Bila hatua madhubuti kuchukuliwa Bakhmut na miji mingine itachukuliwa na Wagner muda si mrefu.
1. Kukosekana kwa tanks, Artillerys, vehicles na risasi za kutosha direction ya Bakhmut kutafanya muda si mrefu Bakhmut na miji mingine kuchukuliwa na Wagner/Russia. Ni ukweli kwamba Wagner wameharibu tanks na Artillery za kutosha eneo la Bakhmut, Soledar na salt mine. Hali siyo nzuri kwa Ukraine kuhusu vifaa.
2. Kucheleweshwa kwa tanks, Artillery, Vehicles na risasi kumeshusha morali ya wanajeshi wa Ukraine direction ya Bakhmut. Moral ya wapiganaji ikishuka usitegemee kupata ushindi. Askari wanataka tanks za kisasa wampige adui.
3. Frontline ya Ukraine direction ya Bakhmut imezidiwa sababu ya uchache wa tanks, artillery, MLRS na risasi.
4. Russia wamepata moral ya ajabu direction ya Bakhmut na Vuhledar. Hawajali wanauliwa kwa kiasi gani, wanapambana kufa na kupona. Hii siyo dalili njema kwa Ukraine na washirika wake.
5. Kama waliyosema USA na Germany ni kweli kuwa Abrams, Leopard 2 na F-16 zinaweza kufika June, sababu ni complex tanks na fight jet, kwamba kufundisha wanajeshi wa ukraine kunahitaji muda. Kwa hali hiyo huenda miji ya Slovyansk, Kramantorsk, Pavlohrad, Dnipro, Nikopol na Zaporizhzhia zitakuwa mkononi mwa Russia mpaka huo mzigo unafika.
6. Ukraine inahitaji powerful air defense system ili kuzuia Hypersonic missile ambazo Russia ameanza kurusha. Patriot na SAMP/T zinahitajika haraka Ukraine. Kichaa cha Putin kimeshapanda maana anayateketeza majengo na miundo mbinu yote iliyoko mbele yake. Ni jini linalotaka damu ya wa Ukraine.
7. Kama NATO hawatapeleka hizo tanks na wataalam wa ku operate F-16, Abrams na Leopard 2 mapema na kusubiri mpaka wanajeshi wa Ukraine watoke mafunzo hiyo June basi hali inaweza ikawa mbaya kwa Ukraine. Indirect Intervention ya NATO inahitajika kummaliza nguvu Russia.