Elections 2010 SMS kutoka CCM

kama kuna mtu ambaye anaona ameingiliwa faragha yake nendeni mahakamani.. angalau muoneshe ujasiri kuwa hamjaridhishwa.. haitoshi kulalamika humu.
Ngoja wanitumie waone.
Network provider wangu watanitambua kama mimi nina elements za Mtikila.
Nawaburuza mahakamani.
 
Kampuni za simu hazitakiwi kutuletea mameseji ya namna hii bila idhini yetu - tena bila kuzingatia muda decent.

Mimi sijawahi kujiunga na hiyo promosheni/utafutaji pesa wa CCM, lakini bado nilipata meseji hiyo usiku wa manane. Mtu unaamshwa ukifikiri kuna dharura - kumbe meseji ya CCM!
 
Mie huko voda nilishaondoka siku nyingi baada ya kugundua kumbe ni mtandao wa fisadi papa Rostam. Damn him and damn him again.
 
Mtandao gan wamewaluhusu ccm hiv jamaa hawa hawana din au marafiki wa karibu wa kuwaambia ukweli.Tumshilikishe mungu jaman atusaidie

Mtandao gani huo kama vipi tupige chini line zake faster kabla hatujaichangia sisiemi kinguvu kaka. Napata hasira sana na hiki chama shule, hospitali, mvua ikinyesha Dar?, foleni, mikataba mibovu, maji, umeme(wanataka kupatisha kwa asilimia 39 mjiandae) bado ni tatizo kwa jamii Tuwaondoe kwa votes guys wake up
 
tuchangie ccm kwa faida gani??? hii inadhihirisha chama hakiko makini, mbona hawatupatii financial statement zao
ili tuone umuhimu huo, yaani wanataka hata kidogo tulicho nacho wachukue??? chama kinajulikana lakini wanatumia
nguvu nyingi, mabango kila mahari, kwa miaka 50 ya kutawala ilitosha kupita kusalimia wananchi maana wangekuwa
washaona hayo maendeleo, kweli kibaya chajitembeza.......
 
bishanga what your saying is rubbish kwa ufahamu wa watu wengi hizi sms hao wanachama wa ccm huwa wanapata toka kipindi cha nyuma kabla ya kampeni.sasa tunapotaka siasa ya nchi yetu ikue tuvunje makundi na tuwe wawazi kama watanzania na wazalendo kwa ujumla wala rushwa ndio adui zetu sms ?kwani cuf au tlp mfano wanashindwa kuanzisha mfumo kama huo wa kuwapatia habari mbalimbali za matukio au vinavyo endelea ndani ya vyama vyao tuache unafiki usio na ujenzi kwa taifa letu MPASUAJI
 
Ccm wana laana ya nini lkn?.....wanachezea watu wakati wa malavidavi?.........au kwa kuwa walisema wanaume wanyimwe unyumba na wake zao kwa kutoishabikia ccm?
mbaya zaidi wengine tumepata saa nane za usiku:mad2:
 
Mimi iliingia saa sita kamili usiku wanakati na do ze nidiful, u can imagine kilichotokea, manake nikadhani ni taarifa ya msiba/mgonjwa. kumbe ni msg za CCM za promosheni ambayo sijawahi kujiunga....


natafuta msaada wa kisheria jamani...
 

Huwezi kuamini, mimi ninatumia mtandao wa TIGO na ZAIN, kote wamenitumia huo upuuzi wao! Kwenye TIGO saa 6 usiku, ZAIN zimeingia sms 2: moja saa 7:33 usiku na ya pili saa 8.59 usiku! Sijawahi wala sitakuwa mwanachama wa CCM, natafuta wanasheria wanisimamie kesi yangu! Nataka kudai bilioni 1.5 TSHS.
 

Sijawahi kujiunga na lotto yoyote, sembuse hiyo ya CCM! Lakini wamenitumia kwenye TIGO na ZAIN!!!
 
...,.Yaaani we acha tu NIMEKEREKA SANAA Imagine mimi si shabiki wala mfuasi wa chama cha siasa nashangaa napata message kutoka Chomoa Chako Mapema nimekasirika sana kidogo hata nihamie mtandao.. Inakera unamtumiaje mtu ujumbe aambaye hana jhaja nao kwa kweli wamechemsha vibaya sanaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa....................ama kweli CHOMOA CHAKO MAPEMA.
 
Changia chadema
account no 2266600140, jana la account ni chadema, bank ni nmb, tumia tawi lolote, hata kama uko nje ya nchi, nenda kwenye tawi lolote la rabobank ,

au tumia namba ya simu 15710, tuma neno chadema,

asante, mchango wako ni muhimu sana.

People power
 
Hiyo ndo CCM!!!
Udanganyifu kwenda mbele!!
 
HAPO HAKUNA CHA NINI WALA NINI, KUNA WAJANJA WANACHUKUAPESA KIULAINIIIIIIII, WE CHANGIA NA WALA PESA HAIENDI CCM WALA NINI.

MIFUKONI AKILI MU KICHWA :confused2::confused2:
 
Bora mimi sijapata,maana ningetapika
 

Asante mkuu, nimetuma imekubali.
 
Mashaka matupu bora ujumbe huu angeutoa DR SLAA humu angeweza kueleweka sasa LipaMungu unataka kujitajirisha!?
 
Asante sana mkuu, inafanyakazi, ni muhimu sana ndugu tuunganishe nguvu kuyashinda mafisadi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…