezwa na watu walio nusu uchi vimezidi. Kuna siku huwa nafungua tv, hasa nyakati za mchana, nakuta stations zote, kuanzia tbccm mpaka c2c wanapiga miziki ya nusu uchi na isiyokuwa na mafundisho yoyote (ukipenda iite bongofleva). Ni bora hata stations za tv zingekuwa chache kuliko zilivyo utitiri sasa hv lakini hazina tija. Kuna haja ya kufanya mageuzi ya utangazaji na kuweka sheria zinazosimia vipindi vya tv na hata redio.
 
Last edited by a moderator:
Inawezekana kwa kipengele hiki ilikuwa mnapata practical orientation ya namna ya kufanya usafi ili mkirudi nyumbani muwe mna-support kazi ndogo ndogo za nyumbani

Hapana. Kumbuka enzi hizo tulikuwa na kipindi cha "domestic science" ambacho kilikuwa ni kipindi maalumu cha kutufundisha kazi zote za nyumbani.

Hapo juu nilikuwa naonesha kuwa badala ya kusoma sasa tukaanza kufagilishwa viwanja, madarasa, vyoo na "Janitor" kawa Mwalim!

Usishangae hili la "Mr. Janitor" kuwa Mwalimu "overnight" huko juu nimeonesha mfano wa kuli wa bandarini alipofanywa kuwa mshauri wa Nyerere Ikulu (tena huyo ndie baba'ke huyu Nape Nnauye), mwambie aje anipinge kwa hili.

Sasa wewe fikiri, hapo kuna kusoma tena?

Leo kama hatujarekebisha makosa yaliyofanywa wakati ule, basi hata tufanye nini tutaonana watoto wenye shule zenye ma "Janitor" siku zote watafanya vizuri zaidi ya zile shule ambazo ma "Janitor" ni wanafunzi wenyewe. Nafurahi kuwa hilo serikali ya kikwete imeliona na linapunguwa kwa kasi kubwa sana, siku hizi si mara nyingi kuona mtoto kabeba fagio na jembe anakwenda shule. Bado kuna kazi kubwa inabidi ifanyike lakini tunapata faraja kuona imeanza kufanyika.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…