Special Thread: Video na picha kutoka Vikosi vya Jeshi la Ukraine walio Frontline dhidi ya Urusi

Hiyo KA-52 inadaiwa ilipigwa picha na Droni tu haikushambuliwa

Sent from my TECNO P704a using JamiiForums mobile app
 
Mhh! Miji kadhaa = sio miji yote..therefore maisha yanaendelea. Usisahau Russia napo miji kadhaa na miundo mbinu muhimu imekuwa magofu e.g. kiwanda cha silaha na vilipukizi, jengo la kibiashara, kituo cha kuongozea ndegevita pale kisiwani, vifaru vingi n.k. Kwa hiyo kulinganisha Hasara sio kipimo sahihi sana.
 
Sasa povu la nini? Tumia akili. Mwezi wa tatu Urusi ilikuwa imeteka mikoa 11 kati ya 26. Sasa hivi Urusi imenyang'anya mikoa yote imebaki mitatu ambayo ndo ina mapambano Luhansk, Kherson na Donbas. Ilikuwa Minne na Kharkiv ambayo Ukraine wameirudisha. Na hii mikoa Mitatu ilobaki Ukraine inashinda. Hakuna wa kuchukuliwa Ubongo, njoo na takwimu. Kama unakereka jinyonge kwa Kamasi
 
Ha-Ha-Ha. Kwa hali hiyo Sasa, inabidi wanachokiona kiwaaminishe - AZOV.
 
Kwani unajua nini kitawapata hao Russia baada ya kutolewa Ukraine? Kupigwa na kuwa magofu siyo ushindi, ukivamiwa tegemea kupigwa kwa aina hiyo maana mabomu yanakuwa yanarushwa kwenye ardhi yako huwezi kuyazuia yote yasitue.

Madhara ya vifo na uharibifu wa mali na majengo hayakwepeki lakini mpaka mwisho ndio utaona ushindi. Vita hubadilika kama upepo. Kumbuka na yeye anafanyiwa hujuma kwenye nchi yake na vita ikiisha atamlipa huyo aliyempiga.

Vita siku 3 kwamba angeshamaliza na kwenda takribani miezi 3 huoni kwamba Russia anapata matokeo ambayo hakuyatarajia?

Kama hapati taabu haw wapinzani wake unadhani wanazuia nini, kwamba wamejificha tu hawapigwi, kwanini anarudi nyuma, anarudi kwa matakwa yake?

Tangia vita imeanza hajapata hasara? Ukraine anaweza kuwa amepata hasara ya majengo na mali lakini Russia kwa silaha alizopoteza, gharama ya kuwahudumia askari wake,wafanyakazi kama madaktar na wafanyakazi wengine, majeruhi wake kuwatibu, vifo vya wanajeshi unaweza kukuta ana hasara kubwa kuliko mwenzake.

Kumbuka Ukraine hayuko mwenyewe wakati Russia yuko peke yake anayeharibu uchumi ni nani kama siyo yeye Russia. Hivyo basi tungoje mpaka Ukraine anyanyue mikono juu au atangaze ushindi, au Russia weseme wameshinda vita.

Huwezi kuwalaumu Westerners wana propaganda za media kwamba wanawapiga Warusi wakati huo huo Russia naye anasema amepata ushindi mkuu juu ya Ukraine wakati pia tunaona hujuma zikifanyika nchini mwake na Ukraine hajatangaza kusalimu amri.

Mfano mzuri angalia vita ya Vietname na US,Vietname walipata hasara kubwa watu kufa, askari na miundombinu lakini je walishinda ile vita? Muda bado upo tungoje hadi mwisho.
 
Nimejaribu kumjibu kwa kumuelewesha hope so hiki ulichokiweka ataelewa zaidi mkuu. Umemjibu kwa ufupi na kueleweka zaidi.
 
Mzigo umefichwa. Halafu Azov sio kwamba waliishiwa Mzigo. Sema wametii amri ya amiri jeshi Mkuu wa Nchi wa kuwaondoa Majeruhi na wao Wasepe.
 
Kifaru cha Urusi aina ya T-72B3 kilikamatwa Kharkiv.
Your browser is not able to display this video.
 
Kikosi cha 59th Motorized Brigade kikisambalatisha Vifaru vya Urusi aina ya T-72B3 na 9K35 Strela-10 SAM system.
Your browser is not able to display this video.
 
Your browser is not able to display this video.
 
Snipers wetu. Busu la kifo
Your browser is not able to display this video.
 
Your browser is not able to display this video.
 
Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…