Special Thread: Video na picha kutoka Vikosi vya Jeshi la Ukraine walio Frontline dhidi ya Urusi

Mrussi ni Fala , mchina mwenyewe alivyopigwa mkwara pale Taiwan akaufyata .
Pumbav
Huyu ndio WA kutunidhiana misuli na mmarekani huyu let alone NaTo Maana NaTo ni giant moja hivi la kutisha Sana .
Tumchukie tumpende Mmarekani ataendelea kuwa kiranja WA ulimwengu Huu ,Mungu ndivyo alivyopanga .
Yani Marekani katoa primitive weapons tena chache kama javelin na Himars na zimemyoosha Mrusi mpaka anaomba po muda si mrefu
 
Logistic mbuvu ndo imevuruga kila kitu kwenye jeshi la Russia
... deployment ya lile limsafara la 64km - vifaru, magari ya deraya, na wapiga vinubi kwenda kuvamia Ukraine ndio hapo utupu wa Putin kichwani ulipoanza kuonekana.

Kwa convoy ya mtindo ule, mabingwa wa logistics walishahesabu 40% ya ushindi imepatikana just by that kind of stupid military deployment.
 
Hahaa asee just imagine mkuu pale ndio ujinga wake ulikuwa wazi.

Halafu nadhani pia askari wazoefu wengi walipotea kwenye ule msafara hawa wa sasa wengi sio wazoefu kwa maoni yangu lakini.
 
Mbona ameshaomba? Mtu mzima tena amiri jeshi mkuu anawaambia wapiganaji wake 'Oyaa? fasta Kimbieni mtakufa hapoo" si amesurrender?
 
Yani nilicheka Sana ,,,walienda vitani Kama vile miaka Ile ya Vita za wafilisti..
... Farao akatuma jeshi lake kuwafuatia wana-Israel; msafara mrefu kweli kweli wenye kila aina ya silaha, na majemedari, na farasi, na wapiga panda, na wacheza vinubi, na wabeba mienge ya moto.

Na ikawa, tazama, Musa akanyosha fimbo yake juu ya bahari maji yakajitenga huko na huko pakavu pakaonekana wana Israel wakapita salama. Jeshi la Farao likaingia; Musa akanyosha tena fimbo yake juu ya bahari maji yakarudi mahali pake. Jesho lote la Farao likateketekea.

Putin alipigana vita vya kale sana aisee! Toafuti ni aina ya vifaa tu; ila approach walitumia approach ya Farao kuivamia Kyiv!
 
Dah! Mkuu umeniamshia mzuka huku. Yani nikizisoma hizo Habari za Farao ambapo mwishoni walipoziona maiti za wamisri na mafarasi yao vikielea ufukweni na kisha wakaimba Zaburi 66:1 (Mpigieni Mungu kelele za shangwe...) na nikilinganisha na matokeo ya Putin naona ni Copy and Paste ya hicho kilichafanyika. Rejea Putin alionywa mno na watu wengi na ikafikia mahali watu wengine wa Imani tofauti-tofauti wakamwomba aache hiyo vita. Lakini alikaza shingo. Matokeo yake Leo shingo hana labda akaze makalio yake.
 
Wapiga Vinubi[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hahaa asee just imagine mkuu pale ndio ujinga wake ulikuwa wazi.

Halafu nadhani pia askari wazoefu wengi walipotea kwenye ule msafara hawa wa sasa wengi sio wazoefu kwa maoni yangu lakini.
"Halafu nadhani pia askari wazoefu wengi walipotea kwenye ule msafara hawa wa sasa wengi sio wazoefu kwa maoni yangu lakini".
Hapana mkuu; Hayo ndo maoni ya wengi sio yako tu. Askari wa sasa hawana uzoefu wa hali halisi ya vita bali wao wanauzoefu wa vita vya kwenye compyuta. Sasa Walipofika kwenye uhalisia(Real war) wakajikuta compyuta haikuwaonesha mfadhaiko vitani, Maumivu, Uchovu, Kutekwa, Hakuna kulala, Silaha tofauti na za kwao,n.k. n.k. Kwa hiyo wakawa totally confused(wakachanganyikiwa) kiasi kwamba Askari wa Urussi anaulizwa namba yake(force number) yeye anataja namba ya cm ya mama yake....
 
Waliingia kwa mbwembwe utadhani msafara wa bwana harusi. Matokeo yake walipukutika na vifaru vyao. Mzee Biden alimsihi Putin asiivamie Ukraine lakini akampuuza tena kwa dharau kubwa.

Sasa hivi hata nchi ndogo kama Latvia au Estonia zinaweza kumkoromea mrusi vimeshamdharau.
 
Hii vita imemdhalilisha sana Putin.
 
Hii vita imemdhalilisha sana Putin.
Akiendelea na kiburi atasababisha wanajeshi wake wengi kuuwawa. Mizoga tunayoshuhudia ilitosha kumfanya ajitafakari upya.

Niliwahi kusema kuwa ni Bora angesingizia kuwa operation aliyopanga imekamilika na akaondoa majeshi yake. angepata aibu kuliko fedheha anayopata sasa hivi.

Siku Crimea ikirudi Ukraine, Georgia nao watataka kuyakomboa majimbo yao waliyonyang'anywa na Putin kwa ubabe. Time will tell.
 
Crimea ni vigumu kurudi Ukraine
 
Putin ameanzisha mchakato wa kujimaliza machoni pa mataifa bila kujua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…