Special Thread: Video na picha kutoka Vikosi vya Jeshi la Ukraine walio Frontline dhidi ya Urusi

Special Thread: Video na picha kutoka Vikosi vya Jeshi la Ukraine walio Frontline dhidi ya Urusi

Hapa ni Makiivka, Mkoani Luhansk. Urusi wamekamatwa kama kuku wa kisasa. Hawakujua wamezungukwa, Wakamrushia risasi Mwanajeshi wa Ukriane.. Wamepelekewa moto hadi wakaweka mikono juu. Ambao walijifanya kujificha ndani, wakitafutwa kwa risasi. Ila hawa waliokufa walitaka wenyeww, wenzako wamejisalimisha, kwanini urushe risasi? Angesababisha wote wauawe. Alidharau alikua askari wa Ukraine yupo peke yake kumbe wengine wamejificha. Watakuwa wamemlaumu sana. Amesababisha watu wapigwe risasi wakati walikuwa wamejisalimisha
 
Mnakumbuka yule naibu Mkuu wa Mkoa wa Kherson waliodai kapata ajali akafa? Imegundulika Urusi walimuua baada ya kumtumia kisha Wakaretreat. Huyu alikuwa raia wa Ukriane, Urusi walipovamia akasaliti na kujiunga Urusi. Wakampa umakamo wa Mkuu wa Mkoa. Mkuu wa Mkoa alitoka Urusi, huyu wa Ukraine alikuwa msaidizi. Urusi walipotaka kuretreat wakasema kapata ajali ambapo gari liliondolewa haraka.

Imebainika baada ya Urusi kumtumia wakamuua ili asitoe siri then Wakaretreat.

Hili ni gari la Stremusov walidai kagongana na lori kumbe gari lilipigwa ambush ya risasi
View attachment 2419678View attachment 2419679
Malipo yake ya usaliti
 
Huyu alitoka nje ameshikilia mtutu, maana yake yupo tayari kwa mapambano. Ukraine hawakumlazia damu
20221118_121920.png
 
Hapa ni Makiivka, Mkoani Luhansk. Urusi wamekamatwa kama kuku wa kisasa. Hawakujua wamezungukwa, Wakamrushia risasi Mwanajeshi wa Ukriane.. Wamepelekewa moto hadi wakaweka mikono juu. Ambao walijifanya kujificha ndani, wakitafutwa kwa risasi. Ila hawa waliokufa walitaka wenyeww, wenzako wamejisalimisha, kwanini urushe risasi? Angesababisha wote wauawe. Alidharau alikua askari wa Ukraine yupo peke yake kumbe wengine wamejificha. Watakuwa wamemlaumu sana. Amesababisha watu wapigwe risasi wakati walikuwa wamejisalimisha
View attachment 2420122

Wanavyotembea wananyata kwa upole kama wanaelekea Altar kupata mkate wa uzima. 😂😂😂😂😂
 
Huyu ndo amesababisha wenzake wauawe. Wanadai Ukraine imeia mateka. Huyu jamaa alimpiga risasi mwanajeshi wa Ukraine aliyekuwa anawamulu walale chini. Hajafa yupo Hospitali, kitendo hicho kimefanya Ukriane wajibu.. Matokeo yake ni vifo kwa Urusi. Wenzake 10 walikuwa wameshalala chini. Yeye na wenzake wanajifanya Makomandoo. Wamekufa
 
Nimesoma utetezi wa Kremlin kuwa wanapiga makombora kwenye miundombinu ya umeme na makazi ya watu eti kwa sababu wanaishinikiza Ukraine ikubali mazungumzo "Negotiations". Maana yake ni hasira za kukataliwa kuzungumza na Ukraine.

Wanasema kwa kuwa uongozi wa Ukraine umekataa mazungumzo na Russia basi wanapiga miundombinu ya umeme na maeneo ya makazi ili wananchi wa Ukraine waishinikize (pressurize) serikali yao wakubali kuzungumza na Russia.

This is nonsense, and old war tactical strategy. mbinu hii ni dhaifu kwa sababu zifuatazo;
1. Russia imechelewa sana (wrong timing), hili lingewezekana kipindi kile Ukraine haijapewa air defense systems za kulinda anga lake. Ukifuatilia utaona makombora mengi yanayotunguliwa na kudondoka ndo yanayoleta athari ndogo kwenye maeneo yanapodondokea. Pia makombora ya Ukrainè yanaposhindwa ku intercept yanaenda kupiga maeneo ya wananchi wake ila hawawezi kusema hilo. Ukraine wanatumia opportunity hiyo kupiga kelele na kuongeza chumvi ili waendelee kupata sympathy kwa mataifa yanayowasaidia.

2. Kwenye battlefield Russia kazidiwa ndo maana kila siku inarudishwa nyuma hata kama ni kwa mita 100. Màana yake yuko zaidi kwenye kujilinda (defensive) ña mbinu anatumia ni ya kujilinda kuliko kufanya mashambulizi kwenye mstari wa mbele.

3. Kitendo cha Russia kupigapiga hovyo nje ya uwanja wa vita na kuleta athari kwa Raia wasio na hatia, anazidi kutengezeza hasira na kupandikiza chuki kwa Raia wa Ukraine, hivyo hawawezi kulalamika au kushinikiza serikali isiwatetee kumwondoa mvamizi. Hii ni akili ya jogoo kumpanda mama yake.

4. Kitendo cha Russia kupiga makombora yake ovyo, anaisaidia Ukraine kupata justification ya kupewa air defense system zilizo imara na silaha nzito za kujilinda na kupambana na adui. Hivyo hataweza kamwe kulazimisha Ukraine ikubali negotiations.

5. Anajiongezea gharama za bure za kuifidia Ukraine, maana hilo hatalikwepa Russia.

Yote tisa, ni aibu kwa anayejiita super power kubembeleza mazungumzo yafanyike wakati yeye alitakiwa aikamate nchi yote ya Ukraine ndani ya masaa 72.

Hii ni dalili kubwa sana ya kushindwa vita.
 
Back
Top Bottom