SMZ na uchukuaji wa maeneo ya wazi (Open Space)

SMZ na uchukuaji wa maeneo ya wazi (Open Space)

silent lion

JF-Expert Member
Joined
Feb 28, 2012
Posts
1,278
Reaction score
1,794
Kwa heshima kabisa naomba kuleta malalamiko yetu katika jukwaa hili kubwa la Jf.

Hivi sasa kisiwani Unguja kumekua na kasi kubwa ya ujenzi wa Majengo mbali mbali. Ni jambo la heri na jambo la kupongezwa na kwa hakika tunamuunga mkono Mheshimiwa Rais wetu .

Jambo lilonifanya kuleta bandiko hili ni kua ujenzi huu unafanyika katika maeneo ya wazi ambayo tangia ukoloni maeneno haya yamewekwa kwa ajili ya michezo na watoto.

Viwanja maarufu vya Malindi ambavyo vipo karibu na bandari navyo vipo hatarini na serikali imeshatangaza rasmi kuvitwaaa kwa ajili ya ujenzi wa maegesho ya magari.

Ikumbukwe sehemu kubwa ya viwanja hivi imeshanyakuliwa na vigogo na hivo vilivyobaki navyo serikali inavitolea macho licha ya pingamizi kubwa kutoka kwa wakaazi wa maeneo hayo.

Hivyo kwa heshima na taadhima tunaiomba Serikali yetu tukufu ya SMZ na mpendwa Rais wetu , isitishe ujenzi huu kwa maslahi mapana ya vizazi vya sasa na baadae.

Na kwa wanachama wote wa JF mtusaidie kupaza sauti juu ya jambo hili.

Mungu awabariki nyote.

Tuipende nchi yetu.
 
Kwa heshima kabisa naomba kuleta malalamiko yetu katika jukwaa hili kubwa la Jf.

Hivi sasa kisiwani Unguja kumekua na kasi kubwa ya ujenzi wa Majengo mbali mbali. Ni jambo la heri na jambo la kupongezwa na kwa hakika tunamuunga mkono Mheshimiwa Rais wetu .

Jambo lilonifanya kuleta bandiko hili ni kua ujenzi huu unafanyika katika maeneo ya wazi ambayo tangia ukoloni maeneno haya yamewekwa kwa ajili ya michezo na watoto.

Viwanja maarufu vya Malindi ambavyo vipo karibu na bandari navyo vipo hatarini na serikali imeshatangaza rasmi kuvitwaaa kwa ajili ya ujenzi wa maegesho ya magari.

Ikumbukwe sehemu kubwa ya viwanja hivi imeshanyakuliwa na vigogo na hivo vilivyobaki navyo serikali inavitolea macho licha ya pingamizi kubwa kutoka kwa wakaazi wa maeneo hayo.

Hivyo kwa heshima na taadhima tunaiomba Serikali yetu tukufu ya SMZ na mpendwa Rais wetu , isitishe ujenzi huu kwa maslahi mapana ya vizazi vya sasa na baadae.

Na kwa wanachama wote wa JF mtusaidie kupaza sauti juu ya jambo hili.

Mungu awabariki nyote.

Tuipende nchi yetu.
Kwahiyo nisipoependa nchi yangu ni dhambi?
 
Uchumi wa buluu 😁.

Mkuu hatuwezi kupiga kelele, mzee baba late John Pombe alisema mkimchagua Dr. Mwinyi uchumi utapaa na zanzibar itabadirika fasta so mpeni muda na ngojeni kidogo afanye yake.

Yaani maeneo yote wazi ni full ma_skyscrapers mpaka pale maisara kuja jirani na hospitali ya mnazi utajengwa mnara mwingine, wacheza mpira watajengewa kiwanja cha kisasa kwingine au pale kwa pembeni.

ahahahaa... sheikh unaanza kulia hata robo bado.
 
Uchumi wa buluu 😁.

Mkuu hatuwezi kupiga kelele, mzee baba late John Pombe alisema mkimchagua Dr. Mwinyi uchumi utapaa na zanzibar itabadirika fasta so mpeni muda na ngojeni kidogo afanye yake.

Yaani maeneo yote wazi ni full ma_skyscrapers mpaka pale maisara kuja jirani na hospitali ya mnazi utajengwa mnara mwingine, wacheza mpira watajengewa kiwanja cha kisasa kwingine au pale kwa pembeni.

ahahahaa... sheikh unaanza kulia hata robo bado.
Lazima tupaze sauti, viwanja vya malindi vina historia kubwa na ni pahala watoto wetu wanapocheza pamoja na sisi tunapofanya mazoezi
 
Tatizo ndani ya huo ujenzi..wanamega na kujenga majumba yao binafsi...

Hapo kikwajuni Kuna eneo zuri la kihistoria sasa hivi taratibu wanalisogelea..

Tunarudi kuleeeeh.. ..halafu baadae tuanze kulalamika.. ...
 
Lazima tupaze sauti, viwanja vya malindi vina historia kubwa na ni pahala watoto wetu wanapocheza pamoja na sisi tunapofanya mazoezi
Sheikh bila kuvunja mazoea hutapata maendeleo, hizo historia watasoma kwenye vitabu.

Mfano; stone town humo mnaishi kwa garama ndogo sana ya kodi ila jumba likipata mushkeli hata mlango kutoka bawaba hutaki kurekebisha unadai shea au mkurugenzi aje kurekebisha.

Mzee baba Dr. Mwinyi kaamua sasa, ukiweza rekebisha, huwezi ondoka pisha mwenye uwezo wa kurebisha aje.

Nchi inataka watu wenye kuweza kusaidia pale inapowezekana, siyo kila kitu serikali, 😄!.
 
Sheikh bila kuvunja mazoea hutapata maendeleo, hizo historia watasoma kwenye vitabu.

Mfano; stone town humo mnaishi kwa garama ndogo sana ya kodi ila jumba likipata mushkeli hata mlango kutoka bawaba hutaki kurekebisha unadai shea au mkurugenzi aje kurekebisha.

Mzee baba Dr. Mwinyi kaamua sasa, ukiweza rekebisha, huwezi ondoka pisha mwenye uwezo wa kurebisha aje.

Nchi inataka watu wenye kuweza kusaidia pale inapowezekana, siyo kila kitu serikali, 😄!.
Mambo ya Mji Mkongwe hayahusiani hapa sisi tunazungumzia open space. Huko New York kuna maendeleo makubwa na open space zipo. Kama hujafika Kuna central park, tembea uone sio unaishia buza na gongo la mboto tu
 
Mambo ya Mji Mkongwe hayahusiani hapa sisi tunazungumzia open space. Huko New York kuna maendeleo makubwa na open space zipo. Kama hujafika Kuna central park, tembea uone sio unaishia buza na gongo la mboto tu
Unategemea open space iliyopo amerika ndiyo uilinganishe na open space ya maisala?, kweli we kinyonga 😧!.

Kwanza, unaweza kuwa umefika ughaibuni na bado huelewi au hata kama unaelewa bado akili imekaa kiafrika afrika, una zile Chembechembe za roho mbaya nk.

Pili, Ulaya hawana aridhi, afrika tuna aridhi, maeneo ya mapoli mengi kila baada ya 20 kilometres tofauti na huko unapoona ndiyo mbinguni, pole.

So unaposema central park ni hujui historia yake ila kufika kwako pale unataka kutambia vijana wenzako, issue ya CP 1957 ulipaswa uoanishe na Darajani au Forodhani, full stop.

👉🏾 If you're empty find to fulfil your empty.
 
Unategemea open space iliyopo amerika ndiyo uilinganishe na open space ya maisala?, kweli we kinyonga 😧!.

Kwanza, unaweza kuwa umefika ughaibuni na bado huelewi au hata kama unaelewa bado akili imekaa kiafrika afrika, una zile Chembechembe za roho mbaya nk.

Pili, Ulaya hawana aridhi, afrika tuna aridhi, maeneo ya mapoli mengi kila baada ya 20 kilometres tofauti na huko unapoona ndiyo mbinguni, pole.

So unaposema central park ni hujui historia yake ila kufika kwako pale unataka kutambia vijana wenzako, issue ya CP 1957 ulipaswa uoanishe na Darajani au Forodhani, full stop.

👉🏾 If you're empty find to fulfil your empty.
Shida ndo hii , mtu anapinga jambo wala hajui umuhimu wake, unaandika wala hujui unaandika nini. Sasa unataka watoto wetu ndo wakacheze maporini?
 
Shida ndo hii , mtu anapinga jambo wala hajui umuhimu wake, unaandika wala hujui unaandika nini. Sasa unataka watoto wetu ndo wakacheze maporini?
Ndiyo mana unakosa, kwa sababu unajifanya mjuaji sana endelea, ila sisi tunaijenga zanzibar ili vizazi vijavyo vije vifurahie tuliotangulia.

Kichwa km chako kingekuwepo wkt wakoloni wanajenga hii stone town unayoiona leo nadhani ungepinga.

Na hapo maisala tutakujengeeni kiwanja cha michezo mpaka taa tutakuwekea, ili ucheze na wanao mpaka machweo.

shwain 😄!
 
Ndiyo mana unakosa, kwa sababu unajifanya mjuaji sana endelea, ila sisi tunaijenga zanzibar ili vizazi vijavyo vije vifurahie tuliotangulia.

Kichwa km chako kingekuwepo wkt wakoloni wanajenga hii stone town unayoiona leo nadhani ungepinga.

Na hapo maisala tutakujengeeni kiwanja cha michezo mpaka taa tutakuwekea, ili ucheze na wanao mpaka machweo.

shwain 😄!
Hivo viwanja vya taa nyie sio wa mwanzo kujenga vipo vingi Zanzibar, ila si kila mtu anamudu kuvichezea , wananchi wengi wanyonge hawawezi kutoa laki na nusu ili kupata fursa ya kucheza.

Viwanja vya Malindi ndo kimbilio la wanyonge na bado mnavitolea macho nchi gani hii itakayokua haina open space or public park ? Maisara mshachukua, Kwa mchina mmechukua, Mpendae mshazungusha mabati hivi kweli ndo mnakosa maeneo mpaka mvamie open space?

Witless worm!!!
 
Tatizo ndani ya huo ujenzi..wanamega na kujenga majumba yao binafsi...

Hapo kikwajuni Kuna eneo zuri la kihistoria sasa hivi taratibu wanalisogelea..

Tunarudi kuleeeeh.. ..halafu baadae tuanze kulalamika.. ...
Hapo MALINDI pia vigogo wamejenga Kuna Amana bank iko kwenye open space. Kuna jamaa mmoja Anaitwa Jussa na yeye kajenga kwenye open space darajani na mbuyuni. Na hicho kilichobaki pia wanakitaka
 
hawa jamaa ni watu wa ovyo kabisa, hivi wanashindwaje kuvunja vijumba vibovu visivo na plan kwa ajili ya hayo majenzi? CCM ni watu wa ovyo sana
 
Watoto zaidi ya mia moja sijui wataenda wapi
 
Back
Top Bottom