Special thread: Wapenda vinywaji visivyo na kilevi (non alcoholic) na changamoto wanazokutana nazo wakikaa na walevi

Mimi sinywi kinywaji chenye kilevi ila kampani yangu kubwa wanapiga masanga, ila sikutani na hizo changamoto wanaheshimu kile nafanya akiwa mgeni kwangu atanishangaa sababu ya muonekano wangu, ni mjanja mjanja hawez amini kama situmii pombe ila maswahiba zangu wanaelewa na nikikosekana katika mitoko yetu huwa wanalalamika hapanogi kabisa.
 
Kuna siku nilikaa na walevi, wao wakaagiza vyao mi nikaagiza maji makubwa, nilishambuliwa sana, mmoja wao aliniuliza "hivi unafuga samaki, mbona unaagiza maji lita nzima?"
Kiboko yao inabidi uwe na maneno ya kifedhuli tuu
 
Donatila nakuja inbox tuyajenge, kucheza ni zoezi zuri sana
 
Hivi jaman kuna wine isiyo na kilev?? Wine sio shampeni
 
Mmh
Sitaki kuamini mie
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…