Somalia ilivyoziokoa Tanzania na Uganda kutoka kwenye vita

Somalia ilivyoziokoa Tanzania na Uganda kutoka kwenye vita

..Obote alirudi madarakani baada ya uchaguzi mkuu.

..Museveni hakukubaliana na matokeo hivyo akaingia msituni.

..sio kweli kwamba Obote alirudi kwa mbinu za Nyerere au Tanzania.

..nakushauri ujisomee kuhusu Moshi Accord ambayo ni mazungumzo na makubaliano ya makundi ya Waganda kuunda serikali ya mpito baada ya Iddi Amin kupinduliwa.

..mazungumzo hayo yalifanyika mjini Moshi Kilimanjaro na yalikuwa Mzee Mkapa akiwa Waziri wa Mambo ya Nje alikuwa mwenyeji wao.

..Mazungumzo hayo yalizaa serikali ya mpito chini ya Prof.Yussuf Kironde Lule. Baada ya hapo akaingia Godfrey Lukongwa Binaisa. Huyo naye hakudumu akaja Paulo Muwanga.

..Baada ya uchaguzi mkuu wa vyama vingi ndio Milton Obote akarudi madarakani.

Asante kwa kulifafanua hilo [emoji120][emoji120]
 
..baada ya Mogadishu Peace Accord ya mwaka 1972 Tanzania iliacha kutoa mafunzo ya kijeshi kwa wakimbizi wa Uganda.

..hata Museveni ktk kitabu chake " Sowing The Mustard Seed " ameandika kwamba wakimbizi wa Uganda walikuwa wamekata tamaa ya kumpindua Iddi Amini kwasababu walikuwa hawana msaada toka kwa Tanzania.

..Hata Iddi Amin alipovamia Tanzania mwaka 1978 hakuwa akidai kwamba tulikuwa tunawasaidia waasi wa Uganda, bali alikuwa anadai kwamba eneo la Kagera ni ardhi / mali ya Uganda.

..Suala hili nakushauri utafute majadala iliyopita ya JF. Tulijadili vita vya Uganda, na sababu zake, kwa kirefu sana, na kwa hoja zilizofanyiwa utafiti.

cc Kichuguu, Nguruvi3
Ila mkuu lazima tukubali kuwa kama Nyerere asingewapa hifadhi kina M7 na wapinzani wa Amin huenda tusingeingia vitani na Uganda.
 
Ila mkuu lazima tukubali kuwa kama Nyerere asingewapa hifadhi kina M7 na wapinzani wa Amin huenda tusingeingia vitani na Uganda.

..Idi Amin alitaka kupigana vita na Kenya mwaka 1976.

..ukichaa wa Amin ndio uliosababisha vita vya 1978.
 
Back
Top Bottom