KERO Songwe: Vyoo vya Stand ya Mabasi ya Tunduma ni vichafu sana

KERO Songwe: Vyoo vya Stand ya Mabasi ya Tunduma ni vichafu sana

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mwanongwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2023
Posts
611
Reaction score
567
Waungwana hivi zile pesa tunazolipa wakati wa kuingia kwenye vyoo hasa maeneo ya Stand zinafanya kazi gani?

Maana vyoo vingi vya Umma vina changamoto ya usafi na ukosefu wa maji bila kusahau ubovu wa miundombinu, nimeona mara kadhaa hapa JF watu wamekuwa wakiripoti kero hiyo kisha kisha wenye Mamlaka wanajitokeza kufanya usafi, kwanini iwe hivyo kila mara?

Nikiwa katika safari zangu nikapita Stendi ya Mabasi ya Tunduma pale maeneo ya Mpemba, nikaingia Chooni mimi na abiria wenzangu, tulichokikuta huko kwa kweli hali ni Mbaya kutokana na mazingira mabovu.

Vyoo havina majina, milango ni mibovu, vyumba vingine ndani ya choo havina milango kabisa, mapima yanayotumika kuhifadhi maji ni machafu kama ilivyo kwa ndoo zilizomo humo ndani lakini ajabu zoezi la kukusanya pesa linaendelea kama kawaida.

Nililipa Shilingi 200 kuingia lakini nilichokiona ni kama nililipa hela ili niingie kupata magonjwa ya kuambukiza ndani ya vyoo hivyo.

Halmashauri ya Mji wa Tunduma tunawaomba basi jitahidini kuweka miundombinu ya maji kwenye hizo Toilet, lasivyo mnakaribisha magonjwa ambukizi.

DSC_0536~2.JPG
DSC_0531.JPG
DSC_0529.JPG

DSC_0525.JPG
 

Attachments

  • DSC_0530.JPG
    DSC_0530.JPG
    296.3 KB · Views: 4
  • DSC_0526.JPG
    DSC_0526.JPG
    348 KB · Views: 5
  • DSC_0525.JPG
    DSC_0525.JPG
    384.2 KB · Views: 7
Hizo hela wanagawana tu. Huduma nyingi za umma ni chanzo cha mapato kwa wenye mamlaka na wala sio huduma kweli kwa umma.

Ila pamoja na hayo watu weusi ni wachafu na waharibifu sana. Huwa hatuna utamaduni wa kutunza miundombinu ya umma.

Miafrika ndio tulivyo.
 
Hizo hela wanagawana tu. Huduma nyingi za umma ni chanzo cha mapato kwa wenye mamlaka na wala sio huduma kweli kwa umma.

Ila pamoja na hayo watu weusi ni wachafu na waharibifu sana. Huwa hatuna utamaduni wa kutunza miundombinu ya umma.

Miafrika ndio tulivyo.
Kabisa
 
Back
Top Bottom