KERO Soko la SIDO mkoani Mbeya na changamoto zilizopo

KERO Soko la SIDO mkoani Mbeya na changamoto zilizopo

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

jumamwaki

JF-Expert Member
Joined
Dec 4, 2017
Posts
244
Reaction score
225
Habari wapendwa.

Tukiwa tupo mbioni kumsaidia mh rais samia kwenye kuleta maendeleo kuna baadhi ya mambo ambayo huenda yanasababishwa na viongozi kwa kujua yaani makusudi au kwa kutojua.

Nianzie kwenye mambo yafuatayo kwenye jiji letu la mbeya ambayo kwa kweli yanakera sana .

#soko la sido ni miongoni mwa masoko makubwa nchini tanzania , soko ambalo lina utaratibu wa kila baada ya muda fulani kufanyika uchaguzi wa viongozi wa soko.

Lakini ni miaka mingi inaenda kukatika bila kufanyika uchaguzi wa viongozi wa soko.

Swali kwa mkurugenzi wa jiji.

Napenda kuuliza uongozi wa jiji la mbeya kwa kuanza na mkurugenzi wa jiji la mbeya .Swali langu ni moja tu

Je, unatambua kuwa ni muda umepita bila kufanyika uchaguzi wa uongozi kwenye soko la sido? Ikiwa unatambua kuna changamoto gani ambayo ni ngumu kuwashilikisha wananchi waliopo kwenye soko husika ?

2. Hivi karibuni uchaguzi uliiitishwa na ghafra ukahailishwa je unatambua hilo,

Ikiwa unalitambua kwa nini usiitishe kikao kuwaeleza wafanya biashara wa soko la sido kuhusu changamoto kama zipo .

3. Miundo mbinu ya soko la sido hadi maeneo ya kabwe .

Ni maeneo ambayo yanasahaulika sana kuhusu ukusanyaji wa taka , takataka zinawekwa kwa muda mrefu ukilinganisha na matumizi ya eneo husika na idadi ya watu wanaolitumia , hivi kwamba kuna muda unakuta harufu ni kali mno jambo ambalo huleta athari kiafya hususa ni kwa walio maeneo ya karibu na wauza vyakula .

4. Wezi na vibaka kuongezeka

Maeneo ya kabwe kwa sasa sio salama sana , kuna hatari sana mida ya kuanzia saa mbili na kuendelea watu wanaibiwa na kuumizwa

Kwa kweli mambo haya ni kero sana kwenye jiji la mbeya .

Tafadhari karibu kwa maoni mengine kuhusu jiji letu la mbeya .
 
Uchaguzi hufanyika kila baada ya muda gani?
 
Soko halina Meneja?

Kabla ya Mkurugenzi, kuna Meneja, Afisa Masoko, Afisa Biashara, na Mkuu wa Idara ya Biashara.

Hao wote wanahusika na Masoko. Mkurugenzi ni mtu mkubwa sana.

Halafu, ushuru mnalipa? Au ndiyo mnawanyanyasa hao wakusanya ushuru wa Jiji halafu mnataka maboresho ya soko?

Kwani bila kuwa na uongozi biashara haziendi?

Wafanyabiashara mnapenda sana siasa kwenye masoko badala ya kazi iliyowapeleka.

Mimi ninadhani Halmashauri iwaandikie barua za madeni yenu ya ushuru wa soko ili muwe bize kufanya biashara na kuacha kelele za uchaguzi.
 
Soko halina Meneja?

Kabla ya Mkurugenzi, kuna Meneja, Afisa Masoko, Afisa Biashara, na Mkuu wa Idara ya Biashara.

Hao wote wanahusika na Masoko. Mkurugenzi ni mtu mkubwa sana.

Halafu, ushuru mnalipa? Au ndiyo mnawanyanyasa hao wakusanya ushuru wa Jiji halafu mnataka maboresho ya soko?

Kwani bila kuwa na uongozi biashara haziendi?

Wafanyabiashara mnapenda sana siasa kwenye masoko badala ya kazi iliyowapeleka.

Mimi ninadhani Halmashauri iwaandikie barua za madeni yenu ya ushuru wa soko ili muwe bize kufanya biashara na kuacha kelele za uchaguzi.
Soko halina meneja?
Ushuru mnalipa?
Kwani bila kuwa na uongozi biashara haziendi?

Ningependa kukujibu baadhi ya maswali
1. Kuhusu soko kuwa na meneja ,
Kama ambavyo ktk taasisi mbali mbali na katika nchi yetu Kuna Sheria ambazo zimewekwa ili zifuatwe Kuna Sheria inataka kuwepo na uchaguzi wa VIONGOZI katika Masoko mbali mbali .
Sheria na taratibu za nchi zimefuatwa ndio maana kinahitajika kuwepo meneja.
2. Ushuru tunalipa ndio, na usipolipa unachukuliwa hatua , jambo ambalo ni Sheria pia zimewekwa kwenye masoko HUSIKA
3. Labda hujaelewa hoja yangu rudia kusoma kwenye hoja yangu.
Tatizo sio kuwepo VIONGOZI.
TATIZO ni kuwa Kuna utaratibu na Sheria kama ambavyo Rais huchaguliwa Kila baada ya Miaka mitano ,baada ya hapo uchaguzi hufanyika.
Lakini Kwa soko la SIDO ni tofauti. Viongozi wapo na Hawa waliopo waliwekwa na Kiongozi mmoja wa serikalini , kabla ya viongozi Hawa kulikuwa na Viongozi ambao walikuwepo Kwa kuchaguliwa na muda Wao ulipita ilitakiwa kuwepo na uchaguzi Mwingine ,
Miaka 6 Sasa inaenda hakuna uchaguzi uliofanyika kinyume na taratibu .
 
Soko halina meneja?
Ushuru mnalipa?
Kwani bila kuwa na uongozi biashara haziendi?

Ningependa kukujibu baadhi ya maswali
1. Kuhusu soko kuwa na meneja ,
Kama ambavyo ktk taasisi mbali mbali na katika nchi yetu Kuna Sheria ambazo zimewekwa ili zifuatwe Kuna Sheria inataka kuwepo na uchaguzi wa VIONGOZI katika Masoko mbali mbali .
Sheria na taratibu za nchi zimefuatwa ndio maana kinahitajika kuwepo meneja.
2. Ushuru tunalipa ndio, na usipolipa unachukuliwa hatua , jambo ambalo ni Sheria pia zimewekwa kwenye masoko HUSIKA
3. Labda hujaelewa hoja yangu rudia kusoma kwenye hoja yangu.
Tatizo sio kuwepo VIONGOZI.
TATIZO ni kuwa Kuna utaratibu na Sheria kama ambavyo Rais huchaguliwa Kila baada ya Miaka mitano ,baada ya hapo uchaguzi hufanyika.
Lakini Kwa soko la SIDO ni tofauti. Viongozi wapo na Hawa waliopo waliwekwa na Kiongozi mmoja wa serikalini , kabla ya viongozi Hawa kulikuwa na Viongozi ambao walikuwepo Kwa kuchaguliwa na muda Wao ulipita ilitakiwa kuwepo na uchaguzi Mwingine ,
Miaka 6 Sasa inaenda hakuna uchaguzi uliofanyika kinyume na taratibu .

Kinyume na taratibu zipi?
 
Kinyume na taratibu zipi?
Sheria inataka uchaguzi ufanyike Kila baada ya Miaka mitatu ,
Na anayesimamia Sheria hii ni Kuitekeleza na MKURUGENZI WA JIJI.
Ndiye msimamiaji wa shughuli zote za uchaguzi wa VIONGOZI Wa soko
 
Back
Top Bottom