Songwe: Miili mitano yaokotwa msituni

Songwe: Miili mitano yaokotwa msituni

Boran Jakutay

Senior Member
Joined
Apr 8, 2023
Posts
110
Reaction score
259
1683809804659.png

WINGU jeusi limetanda wilayani Mbozi katika Mkoa wa Songwe baada ya miili ya watu watano wasiofahamika kukutwa imetupwa kwenye msitu wa Mlima Senjele pembezoni mwa Barabara Kuu ya Tanzania na Zambia (TANZAM).

Miili hiyo ambayo ni ya wanaume wanaokadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 25 na 30, inadaiwa kutupwa katika eneo hilo usiku wa kuamkia jana na watu wasiojulikana.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Songwe, Kamishna Msaidizi (ACP) Theopista Mallya, alisema miili hiyo ilikutwa jana asubuhi na kuchukuliwa kwenda kuhifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi.

Alisema chanzo cha vifo vya watu hao hakijulikani na kwa sasa wanasubiri taarifa ya kitabibu kutoka kwa madaktari ili wajue kiini chake.

Chanzo: Gazeti la Nipashe
 
WINGU jeusi limetanda wilayani Mbozi katika Mkoa wa Songwe baada ya miili ya watu watano wasiofahamika kukutwa imetupwa kwenye msitu wa Mlima Senjele pembezoni mwa Barabara Kuu ya Tanzania na Zambia (TANZAM).
Mwendazake karudi tena!? Maana tuliaaminishwa na watu flani flani kua Mwendazake alikua Dikteta!!
 
Wale jamaa wa maridhiano watatuambia wahusika maana hakuna wasiojulikana kwa sasa!
 
Mwendazake karudi tena!? Maana tuliaaminishwa na watu flani flani kua Mwendazake alikua Dikteta!!
Jinsi alivyoendesha chaguzi za serikali za mitaa 2019 , uchaguzi mkuu 2020 na zile chaguzi ndogo.
 
Sio miili ya Waethiopia ama Wasomali kweli? Maana hio njia huwa inasafirisha sana wahamiaji haramu na in most cases wanakosa hewa humo wanamohifadhiwa.
 
Mwendazake karudi tena!? Maana tuliaaminishwa na watu flani flani kua Mwendazake alikua Dikteta!!
Ningeshanga nisingeikuta hii komenti, wafuasi wake mko kama mmeprogramiwa.
 
Sio miili ya Waethiopia ama Wasomali kweli? Maana hio njia huwa inasafirisha sana wahamiaji haramu na in most cases wanakosa hewa humo wanamohifadhiwa.
Ingekua wasomalia wangesema, so hao ni watanzania. Magufuli muuaji karudi tena?
 
Watatoa taarifa kamwe hawatasema ukweli na Hiyo ndio inaitwa Taarifa ya Habari.
 
Back
Top Bottom