Special thread: Wapenda vinywaji visivyo na kilevi (non alcoholic) na changamoto wanazokutana nazo wakikaa na walevi

Special thread: Wapenda vinywaji visivyo na kilevi (non alcoholic) na changamoto wanazokutana nazo wakikaa na walevi

Mimi sinywi kinywaji chenye kilevi ila kampani yangu kubwa wanapiga masanga, ila sikutani na hizo changamoto wanaheshimu kile nafanya akiwa mgeni kwangu atanishangaa sababu ya muonekano wangu, ni mjanja mjanja hawez amini kama situmii pombe ila maswahiba zangu wanaelewa na nikikosekana katika mitoko yetu huwa wanalalamika hapanogi kabisa.
 
Kuna siku nilikaa na walevi, wao wakaagiza vyao mi nikaagiza maji makubwa, nilishambuliwa sana, mmoja wao aliniuliza "hivi unafuga samaki, mbona unaagiza maji lita nzima?"
Kiboko yao inabidi uwe na maneno ya kifedhuli tuu
 
Habari wadau,

Mimi ni si mnywaji wa vinywaji vyenye kilevi ni mnywaji wa vinywaji visivyo na kilevi kama juice, soda, bavaria, nk. Najua wapo wenzangu ambao nao ni wapenzi wa vinywaji hivyo.

Nikiwa kama mnywaji wa vinywaji visivyo na vilevi hua nakutana na changamoto sana wakati nikitoka na marafiki, wengine hunilazimisha ninywe, wengine hunicheka.

Mara waseme nawajazia nzi kwenye meza zao, mara sasa utaweza kukaa kweli mpaka usiku, utaboereka, onja basi kidogo.

Ajabu ni kuwa napenda sana kucheza muziki, muonekano wangu mimi ni mcheshi,yani ukiniona nacheza utasema huyu kanywa, sioni aibu.

Haya twende kwenye hoja;

Ni kero gani ambayo unakutana nayo wewe usiyekunywa.
Na ni kwa namna gani unaondokana nayo.

Karibuni
Donatila nakuja inbox tuyajenge, kucheza ni zoezi zuri sana
 
Hivi jaman kuna wine isiyo na kilev?? Wine sio shampeni
 
Mimi sinywi kinywaji chenye kilevi ila kampani yangu kubwa wanapiga masanga, ila sikutani na hizo changamoto wanaheshimu kile nafanya akiwa mgeni kwangu atanishangaa sababu ya muonekano wangu, ni mjanja mjanja hawez amini kama situmii pombe ila maswahiba zangu wanaelewa na nikikosekana katika mitoko yetu huwa wanalalamika hapanogi kabisa.
Mmh
Sitaki kuamini mie
 
Back
Top Bottom