SMZ yazidi kuubomoa Muungano yataka bara walipe kodi ya ardhi


...te-he!

ndipo mtapotambua Zanzibar ni Nchi au Mkoa! ...tena hapo kwenye 'mwenye asili ya Zanzibar kulipa dola 500 (sh650,000)' ...mwandishi angeongeza Tu!

Zanzibar ni njema, atakaye na aje!
 
i say hiyo achana nayo wao wakitaka kura watatupa kadi ya raia hapo kwa wapemba kula jiwe tu subiri uchaguzi unakuja hakuna kula chi chi mm tuone jeuri
 
kulipa kodi its okay......najaribu kuangalia/ kufikiria US$ 5000 kwa mwaka!!....virtually only Chenge et al will own/lease/rent land in visiwani
 

Tatizo si kodi bali ni hizo tofauti ya viwango. Zanzibar wametumia haki yao kueleza wazi kuwa mtanzania bara akiwa kwao ni sawa na mfilipino. Hii ni haki yao lakini wahenga walisema kuwa ukila na kipofu.......!
 
Tukimaliza Wahindi na Muiran, Zanzibar you are NEXT.
Niite Mbaguzi, poa tu. Ila watu kama mimi ni muhimu kwa kila nchi.
Sisi ndiyo tunaitwa WAFANYA KAZI CHAFU.
 
Hebu tulia kwanza. Haya maneno ya Nyerere hapa hayafanyi kazi maana siyo sisi tueanza kuuvunja Muungano na kutenga watu. Tumelilia sana turekebishe mambo na tubaki pamoja. Tumeitwa majina ya ajabu sana, tumenyanyaswa na sasa tunaanza kutengwa waziwazi.

Nyerere huko juu, nafikiri utakuwa na sisi wakati tukiruhusu Wazenji KULA NYAMA YA MTU. Wao ndiyo wataendelea kulana. Kwani sisi kuna kabila linataka kujitenga Tanganyika? Au kuna mtu kasema kabila fulani inabidi litengwe? So longer Wanyamwezi/Wasukuma bado hawana noma, Tanganyika itasimama pamoja.
 
Urgently Inabidi ku-revisit mambo muhimu ya Muungano.......ili uendelee......ama sivyo.....what a time BOMB............tik tak tik tak!!!!
 
Hivi uliposema Muirani, umekusudia WASHIRAZI! Ahsante msee!
 
Muungano unatia kichefuchefu.....kwa nini Kila nchi isende kivyake??? Wananchi wengi wameishaonyesha wazi kukinaishwa na Muungano......ni wakati sasa kila m2 afe kivyake....kila m2 achukue kilicho chake....
 
Huo ndio utakua mwisho wa Muungano. Sijui kati ya Bara na Visiwani ni wepi watakaoumia.
Hautakuwa mwisho wa muungano kama walipitisha wimbo wao wa taifa na bendera yao unafikiri hili litawasitua wabara.Unaelewa wabara tunapenda sana sifa.na wengi wao hawana uzalendo na nchi hii.Hebu fikiria baada ya kuruhusu wawekezaji kwenye kilimo kutoka nje sheria ya ardhi ilipitishwa na kuongeza umiliki wa ardhi toka miaka 33 hadi 99.
 
Ni nani Mwekezaji ? Naomba ufafanuzi kupitia hapa JF.
 
watakufanye njaa huku wamejazana bara wanalima mashamba makubwa wanaendesha biashara kubwa za kila aina tatizo hawapeleki pesa zanzibar bari kule kwa mjomba.
 
..kunaweza kukawa na viwango vya kodi wa wa-Zenj.

..halafu kikawekwa kiwango kingine kwa wa-Bara wanaotaka kuweka makazi na uwekezaji Zenj.

..haki itatendeka kama baada ya muda fulani wa kuishi Zenj, m-Bara akawa na haki sawa kama wa-Zenj, na kuruhusiwa kulipa kiwango cha kodi kinacholingana na wa-Zenj wengine.
 

Mbona unaleta CHANO hata pepo bado hajataja jina ?.....Mungano ni kama mapenzi ni jambo la hiyari na huwezi kulazimisha .umesahau pale Rais aliposema ndani ya Bunge wakati ule wa mjadala wa upatanishaji wa mpasuko kule zanzibar na wajumbe wa CCM kutoka ZANZIBAR wakatowa maneno ambayo yalishangaza bunge na hata kufikilia kusema wapo tayari warudi na ASP yao. Hakukuwa na mtu hata mmoja aliyeweza nyanyuwa mdomo wake kuikemea kauli ile, sasa jiulize kauli kama hii nani anaweza ingilia wakati imo ndani ya katiba ya SMZ.Tukirudia kauli ya kule bungeni hata Rais Kikwete aliwatetea wajumbe kutoka CCM ZANZIBAR, kwa kusema wajumbe wale wametumia haki yao kikatiba ,sasa na kwa kauli yao hii wanatumia haki yao kikatiba na kama hupendezewi ni vizuri ukanyamaza tu kwani wewe huzimi ,na wala huwashi inapokuja mamuzi yao serekali ya ZANZIBAR.
 

Naam na huu muungano uchwara unalindwa kwa kila hali na the so called viongozi wa chama na serikali ili kulinda maslahi yao. Watanganyika hatuutaki maana ni muungano ambao una kasoro chungu nzima ambazo viongozi hao wa chama na serikali wanazifumbia macho na pia hauna maslahi yoyote kwa Watanganyika, kwa mfano Z'bar pia imechangia sana katika matatizo ya TANESCO kwa kukataa kulipa mabilioni ya bills za umeme ambayo walitakiwa wayalipe kwa TANESCO.
 
Nadhani walichotakiwa kufanya katika kupanga gharama ya kodi ni kuweka makundi matatu, yaani wazanzibari, watanganyika(watanzania ambao sio wazanzibari) na wageni. Kuweka mgogo kundi moja na mjerumani si sahihi kisiasa. Ni vyema gharama hizi zipitiwe upya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…