Songea: Waumini wachoma Kanisa kwa hasira baada ya Padre kukataa kwenda kumzika muumini

Songea: Waumini wachoma Kanisa kwa hasira baada ya Padre kukataa kwenda kumzika muumini

Hii taarifa nafikiri ipo nusu nusu ila pia mpaka raia kufikia walichokifanya kimechagizwa na chuki iliota kwa muda mrefu baina ya viongoz wa kiroho na watu wa kawaida.

Kuna muda baadhi ya mapadri/viongozi wa kiroho wamekuwa wakijisahau na kuonyesha madhaifu yao wazi wazi.

Kanisa lijifunze kwa tukio hili dogo ilikuendelea kuleta umoja lasivyo mambo yatakuwa magumu sana mbeleni
Hawa jamaa wanabebesha mimba watoto wa watu na kisha kutekekeza watoto wao!
 
Umeme hamna, Maji hamna, Padre nae anataka kutuchanganya akili alaaaa!
 
wamekosea sana kuchoma nyumba ya ibada.
maana hiyo sio nyumba ya Padre.
JNi kosa kujichukulia sheria mkononi.
ni bora wangemtenga Padre kwa kususia kwenda kanisani badala ya kuchoma.
Jingaz sana hao jamaa! Halafu si watakuja kulijenga wenyewe bure kwa mpango wa kujitolea??
 
Hawa jamaa wanabebesha mimba watoto wa watu na kisha kutekekeza watoto wao!
Hilo ni kosa padri akifanya hivyo inabidi asaidiane na mwenzake kulea kama kawaida na endapo mdada akipigwa mimba na uhakika ni ya padre anapaswa kufika kwa dekano au paroko wa parokia jirani kuelezea tukio iliutaratibu wa kusimamia malezi ya mtoto ufwate ....
 
Padre alikataa kwenda kumzika muuamini (sababu bado haijajulikana), waumini wamezika baada ya kumaliza kuzika wakaenda Parokiani wakachoma kanisa kwa hasira.


View attachment 2016428
RC tunaowafahamu sote wamefikia hatua hiyo!!! Yaani waunguze kanisa na sanamu ya bikira maria ndani!!! Sitakaa niamini kama hao ni wakatoliki
 
Duu!!! Mleta mada tusaidie kujua sababu za baba Paroko kugoma kuendesha ibada ya mazishi ili tutoe maoni yetu.
Kama marehemu alikuwa mwanamme huenda alinkwaza paroko hukooooo ntaani na kama alikuwa mwananke huenda alinkataa paroko
 
Binadamu ni wajinga sana. Sasa Padre au shekhe kumzika mtu kuna faida gani?
Inategemeana na mambo wanayowahubiria, yakiwaingia sana ndiyo hayohayo yanageuka kichocheo cha yaliyotokea
 
Kuna harufu ya aliezikwa hakuwa mchangaji/mhudhiriaji mzuri wa parokiani au ana lake na Paroko wa pale.

Vyovyote iwavyo tukio hilo wangefanya wale wengine,
Wangeitwa MAGAIDI tu humu.
 
Alafu ukute wahuni wa mtaa ndiyo walikua mbele ambao hawaoni uchungu wa michango yao ya ujenzi😂😂
Issue sio michango, watu wamejenga kanisa kuwasaidia changamoto zao za kiroho linapokuwa
linazidisha matatizo yao halina maana tena.
Na msimamo wa padre hauwezi kutofautishwa na msimamo wa kanisa.
 
Sababu kuu ni pesa!! Kanisa limekuwa na muelekeo wa kipesa zaidi kuliko ibada . Kuna michango mingi sana na mingine imehamishiwa kwenye jumuiya kwa lengo la easy monitoring.

Mfumo huu unachagua sana watu , watu wenye influence wanazikwa hadi na maaskofu hata kama walikuwa hawakanyagi kanisani, nina mifano kadhaa kwa hilo ,

On a serious note, swala la
Kutimiza au kutotimiza masharti ya kanisa mtoa hukumu ni mwenyezi Mungu , sio padri au die hard pilgrims, Rc mmejipa majukumu ya kimungu kwa watu wanoondoka hapa duniani.
Hapo kwenye watu wenye influence umenikumbusha mzee Kingunge RIP.
Kanisa linajinasibu kuhubiri haki na upendo lakini matendo yake ni mbingu na ardhi.
 
Back
Top Bottom