Son of Ex-Minister Malima in historic medical discovery

Dada dini inaku brain wash vibaya mno.... hata hivyo Asanterabi ni jina la kikristo...check it out!
Mkuu Mirisho, asante, ila nadhani hili jina ni la dini zote, I have a friend ni Muislamu anaitwa Asanterabi Tambwe, na nikiwa Boston, nilikutana na Mbongo Mkristo akiitwa Asanterabi Nsilo Swai, wanamuita kwa kifupi Asante! na alilipata hili jina kutoka kwa baba yake, yule waziri wa kwanza Mchagga, Asanterabi Zephaniah Nsilo Swai (RIP) ambaye Mwenyekiti wa sasa wa CCM Kilimanjaro, Mama Vicky Nsilo Swai ni mjane wake ambaye ndie mama yake Asante!.
Pasco.
 
CC: chrisslukosi achana na kubeba maboksi unaliletea taifa aibu.ona wenzako wanavyopambana.
 
Last edited by a moderator:
Pasco,

Nawafahamu watoto wake Adamu, Amani, akilimali, na huyu mdogo wao Asanterabi,kasoma Azania kisha kasoma Aga Khan, kazaliwa mwaka 1979.
 
Last edited by a moderator:
Wakati nasoma hu uzi nilitegemea kabisa kwamba lazima baadhi ya wachangiaji wachangie kwa mtazamo wa kidini, nazidi kujithibitishia mwenyewe kua akili zetu wabongo hazipo sawa kabisa, kwasasa nafanya research ya kwanini akili zetu zipo hivi, si amini katika uchawi though jamaa yangu 1 alinambia eti mwenge wa uHuru ni tambiko la kuondoa akili zetu, mi natafuta sababu za kisayansi zaidi, nataka nianze na hivi vyakula tunavyo kula, nahisi Sembe na mchele (White rice) vina issue! Sio bure, tunalo tatizo!
 
Khaa!!! Wewe wa wapi?? Sayansi bongo?? Una wazimu wewe. Bongo kila kitu siasa. Wanakesha wakiomba ebola iingie nchini wafanye siasa. Siasa ni kila kitu kuanzia usafi wa mazingira hadi kikombe cha babu. Ndiyo tulivyojichagulia.
 
We ujuwe kuwa si ajabu kugundua kitu. Hewa unayovuta ni wazungu hao ndo wanakwambia inamchanganyiko gani.

Lakini cha msingi, elimu hii ambayo unaona ya Wakiristo ndo unasifia. Kwa hiyo tungeanza kuorodhesha mangapi yaliyofanya na Watafiti wa Kikiristo????

Obviously ni yote.

Waza kimaendeleo zaidi na si kidini.

Wengi hawaitaji kutaja dini kwenye masuala ya maendeleo.

Naona umeshaamua kuwa kila mzungu si Muislam? au sio?

 
Mkuu nashukuru me wa Bongo tu. Angalia nilichoandika!!!! Bongo siasa ndo kila kitu ndo maana hatuna mipango na sera za maendeleo zinazoelezea jinsi ya kutumia rasilimali tulizo nazo.

Haya unayoona ni opportunities ambazo wenzetu wamepata, pengine kwa sababu ya familia zao au kwa siasa zetu.

Na mimi binafsi sioni cha ajabu, maana vitu kama hivi wanafanya undergraduate China, Singapore, India, Korea na Japan.

Khaa!!! Wewe wa wapi?? Sayansi bongo?? Una wazimu wewe. Bongo kila kitu siasa. Wanakesha wakiomba ebola iingie nchini wafanye siasa. Siasa ni kila kitu kuanzia usafi wa mazingira hadi kikombe cha babu. Ndiyo tulivyojichagulia.
 
Pasco,

Nawafahamu watoto wake Adamu, Amani, akilimali, na huyu mdogo wao Asanterabi,kasoma Azania kisha kasoma Aga Khan, kazaliwa mwaka 1979.
Mkuu Ritz, asante. Kumbe jamaa alikuwa dogo sana ndio maana sikumfahamu kwa sababu mpaka tunamalima primary na Amani, dogo bado hajaanza shule!, ila nimemkumbuka Akili alikuwa nyuma yetu!.

Ila pia nimefuraha kutambua ndugu wengine wa familia hiyo, baba akiitwa Ali, watoto Adamu, Amani, Akili na Asante!.

Thanks.
Pasco
 
wanamjuaje??

Alikuwa mwanafunzi bora wa mwaka huo na si hilo tu pia ndio mwanafunzi bora kutoka africa kupata kutokea.media za uturuki zilimtangaza sana na hapo heshima ya watanzania iliongezeka wakati tunaenda kusoma uturuki kwa sifa alizoziacha.
 
Hongera Son,
Lakusikitisha sana kuwa baadhi humu wachangiaji mumegeuza uzi na kuonyesha ujinga na upuuzi mlonao !!! Very sad..
 
Jaman! Hii imegeukaje kuwa ya kidini? tunaitana majina mabaya, makali kwan shida n nn?
Huyo kafika huko si kwa ajil ya dini bali ni juhudi zake na uwezo wa familia. Maana kuna wengi tunao wa iman mbalmbali wakifanya ugunduzi mitaan ila hawana kiwezeshwa na serikal wala jamii inatowazunguka. Na pia kuna watoto wa viongozi ambao wako huko pamoja na kuwa na fursa hamna walilolifanya zaid ya kupiga picha.

Wanadin msituharibie thread kwa kweli, tuko watu katika nchi hii bado tunaamin inawezekana kufikia maendeleo kama vitu flanflan vitabadirika. Huyu kijana ametuthibitishia kuwa ipo hazina kubwa katika nchi yetu , swali ni tunafanyaje ili kiwawezesha wafikie malengo yao katika ubunifu na uvumbuzi?
 
Kwani umeona hii ndo breakthrough kwako. Hakuna jipya mkuu. We dini inaanzia wapi zaidi ya kujua alichofanya. Mangapi yanafanyika?? Unawajua wamasai mapacha wanaosoma Havard!!!! Wameleta model ya kutengeneza Magari Chuo Kikuu cha Mandela-Arusha.

Najua kuna wengi sana, ila nchi ndo imelala.
Teh teh teh.

Hao wanajua kuwa hakuna wazungu waislaam.

Pua wanadhani kuwa hakuna waarabu ambao ni wakristo teh teh teh
 
Teh teh teh eeeeeh!!!

Naona ndo wa kwanza. Wote wanaojadili hili ni wale wasiojua hata principles za "sensor" Nenda NIMR pale OBAMA Rd au Amani Tanga, utaona watu wanatengeneza "diagnostic kits" ambazo hapa mnaona sayari nyingine imegunduliwa na MTZ.

Wengi mtajua.
Ugunduzi wa muislam!
 
Huyu kijana ni moto tena wa kuotea mbali sana watanganyika msianze siasa zenu za udini hapa,jamaa kaipandisha nchi yetu mahali pazuri sana na tutaheshimika kwa hilo,ametufagilia sisi wote pamoja na watoto zetu au kizazi chetu ,

Halafu hakuna mkristo au muislam hapa bali ni mtanzania ndio kashinda hiyo tuzo so punguzeni tabia za kuuweka udini mbele hapa,kumbukeni mbongo ni mbongo tuu. Tulikula unga wa njano pamoja na kukombania mikate na vyakula kwa pamoja pale national milling.

Au katika maduka ya ushirika hata vita tulipigana kwa pamoja,wakristo kule vitani na waislam wote walikuwa wakipeana zamu kuomba mungu au kufanya ibada na mori wetu wa kupigana vita ulikuwa hauna dini tulizipiga kwa nguvu na ari kubwa sana na hata hivi sasa yeyote atakaye tujaribu asitegemee atapigana na jeshi lisilokuwa na umoja.

Atakutana na watanzania wenye upendo na imani na nchi yao,acheni tabia za kudharauliana kwa kupitia imani ya mtu.Hongera sana bwana Asante Rabi hata marehemu Proffessor Kighoma kafurahi sana huko aliko na anazidi kukuombea mungu uliendeleze libeneke.M/Mpamba
 
Hawa mabwana wa COSTECH hawana hata chembe ya aibu? Wao wamefanya nini kuhusu state of research in TZ at the moment?kila siku ni warsha na makongamano,then Mtanzania anafanya vizuri nje ya nchi wana-jump the wagon ili waonekane kuna lolote la maana wanafanya.

It's time COSTECH reasses its position in contributing to the development of this country, rather than being a money pit it currently is.
When was the last time a world class research work has been sponsored by COSTECH?
 

Utataja majina mpaka mate yakauke. (Waminsharrir hasidin idhaa hasada)

Kuna maneno mazuri sana yanasema hivi kwa lugha ya kiungwana
"Walaa yazidu llahu Dhalimuuna illa khasara".
Katafute maana yake. Huenda ukafunguka macho Pasco mwana wa mayala.
 
Last edited by a moderator:
nawaza kwa nguvu huyu lazima alitokea ukerewe bhana na sio mkuranga................huko ni mzamiaji kama mr mtembei wa bukoba.....dr kairuki etc
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…