LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Ha haaa mnachekesha washabiki wa urusi , kwamba hao ameokota Tu kitaa , so they are poor and inexperienced , katika jeshi ambalo linatuaminisha lipo imara kuliko US? ... Si walituambia ni full scale military invasion au walikuwa wanatania ?? Anyway kama wanabip Acha wenzao wawapigie
 
Kwayo watu wabad kama kina UK na kina USA wake kushototu.
 
Zote ni program za freemason. Lengo la covid ilikuwa ni kuongeza idadi ya watu kuzimu. Kuna idadi waliyoitaka imetimia.
Lengo la kutengeneza ukimwi kuzimu Ili kuwapeleka kuzimu vijana wengi sana yaani wengi wafe haraka wangali vijana kabla ya kufikia umri wa utu uzima.
 
Urusi inasemwa kuwa nchi yenye uwezo wa kupiga nchi zote za nato at the same time.
sasa kinachoendelea pale Ukraine tumeanza ku- question uwezo huo unahubiriwa kwenye social media
Russia kabakiza Kiev tu ili awe ameteka nchi kitu ambacho kitazua kelele ndio maana Putin aliagiza jeshi lisichukie Kiev kwanza ili kutoa nafasi ya mazungumzo na Ukraine ambapo imeshindikana,now katoa go ahead so subiri kisha utaona kama atafanikiwa au lah.Pili lazima ujue kuwa hata Ukraine wanapigana kama ambacho kila nchi ingepigana lkn wataangushwa tu pamoja na support yote wanayopewa.Na mwisho Russia anajaribu kuichukua Kiev bila mauaji mengi ya raia ya kawaida ambapo akiona kuna ugumu wa kukwepa hayo mauaji basi anaweza kuamua kufyeka wote.
 
Porojo za wafia dini. Biblia tu ametuambia kuwa kuelekea siku za mwisho yatazuka na maradhi yasiyotibika lkn wewe bado tu huamini na badala yake eti unaamini propaganda. Poor you.
 
Russia na kiwebsite chao cha RT.com ukisoma habari kwao mara mbili ukirudi mara ya tatu wananza kukuambia"We have registered suspicious traffic coming from your network. Using this page, we will be able to determine that you are not the robot. Wakti maBBC, Maaljazeera huko hawana hizi mambo kweli. Kwa kifupi mrusi alidhani myukreni mlaini kama pamba sasa kakutana na upinzani ambao hakuutarajia zile siku za mwanzo Putin alikuwa anabweka hatarii sasa hivi kidogo kafunga mdomo wake,
 
Urusi inasemwa kuwa nchi yenye uwezo wa kupiga nchi zote za nato at the same time.
sasa kinachoendelea pale Ukraine tumeanza ku- question uwezo huo unahubiriwa kwenye social media
Hivi nyie mnavuta bange za wapi....?

Marekani and the allies walitumia miezi mingapi Libya.? Ka nchi ka Africa... na Iraq je.??? Haya kimewakuta nini Syria.??

Na hapo haendagi pekeyake lazima aweke neno the allies..

Nyie subirini kichapo..
 
Ila pro USA mnashangaza sana na mna unonko sana yaani vita ndo kwanza ina siku tatu ila mmesha muhukumu putin kwamba kashidwa?

Urusi ina haki ya kufanya chochote pale inapoona usalama wake una tishiwa kama marekani alivyo ivamia Iraq, Afghanistan na kuuwa mamilioni ya raia.

Kama Israel anavyo uwa wapalestina bila huruma kwa kisingizio cha kujinda.

Kwenye vita ni lazima ulipie gharama hizo ulizo zitaja na Putin analijua kabisa ya kwamba hajaenda vitani kwenda kucheza ngoma bali kaenda vitani kupambana na watu wenye mafunzo kama walivyo wanajeshi wake.

Kwenye vita ni lazima upoteze wapiganaji, vifaa,na pesa hata uwe una nguvu kiasi gani ,hata kama unaye pambana naye ni dhaifu kiasi gani.

Marekani aliivamia Iraq mpaka ana iteka Baghdad alikuwa amesha poteza maelfu ya wapiganaji na vifaa vingi vya kijeshi na amepoteza matrion ya $ lakini hakujali hilo alicho jali ni kile kilicho sababisha anavamia.

Alafu kingine ukijaribu kuangalia kiuhalisia bila ushabiki utagundua ya kwamba Urusi hatumii nguvu kubwa sana kwenye hivi vita bali anatumia nguvu za wastani hata mashambilizi ya anga sio makali sana, nadhani ana hofia mauaji ya raia yatakuwa makubwa.

Gharama ambayo angeilipa Urusi baada ya NATO kiweka base zake Ukraine ni zaidi ya mia ya atakaye zilipa kwenye vita na Ukraine.
Hata ungekuwa ww mkuu ungefanya alicho kifanya Putin.
 


Hatimaye uzi wa Hilda Newton umehamia Ukraine na Russia
Mungu ibariki Tanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…