Special Thread: Video na picha kutoka Vikosi vya Jeshi la Ukraine walio Frontline dhidi ya Urusi

Hongera sana Ukraine. Kaza mwendo, ule mwisho ambao sote tunautarajia kwa matumaini makubwa umekaribia sana.
 
Siku zote mshahara wa dhambi ni mauti. Usimwonee mtu, au kumdhulumu haki yake kwa sababu tu ya hali yake. Mungu anaweza kukugeuzia kibao ili na wewe uionje hali mbaya ili ujifunze. Mrussi alimvamia Ukraine kwa kumwonea eti kwa sababu tu Ukraine ni mdhaifu kijeshi ukilinganisha na maguvu ya Mrussi(Ubabe)- sasa ona hapo Mrussi anaikumbatia na kuilamba barabara utadhani anaipiga lami upya kwa ulimi wake.
 
Putin amelisababishia Taifa la Urussi FEDHEHA kubwa duniani. Bendera ya Taifa lolote kunyofolewa hivyo na kutupwa chini kana kwamba ni sawa na dekio; Ni Aibu. Ina maanisha Taifa la Urussi limekuwa sawa na matambara yasiyohitajika tena kuusitiri mwili. Hilo Taifa Putin analoliongoza Halifai tena. - Ni takataka.
 
Mwezi uloisha Frontline ya Ukraine imesonga mbele kiasi chake. Pamoja na Urusi kusema ina jeshi kubwa, tumewarusisha nyuma sana
View attachment 2374583
Mrussi kwa sasa amebakiza kazi anayoimudu walau kidogo nayo ni ya kurudi nyuma tu sio kusonga mbele. Kusonga mbele kwa Mrussi imeshakuwa ni marufuku na Asipoweza kurudi nyuma anageuzwa mbolea chap na labda akibahatika anaweza kuwa mateka ila sio mikononi mwa AZOV.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…