Special Thread: Video na picha kutoka Vikosi vya Jeshi la Ukraine walio Frontline dhidi ya Urusi

Huyu dada alikuwa ni Nesi wa Azovstal kule Mariupol akitumia jina la kijeshi Kateryna “Ptashka”, kwa sasa yupo Ujerumani, hapa akiimba wimbo wa Azov huku amekaria kifaru cha Urusi kilicho haribiwa na Majeshi ya Ukriane. Hapa ni Walipoandamana kwenye Ubalozi wa Urusi huko Berlin Ujerumani
Your browser is not able to display this video.
 
Hii ni kazi ya AZOV. Urusi wamwshondwa kusonga mbele huko Bakhmut. Matokeo yake wanazungukwa. Kama Wasiporetreat watatekwa wao. Kibao kimegeuka. Hii ni kazi ya 17th Armored Brigade na 3rd Assault Brigade (Ex #Azov) ambao wanawapiga Urusi kutokea kaskazini na kusini Wakutane katikati. Hawa Wagners kazi wanayo mbele ya Azov
 
Kama ngoma imegeuka basi hii ni good news.
 
Ndege ya Urusi Beriev A-50, yenye radar systems imelipuliwa huko Belarus. Ni ndege ya gharama yenye uwezo wa kutrack hadi km 400. Kazi imefanywa na vijana wawili kwa kutumia drones zilizojipenyeza hadi kwenye uwanja wa ndege wa Machulishchy airbase Mkoani Minsk huko Belarus. Na special operation yao waliita "Victory Plan". Tayari vijana hao wameshavuka na Ukraine na wapo sehemu salama. Inakadiliwa gharama yake ni Euro Milioni 330. Wamelipa kisasi kwani Urusi pia ililipua Antonov An-225 Mriya ya Ukraine
 
Ila kwa jana Wagner wame dig zaidi kuingia katikati ya Bakhmut. Sehemu ya makutano ya mtaa wa Shchedra na Rostovska uko under their control. Kwa lugha nyingine mtaa wote wa Rostovska uko chini ya Wagner.

Bado nasema Ukraine ina kazi kubwa ya kufanya kuwatoa Wagner katikati ya Mji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…