Special Thread: Video na picha kutoka Vikosi vya Jeshi la Ukraine walio Frontline dhidi ya Urusi

Natamani kuona wanalenga vituo vya kijeshi sio makazi ya wananchi. Jeshi kwa jeshi. Lakini hii ya kuzidiwa unaenda kuua raia kama kulipiza kisasi ni aibu kwa Urusi
Hawana huo uwezo na wanajua GUR HQ, SBU HQ zinalindwa ndo maana hawajajisumbua.
Wamepiga hadi mgodi afu wanasema walitumia High Precision Missiles

Kingine ni kuwa missiles zao zilipenya kwa 51%
 
Rockets lengo ni kulenga critical infrastructure sio watu
Kwanini hamjalenga panapotolewa maamuzi?
Mlisema SBU ndo wamehusika, maana yake Crimea iko infiltrated, kwanini msingelenga majengo ya SBU?
 
AZOV walishalibaini hilo la kutofuata kanuni na ndo maana hawachukui mateka. AZOV akikamata askari wa Mrussi kazi ni moja tu- kuwaua.
 
We umezaliwa 2005 itakuwa. Hujashuhudua vita ya USA. USA anashusha makombora katikati ya Mji na mara nyingi usiku.
 
Kwanini hamjalenga panapotolewa maamuzi?
Mlisema SBU ndo wamehusika, maana yake Crimea iko infiltrated, kwanini msingelenga majengo ya SBU?
Mkuu; Maamuzi hutolewa na watu kutoka vichwani mwao. Majengo ni fixed. Watoa maamuzi ni mobile -wanaweza kuhamia majengo mengine au hata wakaenda kukaa chini ya mti na wakaendelea kutoa maamuzi. Kinachozungumzwa hapa ni majengo yenye maslahi ya kivita i.e. Miundombinu ambayo ikiondolewa/ikiharibiwa majeshi ya adui yatatatizika au yatashindwa kutekeleza na kufikia malengo yake. e.g. daraja likibomolewa adui hawezi kusafirisha silaha au kupitisha support kupitia hapo darajani labda azunguke mbali. Maghala ya silaha ya adui yakiharibiwa silaha zitateketea na hakuna mahali tena pa kuhifadhia silaha labda kujengwe maghala mapya n.k. n.k.
Je; huko Kyiv alikopiga au majengo ya watoto n.k. kijeshi yana umuhimu gani kwake kivita ?
 
Kwanini hamjalenga panapotolewa maamuzi?
Mlisema SBU ndo wamehusika, maana yake Crimea iko infiltrated, kwanini msingelenga majengo ya SBU?
Makao makuu ya azov imepigwa na makombora
 
We umezaliwa 2005 itakuwa. Hujashuhudua vita ya USA. USA anashusha makombora katikati ya Mji na mara nyingi usiku.
.........USA anashusha makombora katikati ya Mji na mara nyingi usiku.
Wapi hiyo ? OK. Kwa lengo gani? Chunguza vizuri
 
.........USA anashusha makombora katikati ya Mji na mara nyingi usiku.
Wapi hiyo ? OK. Kwa lengo gani? Chunguza vizuri
Nichunguze nn, ndio nakwambia anaharibu tu, hata Libya huko, Iraq ndio usiseme alishusha makombora zaidi ya 500 jijini Baghadad tena usiku. Tafuta video yake uone. Unaongea kishabiki na kijinga sana.

Kisa huipendi Urusi basi unadanganya hapa?? Acha hizo mambo, ndio maana mnatolewa akili. Afghanistan ilishambuliwa mpaka mjini na ikaharibiwa vibaya sana.
 
Hawana huo uwezo na wanajua GUR HQ, SBU HQ zinalindwa ndo maana hawajajisumbua.
Wamepiga hadi mgodi afu wanasema walitumia High Precision Missiles

Kingine ni kuwa missiles zao zilipenya kwa 51%
😳
 
We umezaliwa 2005 itakuwa. Hujashuhudua vita ya USA. USA anashusha makombora katikati ya Mji na mara nyingi usiku.
Sawa, Libya alikuwa anamtarget Ghadafi alimkosakosa akaua mtoto wa kambo,Baghdad?
 
Hapana mkuu. Urussi sio adui kwangu hata siku moja.-naipenda Urussi ILA NAKICHUKIA SANA NA SIUNGI MKONO KABISA KITENDO ALICHOKIFANYA CHA UVAMIZI UKRAINE.
Bila kuhamisha magoli, huko kote ulikotaja utakuta wanajeshi/wapiganaji wanajificha katika makazi ya raia na raia hao hao wanashiriki kwa namna fulani katika mapigano. Huko kote ulikotaja majengo husika yalikuwa yanatumika kuhifadhi silaha au ni RVs (mahali pa kujikusanya baada ya tukio la hujuma) kwa ajili ya wapiganaji. Huko kote ulikotaja uwepo wa jengo fulani mahali unakuwa ni kizuizi (Obstacle)kwa mtoa kipigo kwa adui. Kwa hiyo jengo linaondolewa kupisha utekelezaji wa kutoa kipigo.
Mashambulizi katika maeneo ya watu au yenye mikusanyiko ya watu wengi yaliyofanywa usiku ili kupunguza idadi ya vifo vya raia wasio na hatia.
Yapo maeneo ambayo hupigwa bila kujali kanuni kwa sababu - si askari , si raia pamoja na majengo yaliyopo vyote kwa pamoja vinakuwa ni kundi la ki-Adui i.e. huwezi kutofautisha askari na raia au majengo yenye silaha au wanapojificha askari.(Ni mseto au mixture).
 
Kwahito kisa marekali aliipiga iraq basi ndo tumuache na mrusi aipige Ukraine..??......halafu bora ata mmarekani anapiga na kuondoka mrusi ana watawala hilo halitowezekana
 
Marekani yeye alitaka kuiba wese tu Iraq lakini Urusi anaiba ardhi nzima hadi kinu cha Nyukilia anakitwaa kibabe
Sio hivyo tu, ikafikia mahali akabweteka na tar.24 Feb 2022 akajiamulia aongeze mipaka na akataka afike hadi Kyiv kwa madai eti kumwondoa Zele madarakani cjui sio msikivu, hataki kumsikiliza, blaa blaa nyingi n.k.n.k. alitaka atawale yy au vp. Huko Bucha usiseme alipageuza kuwa buchani kweli kweli. Mrussi gani huyo kama sio kirusi(Virus) kwa Taifa la Ukraine?? Wacha apewe chanjo ya nguvu sio ya hiari tena..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…