Sophia Simba, Madabida wavuliwa uanachama CCM. Emmanuel Nchimbi apewa onyo kali

Sophia Simba, Madabida wavuliwa uanachama CCM. Emmanuel Nchimbi apewa onyo kali

Mlipobadilishiwa katiba ya chadema na kumpa uenyekiti endelevu Mbowe kwenu ilikuwa raha na kawaida na hamkuhoji, iweje unakuja na day dreams!! Eti akisema aongezewe! Wakwenu aliyekwishajiongezea haumsemi! Ndio maana mnaitwa nyumbu!
Hapo hadi kichwa kinakuuma ila hauna namna.
 
Hakuna kinachobadilika, ni kiini macho tu. CCM imeshafikia maturity level katika siasa za nchi, it started with "party-state" (1961-64), ikashindwa, ikahamia kwenye "developmental state" (1965-1984), ikashindwa, ikahamia kwenye "contracting state" (1985-2015), ikashindwa, sasa chini ya Populist Magufuli inarudi back to "party state" era, na mbaya zaidi without any practical ideology. CCM kwa sasa ni genge tu waiting for the populist personality to do anything that helps the party make to the next day.

Hakuna kitu hapo.

Kama huyaelewi niliyojadili, Nina uzi nauandaa wenye lengo la kuelimisha wana JF jinsi gani CCM is running out tricks, and how Magufuli has defined its down fall.

Nitakukaribisha.
Nikaribishe na mimi mkuu,asante.
 
Mkuu uko sahihi. Jana Humphrey Polepole alijiikanyaga sana alipoulizwa sababu ya mabadiliko hayo ndani ya CCM. Ukweli ni kuwa hapo hakuna mabadiliko ya ukweli kutokana na kwamba mabadiliko ndani ya Chama lazima yawe ya kiitikadi zaidi ili kukiwezesha chama kutekeleza majukumu yake na kukabili changamoto zinazojitokeza katika kuleta maendeleo ya nchi. Lakini hapa mimi silioni hilo. Na kwa kweli kuna mambo ya kuleta wasiwasi. Kwanza kukosa uvumilivu wa kusikiliza mawazo mbadala. Chama lazima kiruhusu mambo hayo hasa kwa ngazi ya Wenyeviti na Makatibu. Nyerere alifanya hivyo na Chama kiliimarika sana. Hii ya concentration of power at the top bila grassroots representaion itaua Chama. Pili CCM wadefine ideology yao ni nini na wanataka kufanya nini. Ningetegemea katika kikao hiki at least wangetoa angalau mwelekeo wa kiuchumi w nchi. Tatu katika kutathmini Uchaguzi uliopita CCM ingeachana kabisa na witchhunting kama ilivyofanya. Uongozi umekuwa na hasira sana kuhusu hao "wasaliti" kiasi cha kwamba tathmini halisi ambayo ilitakiwa kufanywa haitafanyika. CCM wangejiuliza kwa nini wameshindwa katika miji yote mikubwa Tanzania Bara na Visiwani? Dar, Arusha,Mwanza(ilirudi dakika za majeruhi), Mbeya, Iringa, Tanga na Mtwara kote huku Chama kiko hoi. Kujikita kuwafukuza akina Sophia Simba watu ambao wamekitumikia chama maisha yao yote naona siyo busara. Niwatakie kila la kheri!
[emoji106] [emoji106] [emoji106] [emoji106] [emoji106] [emoji106]
Bora CCM wameamua kuvua unafiki ....wapinzani wanaibeza CCM inayojitengeneza ...watatutawala hadi labda wajukuu zetu wajielewe lakini si upinzani huu uliojaa ujanja ujanja ....
 
Mkuu Richard ngoja ngoja nikudadavulie kwa ufupi sana kuhusu huyo mama.

1.Kwanza anaitwa Jesca Msambatavangu. Alikuwa diwani wa ccm kata ya miyomboni mkoani Iringa.

2. Pili anakaaa Iringa mjini pale mitaaa ya uhindini (Karibu na duka maarufu la miyomboni pharmacy mujini Iringa). Vijana wa kitanzini wanajua vema, mshindo , makorongoni mpaka pale ofisi yakel ilipo mitaa ya saba saba. Opposite na makaz salim asas wa asas milk.

3. Amesoma elimu ya kiutu uzima Q.T pale Iringa , akasoma shahada /degree ya kwanza chuo kikuu cha Tumaini -Iringa. Pia masters yake kachukua pale pale , nitafatilia zaid kwenye vyanzo vyangu kama alifanikiwa Kuhitimu PhD pale Tumaini maana kuna kipindi alikuwa anachukua shahada ya uzamivu (PhD).

4. Aliwahi kuingia mgogoro na mama Monica mbega (former MP -Iringa constituency) ,pia mkuu mwakalebela Utakuwa naye anamkumbuka kwa namna alivyomletea zengwe kwenye kupitishwa kugombea ubunge , Mzee asas wa Asas dailies anajua vema.

5.Aliwahi kufundisha kuuza vitumbua na maandazi mpaka pale alipokutwa na mzungu akiwafundisha watoto wa hali ya chini lugha ya malkia licha ya yeye kuishia la7 tu ,ndipo alipopata wafadhiri wa kumjengea shule niliyoitaja pale juu.

6. Ni mama mjasiriamali mzuri sana na mpambanaji wa uhakika. Muulizs jah pipo wa makambako (sanga deo).

7.Ukibisha na hata ntafunguka zaid juu yake. Twende kazi.

NB: siyo kila unayemuona humu JF ukadhani ni wa kijiweni.

4.Ni mmiliki wa while maarufu sana Iringa ijulikanayo kama star international...nkwa kweli ni while bora kwa wale wazee wa shule za hi...madam, gd morning dad, etc.


Nimekuelewa mkuu ila nilipata jina la Joyce Msavatavangu kutoka katika mtandao wa Hakingowi na chanzokingine na wakimtaja huyo mama kwa jina la Joyce lakini kwa mara ingine tena vyanzo hivyo haviko sahihi.

Nimethibitisha pia jina hilo kutoka katika tovuti ya CCM Iringa hivyo hakuna matata.

Wewe si wa kijiweni wala sina shaka nawe kabisa.

Kwa kiingereza twasema, "no bad feelings".

CCM oyeeee!!
 
CHADEMA ni chama kinachojitabua na watu wanao jielewa na mchango wao tumeuona hata bungeni sio kulalia 'unafiki' kama kijani. Tuipe muda bado kuna mazuri mengi. Badi ni mfano wa kuigwa kwa kuonyesha upinzani thabiti.

Sio CHADEMA wala Sio CCM, tena afadhali huku CCM kwa sasa wanafagia fagia hakuna anaeona vizuri hasa watu wa chini wapo tu tunakoenda ndio huko huko, utamshangaa mtu wa CHADEMA pove linamtoka utadhani kwake hakuna udikteta, tena huyo Tundu Lizu nani wa kupinga wazo lake, semeni ukweli? Na Mbowe nani wa kumkosoa kwa sasa? Si umeona waliojaribu yaliyowakuta, na najua hamna uchaguzi wa Mwenyekiti tena dah...

Siasa za Tanzania ni bora wale wasio na vyama lakini hawa mashabiki uchwara ambao hata katiba za vyama vyao hawazijui ni shida... wako kusubiri nani wa kumtukana na kuongea USHILAWADU badala ya kujadili hoja za msingi kwa maendeleo ya taifa hili..

CCM acha ifagie, wakimaliza tunasubiri kama CHADEMA na nyinyi mtafagia au hayo makombo waliotupa chini CCM ndio mtaokota kama kawaida yenu?

Maana hamtaki kujibidiisha na nyinyi mkae mezani mle chakula fresh sijaona hata program za kuelemisha vijana wenu kuhusu maono ya CHADEMA kila siku viongozi wenu kwenye makorido kulinda nafasi zao kwa kutafuta kashfa ya mahakamani au ya kuuchafua utawala, huku mkipata washabiki badala ya wanachama watakao kijenga chama.
 
Walipewa nafasi kujitetea kweli? Au ilikuwa ubabe ubabeni...anyways hichichama kinakoelekea Ni korongoni na Hamna kinana wala nape atayeweza kukikomboa tena. Huyo mwenezi mwenyewe Ni serikali tatu na anapingana na misimamo mingi tuu ya chama
 
Dikteta uchwara katika ubora wake hataki kupingwa! Lakini wakati huo huo bado kawakumbatia wahuni, majangili, wezi, wapokea na watoa rushwa, wafitini na mafisadi ndani ya chama. Kama ilivyomshinda nchi chama pia kimemshinda kukiendesha huyu mkurupukaji.

Utaishia kutukana na tukisoma bandiko zako tunakuonea huruma, unavyojiamini kwa lugha chafu.
 
Mwanri si yeye bali Majaliwa ndiye aliforce awepo tu. Mwanri na Majaliwa wote walikuwa manaibu ofisi ya Waziri Mkuu na walikuwa marafiki wazuri tu..

OK, endeleeni kula mema ya nchi.. 2025 pia alete zengwe ahakikishe mrithi anatoka hukohuko kanda pendwa..
Vipi Sendeka...?! Hao walimpigania sana jamaa mpaka wakapigwa chini ubunge...

Unajua kila mtu anakuja na watu wake anaoamini atafanya nao kazi na zitaenda vizuri, ndio maana hata Kimei yupo na watu wake na mambo yanaenda shwari tu...

Kipindi kile huku hadi wale ccm wenzake wote waliungana aisee ilimgaragaza mbaya sana...

Hivi ni kweli ilisha nenwa rais hawezi toka kanda chukiwa...?! Au ni uzushi tu...?! Na kwanini inenwe hivyo...?! 2025 labda itarudi kusini ama pwani kama kawaida...

Kanda Pendwa wametoka marais wawili tayari, Pwani Wawili tayari, Kusini Mmoja...
 
Siku zake zinahesabika
Kuna kosa gani mbunge wa CCM kuikosoa serikali yake au kutoa maoni yake ambayo wakati mwingine yanaweza kupingana na baraza la mawaziri hasa endapo mawazo yake ni ya tija kwa taifa?
 
Back
Top Bottom