Special thread: Kilimo cha umwagiliaji (Irrigation)

Special thread: Kilimo cha umwagiliaji (Irrigation)

Mkuu kabla ya yote lazima ujue spacing ya zao lako!! Ukishajua...then ujue eneo lako ni eka ngapi!!! ...na kuhusu kudumu kwa drip ina tegemea ..je utazukia au utaweka juu...na je mazingira yakoje??? Jua kali..zinakanyagwa mara kwa mara!! ?? Ngoja nikitulia ntakuja na data kamili!!!
Haujatulia bado mpaka leo Mkuu??
 
Njoo tulime kilimo chetu.
Drip zipo za level mbalimbali kulingana na level ya mkulima kuanzia Mil 1.8/Acre ambazo hazina dripper ambazo huwa zinasaidia flow ya maji japo zinahitaji shamba ambalo halina miinuko....mpka Mil 10.0/Acre.
Kwa utaalamu zaidi nicheki inbox.
 

Attachments

  • 1478360757642.jpg
    1478360757642.jpg
    78.7 KB · Views: 312
Mkuu usihofu...bado nipo...!! Wiki hii ntaanza na basics (somo la kwanza) kabisa on what to consider kuanzia gharama...mazingira na kila kitu kama unataka kuanza kilimo cha umwagiliaji!!! Nadhani itakua mada nzuri kwetu!! Ntaku tag mkuu
Itakuwa vyema sana mkuu Upepo wa Pesa. Mi mwenyewe niko na shamba langu la ekari 10 linapakana na mto wenye maji mengi muda wote huko Kilosa. Ningependa nijue ABCs za kilimo cha umwagiliaji kabla sijaanza uwekezaji.
 
Njoo tulime kilimo chetu.
Drip zipo za level mbalimbali kulingana na level ya mkulima kuanzia Mil 1.8/Acre ambazo hazina dripper ambazo huwa zinasaidia flow ya maji japo zinahitaji shamba ambalo halina miinuko....mpka Mil 10.0/Acre.
Kwa utaalamu zaidi nicheki inbox.
Inbox tutaibiana,
We fafanua hapa, dripper ni nini??
Na tuseme heka oja ya nyanya inahitaji drip tapes za urefu gani jumla??
 
Inbox tutaibiana,
We fafanua hapa, dripper ni nini??
Na tuseme heka oja ya nyanya inahitaji drip tapes za urefu gani jumla??
Swali lako la kwanza ...dripper ni kile kitundu au kifaa kinachotoa maji kwa matone kwa jina lingine kinaitwa emitter!!

Swali la pili ni hesabu tu ya kawaida...ngoja ntakuja na jinsi ya kusolve mkuu Shark
 
Itakuwa vyema sana mkuu Upepo wa Pesa. Mi mwenyewe niko na shamba langu la ekari 10 linapakana na mto wenye maji mengi muda wote huko Kilosa. Ningependa nijue ABCs za kilimo cha umwagiliaji kabla sijaanza uwekezaji.
Wala usihofu mkuu nikiweka ntaku tag!! Karibu
 
Mbona maswali ya msingi hayajibiwi kikamilifu? Roller 1 ya drip pipe ina urefu gani na bei yake ikoje?
 
Mbona maswali ya msingi hayajibiwi kikamilifu?
Tusamehe kwa hili mkuu.
Roller 1 ya drip pipe ina urefu gani
Roll moja ya drip line/pipe ina tegemea na wewe ulivyoagiza kiwandani ila nyingi za madukani ni kuanzia mita 1000. hizi roller ziko za urefu tofauti tofauti inategemea zilivyoagizwa.
na bei yake ikoje?
kwa 1000 mita inaanzia laki tatu mpaka nne kulingana na sehemu ulipo mkuu!
 
SEHEMU YA KWANZA.

MAMBO YA KUZINGATIA UNAPOTAKA KUANZA KILIMO CHA UMWAGILIAJI!

Habari wana jamvi…

Awali ya yote naomba mnisamehe kwa kuto fulfill my promise kushindwa kuweka somo kila wiki kama nilivyo ahidi, okey leo nlitaka kushare nanyi kitu cha kwanza ambacho mtu anatakiwa kumbuka kama anataka anzisha kilimo cha umwagiliaji. Tumeshaona maana ya kilimo cha umwagiliaji katika pati ya utangulizi, sasa leo nlitaka tujadili mambo machache ambayo ni vyema yazingatiwe pale mtu anapotaka kuanzisha kilimo cha umwagiliaji!

1. Maji na upatikanaji wa maji (availability of water)

Maji katika kilimo cha umwagiliaji ni kama mafuta kwenye gari, kwa lugha ingine kilimo cha umwagiliaji hakiwezi fanikiwa kama hakuna maji tena maji bora nay a kutosha (quality and quantity)! Kuna madhara makubwa sana ambayo yanaweza tokea kama ubora wa maji (quality) ukiwa mbovu, kwa mtazamo wangu haya ndiyo mabaya Zaidi ya yote katika kilimo cha umwagiliaji…embu angalia mashamba kama lower moshi na tpc ambayo kwa kiasi kikubwa yameathiriwa na magadi/chumvi chumvi (salinity)!! Japo tunahitaji maji kwa umwagiliaji ila maji haya yasipo angaliwa yanaweza kuwa bomu baya sana kwa kilimo!! Katika part hii pia ni vyema kujua allocation ya chanzo cha maji, je kipo karibu au mbali na shamba husika!!! Je kipo mlimani au mremkoni??

2. Aina ya zao (crop type).

Tukishajua upatikanaji wa maji,sasa ni vyema tukajifunza kwanini ni vyema kujua aina ya zao kabla yaku set sistimu wa umwagiliji. Mfano kuna mazao ambayo ni lazima utumie umwagiliaji wa mifereji au boda, na kuna aina ya mazao ambayo sio lazima mfano mahindi na mboga mboga! Mfano katika drip irrigation aina ya zao itakuwezesha kupata ni mipira (drip lines) ngapi utahitaji katika eneo fulani! Hapa nitapawekea somo lake maana kuna mengi yaku cover.

3. Aina ya udongo (Soil type).

Wote tunajua tunapo mwagilia maji katika mashamba yetu maji yanaenda ardhini, basi kwanini hasa niweke sababu hii kama kigezo cha kucheki unapotaka kumwagilia shamba?? Kuna aina nyingi za udongo ila common ni mfinyanzi, kichanga na tifutifu au loam. Kila udongo una sifa yake katika kutunza maji kwa ajili ya mmea. Utunzaji wa maji wa mfinyanzi/clay ni tofauti na mchanga! Mfano clay inavyonza maji haraka na kutunza maji tofauti na mchanga!

4. Mwonekano wa ardhi na hali ya hewa (topography and climate).

Kuna baadhi ya maeneo kuna milima, miinuko na mabonde. Sehemu kama hizi mara nyingi njia inayofaa kutumia ni njia yeyote ya umwagiliaji inayohitaji presha na hasa kama kuna milima na maji niya kupandisha mlimani. Kama eneo liko tambarare umwagiliaji wa mifereji unaweza tumika tofauti na kwenye miinuko! Umwagiliaji wa mifereji kwenye milima unaweza faa kama mifereji itawekwa across the slope na pia angalizo lichukuliwe kuangalia spidi ya maji ili kuzuia mmomonyoko wa ardhi!

5. Mazingira (environment)

Maji yanahitajika katika kila sekta inayomuhusu mwanadamu, japo maji ni uhai ila maji yanaweza hatari zaidi ya bomu kama hayatatumiwa kwa uangalifu yakinifu. Maji ya umwagiliaji yanaweza kuwa chanzo cha magonjwa hasa kichocho (water borne desease), malaria (water related deseases) na hata kuwa maficho ya wanyama hatari. Magonjwa na mmonyoko wa ardhi unachangiwa sana umwagiliaji wa mifereji na kutumia boda system kama za kwenye kilimo cha mpunga. Maji pia yanaweza kuwa chanzo cha uharibifu wa udongo hasa katika miinuko. Ni vyema kabla hujafikiria kutumia umwagiliaji ujue pia ni vyema ukaangalia mazingira yako na jamii pia.

6. Cost/gharama

Kukiweka cha mwisho haimaanishi kwamba hakina umuhimu, na nnaeza sema nimeweka mwisho ili iwe rahisi kukumbuka! Kuna njia nyingi za umwagiliaji, kuna ambazo ni za gharama ndogo mfano umwagiliaji wa mifereji na kuna ambazo ni za gharama kubwa mfano drip irrigation systems, centre pivot na sprinkler irrigation systems. Mifumo hii kwa namna moja au ingine inahitaji gharama kubwa katika kuianzisha na pia muda mwingine katika kuiendesha. Pia inakua logical kama utatumia mifumo ya gharama kubwa katika kilimo chenye faida kubwa mfano kilimo cha high valuable crops nyanya, kabeji na mengine yenye uhitaji mkubwa sokoni!!

Hizo ni baadhi tu, ziko nyingi! nakaribisha mawazo na challenge hasa washika dau katika sekta hii

Link Things to consider before you start to irrigate

Snipper Red Giant sun Shark moniccca iyengamuliro
 
SEHEMU YA KWANZA.

MAMBO YA KUZINGATIA UNAPOTAKA KUANZA KILIMO CHA UMWAGILIAJI!

Habari wana jamvi…

Awali ya yote naomba mnisamehe kwa kuto fulfill my promise kushindwa kuweka somo kila wiki kama nilivyo ahidi, okey leo nlitaka kushare nanyi kitu cha kwanza ambacho mtu anatakiwa kumbuka kama anataka anzisha kilimo cha umwagiliaji. Tumeshaona maana ya kilimo cha umwagiliaji katika pati ya utangulizi, sasa leo nlitaka tujadili mambo machache ambayo ni vyema yazingatiwe pale mtu anapotaka kuanzisha kilimo cha umwagiliaji!

1. Maji na upatikanaji wa maji (availability of water)

Maji katika kilimo cha umwagiliaji ni kama mafuta kwenye gari, kwa lugha ingine kilimo cha umwagiliaji hakiwezi fanikiwa kama hakuna maji tena maji bora nay a kutosha (quality and quantity)! Kuna madhara makubwa sana ambayo yanaweza tokea kama ubora wa maji (quality) ukiwa mbovu, kwa mtazamo wangu haya ndiyo mabaya Zaidi ya yote katika kilimo cha umwagiliaji…embu angalia mashamba kama lower moshi na tpc ambayo kwa kiasi kikubwa yameathiriwa na magadi/chumvi chumvi (salinity)!! Japo tunahitaji maji kwa umwagiliaji ila maji haya yasipo angaliwa yanaweza kuwa bomu baya sana kwa kilimo!! Katika part hii pia ni vyema kujua allocation ya chanzo cha maji, je kipo karibu au mbali na shamba husika!!! Je kipo mlimani au mremkoni??

2. Aina ya zao (crop type).

Tukishajua upatikanaji wa maji,sasa ni vyema tukajifunza kwanini ni vyema kujua aina ya zao kabla yaku set sistimu wa umwagiliji. Mfano kuna mazao ambayo ni lazima utumie umwagiliaji wa mifereji au boda, na kuna aina ya mazao ambayo sio lazima mfano mahindi na mboga mboga! Mfano katika drip irrigation aina ya zao itakuwezesha kupata ni mipira (drip lines) ngapi utahitaji katika eneo fulani! Hapa nitapawekea somo lake maana kuna mengi yaku cover.

3. Aina ya udongo (Soil type).

Wote tunajua tunapo mwagilia maji katika mashamba yetu maji yanaenda ardhini, basi kwanini hasa niweke sababu hii kama kigezo cha kucheki unapotaka kumwagilia shamba?? Kuna aina nyingi za udongo ila common ni mfinyanzi, kichanga na tifutifu au loam. Kila udongo una sifa yake katika kutunza maji kwa ajili ya mmea. Utunzaji wa maji wa mfinyanzi/clay ni tofauti na mchanga! Mfano clay inavyonza maji haraka na kutunza maji tofauti na mchanga!

4. Mwonekano wa ardhi na hali ya hewa (topography and climate).

Kuna baadhi ya maeneo kuna milima, miinuko na mabonde. Sehemu kama hizi mara nyingi njia inayofaa kutumia ni njia yeyote ya umwagiliaji inayohitaji presha na hasa kama kuna milima na maji niya kupandisha mlimani. Kama eneo liko tambarare umwagiliaji wa mifereji unaweza tumika tofauti na kwenye miinuko! Umwagiliaji wa mifereji kwenye milima unaweza faa kama mifereji itawekwa across the slope na pia angalizo lichukuliwe kuangalia spidi ya maji ili kuzuia mmomonyoko wa ardhi!

5. Mazingira (environment)

Maji yanahitajika katika kila sekta inayomuhusu mwanadamu, japo maji ni uhai ila maji yanaweza hatari zaidi ya bomu kama hayatatumiwa kwa uangalifu yakinifu. Maji ya umwagiliaji yanaweza kuwa chanzo cha magonjwa hasa kichocho (water borne desease), malaria (water related deseases) na hata kuwa maficho ya wanyama hatari. Magonjwa na mmonyoko wa ardhi unachangiwa sana umwagiliaji wa mifereji na kutumia boda system kama za kwenye kilimo cha mpunga. Maji pia yanaweza kuwa chanzo cha uharibifu wa udongo hasa katika miinuko. Ni vyema kabla hujafikiria kutumia umwagiliaji ujue pia ni vyema ukaangalia mazingira yako na jamii pia.

6. Cost/gharama

Kukiweka cha mwisho haimaanishi kwamba hakina umuhimu, na nnaeza sema nimeweka mwisho ili iwe rahisi kukumbuka! Kuna njia nyingi za umwagiliaji, kuna ambazo ni za gharama ndogo mfano umwagiliaji wa mifereji na kuna ambazo ni za gharama kubwa mfano drip irrigation systems, centre pivot na sprinkler irrigation systems. Mifumo hii kwa namna moja au ingine inahitaji gharama kubwa katika kuianzisha na pia muda mwingine katika kuiendesha. Pia inakua logical kama utatumia mifumo ya gharama kubwa katika kilimo chenye faida kubwa mfano kilimo cha high valuable crops nyanya, kabeji na mengine yenye uhitaji mkubwa sokoni!!

Hizo ni baadhi tu, ziko nyingi! nakaribisha mawazo na challenge hasa washika dau katika sekta hii

Link Things to consider before you start to irrigate

Snipper Red Giant sun Shark moniccca iyengamuliro
Nashukuru sana mkuu Upepo wa Pesa esa kwa kuendelea kutupatia elimu hii ya kutukomboa kiuchumi kupitia kilimo cha umwagiliaji. Kwa kweli kupitia mada hii mimi binafsi najifunza mengi sana. Mungu akubariki sana. Tunategemea kupata mengi zaidi.
 
Nashukuru sana mkuu Upepo wa Pesa esa kwa kuendelea kutupatia elimu hii ya kutukomboa kiuchumi kupitia kilimo cha umwagiliaji. Kwa kweli kupitia mada hii mimi binafsi najifunza mengi sana. Mungu akubariki sana. Tunategemea kupata mengi zaidi.
Nashukuru sana mkuu Snipper ! Irrigation ni pana sana, ki uhalisia bado tunahitaji mapinduzi makubwa kwenye kilimo hasa cha umwagiliaji! mamlaka ya hali ya hewa walitangaza kutakua na upungufu wa mvua hasa miezi hii!!

Tuendelee kujifunza mkuu mengi sana ya kujifunza, pia kama utakua na pendekezo la mada ambayo utapenda tuiongelee kwenye umwagiliaji nakaribisha maoni yako na kila mtu pia!! Karibu sana mkuu
 
Upepo wa pesa na wadau wengine ninashukuru kwa mada muhimu ukizingatia hali yetu ya kiuchumi Tanzania kwa sasa kilimo ndio biashara ambayo bado inalipa maana watu wataacha anasa zote lakini sio kula. Moja ya changamoto ya watu wengi wanaotamani kuingia kwenye kilimo cha umwagiliagi ni maswali kama 1. Zao gani linalipa zaidi? 2. Eneo gani rafiki kwa kilimo cha umwagiliagi? lets say katika mikoa ya pwaniiliyopakana na bahari. 3.Je nikiwa muajiriwa ninaweza tumia njia gani za usimamizi nifanikiwe katika kilimo? 4. Ni mtaji wa kiasi gani ninaweza anza mradi wa kilimo? Haya mambo ni muhimu kuyafahamu ninaomba tufahamishane wadau sifurahishwi na hali ya watu wengi kuwa ajira ndio sehemu kubwa ya kipato bila kuwa na mpango wa kujitengenezea kipato binafsi kwangu mimi milioni moja ya kujiajiri ina thamani kuliko milioni ya kulipwa mshahara ni basi tuu.
 
Tatzo la watanzania tunaumizana sana...mtu anataka 1.8-2m kwa drip pipes za heka moja while for io hela ukiagiza kutoka china unapata pipes za heka 5....
+86 150 7569 8509 add hio no then anza kuchat na huyo dada watsap mpe requirements zako atakutengenezea design na kukuuzia drip pipes na kukutumia hadi tz unachotakiwa ni kulipia gharama za bandari,wakala na tra utoe mzigo wako...
+8675533556323 hii no ni kwa wale wanaohitaji solar water pump systems kwa wale ambao hawapo karibu na mito...with solar power pump system & drip irrigation u r one point close kua mkulima wa kisasa...Goodluck guys
 
Tatzo la watanzania tunaumizana sana...mtu anataka 1.8-2m kwa drip pipes za heka moja while for io hela ukiagiza kutoka china unapata pipes za heka 5...
Mkuu cha kushangaza kuna baadhi ya watu inaonekana wanaufahamu mzuri lakini hawakawii kusema njoo pm. Ninapenda kilimo na ufugaji lakini sio mtaalamu wa kilimo
 
Back
Top Bottom