Nisielewe Kiswahili kwa sababu tu ya nukuu ya Kilatini? Nimekuelewa fika. Kwamba si juu ya Kiongozi kujibu kila habari inayovuma. Wewe ndiye hujanielewa. Kwamba hii ya Niyo na Ngoma kujiunga na Simba kama mkakati wa timu kujiimarisha na kufanya vyema kwenye mashindano ya kimataifa kutokana na fedha ya Mo Dewji si kama hizo habari nyengine. Ni miongoni mwa hizo habari muhimu zinazohitaji ufafanuzi - au ukanushi - ili kutowachanganya wachezaji waliopo na wapenzi/washabiki wasichanganyikiwe kisaikolojia pale tamaa yao itapokuja kutamauka, kama ilivyotamauka kwa swala la Ngoma. Kama unafahamu Kiswahili vyema nadhani umenielewa.
Wanachama na wapenzi wa timu ya Simba Sports Club.
Wakitaka habari za usahihi huwa wanazipata toka katika uongozi wa Simba sc.
Au
Kutoka kwenye vyanzo vya habari vya timu.
Uongozi wa Simba sc, haujawahi kutoa habari za kuwasajiri wachezaji unaowaongelea.
Wala kocha hajawahi kuwahitaji.
Wala vyombo vya habari vinavyotambuliwa na wanasimba kama Simba Blog, Msemaji wa timu nk. havijawahi
kuzungumzia usajiri wa hao wachezaji unaowasema.
Sasa
wewe ndugu unachukua habari unakokujua halafu unawa lazimisha viongozi wa Simba sc wazijibu. Ni jambo la kustaajabia.
Ivi wewe hizo habari umezipata wapi ? Na nani alizipeleka huko.
Mnaandika habari huko mnakokujua bila kushirikisha viongozi wa Simba, halafu mnawalazimisha wazijibu.
Ivi mliwashirikisha kuziandika ?
Kwanini msizijibu wenyewe mliozitunga ?
Naomba hizo habari uzijibu wewe maana naona unazijua kwa undani,
Sisi huku Msimbazi hatuzijui hizo habari na wala hatujasema popote kuhusu huo usajiri.
Unaelewa kiswahili au mwenzetu ni
Mlatino.