LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
hapa mim ndio huwa nashangaa sana
kama taarifa za jana ni kuwa bweni la wanafunz wa kutoka India waukrain wamelichoma moto na kujeruhi.
 
ni chanel ipi mkuu niweze kuchek
mim sipend kushikwaga maskio ndio mana nachek RT chanel kujua ukwel
 
Hatutaki jimbo lolote.mpaka sasa tuna vinu 2 vya kuzalisha umeme,bado vi 3 tu tuanze kuwauzia umeme wa ukraine
Wee mwehu kweli leo asubuhi kinu cha mlichoteka juzi kimerudi kwa wenyewe Jeshi la Ukrainlimekikomboa au bado uko usingizini nini mzee amka stuka Putin anakupeleka chaka kweli kweli
 
Anaefuata kufa ni Baba yenu Putin,tena huyu atakufa kifo kibaya sana cha kudharirika,kama siyo mimi basi watoto wangu watashuhudia Mungu akimwadhibu huyu shetani mkubwa cousin wa Rucifer
amemkosea nini Mungu labda, na kipi amekifanya ambacho marekeni na washirika wake hawajakifanya.
 
Hahaha unanichekesha sana Nyamizi yaani Urusi jeshi lake linaasi? Jana tu wamegawa chakula huko Ukraine na pili raia wote huko Ukraine wanamwagiwa hela na wanafurahi sana. Inaonekana haujui kinachoendelea Ukraine nenda hata BBC ukapate taarifa maana wao wameposti PUTIN'S CRUELTY IN UKRAINE PEOPLE IS DANGEROUS. Kawa wao wanaona hatari ya Putin huko Ukraine sasa nyie akina nani?
 
Wew mwenyewe

Wew mwenyewe una ushabiki umesema ule alofanya Putin s uvamiz na uko serious kabisa umeleta na story za marekan kuwa nae anavamiaga kwahiyo nawew umerud kwenye ushabik wa simba na yanga
Uyu ni mwehu kabosa akili zake zimekuwa cracked sijui anaongelea Urusi gani iyo kama ni hii ambayo ndani ya siku kumi za vita imeshindwa kuuteka ata mji mmoja mkubwa ndani ya nchi ya Ukrain alafu uniambie kuwa eti ina jeshi imara labda waongopee wenzio nimesoma hili gazeti lako nikaishia katikati maana ni ujinga tu umeandika braza
 
Wee mwehu kweli leo asubuhi kinu cha mlichoteka juzi kimerudi kwa wenyewe Jeshi la Ukrainlimekikomboa au bado uko usingizini nini mzee amka stuka Putin anakupeleka chaka kweli kweli
Atajulia wapi wakati akiamka tu anakimbilia kwenye page za Pro Russia anasoma huku kisha anakuja hapa kutuletea "breaking news" zake zilizopitwa na wakati
 
Raisi Volodymr Zelensky ameikosoa NATO baada ya kukataa ombi lake la kushinikiza kuwekwa kwa "no fly zone" huku uongozi wa NATO ukiweka wazi maamuzi hayo yatachochea yatachochea mlipuko wa Vita ya Nuclear na Urusi.
Raisi Zelensky amezungumza akisema,
"Leo kulikuwa na kikao Cha NATO kikao dhaifu kikao kilichochanganyikiwa, kikao ambacho kimeweka wazi siyo kila mmoja anachukulia Vita Kama uhuru wa Bara la ulaya Ni lengo namba moja.

Tunaamini kwamba nchi washirika wa NATO wamejitengenezea dhana ya kwamba kulifunga anga la UKRAINE kutachochea uhasama/uchokozi(direct aggression) wa moja kwa moja na Urusi, mawazo ambayo ni dhaifu na kukosa kujiamini japokuwa wanaweza wakawa wanamiliki siraha imara(nzito) kuliko zetu.
Hayo yamesemwa na Raisi wa Ukraine baada ya kukasirishwa na kitendo Cha Nato kutupilia mbali maombi yake.



 
Hicho chakula wanachokigawa si ndicho kile kilicho expire 😂,nachojua wao wana njaa sana wapelekee wali na mandondo ya nazi wakale washibe wapate nguvu ya kushusha makombora kwenye majengo na makazi ya watu. Anyway ngoja niende kwa BBC nikajisomee na nitakuja kukujibu tena hapa.
 
Watu wote wanaokufa wanakufa kwasababu yenu'
Akiripotiwa kuzungumza kutoka katika ofisi yake katika mji mkuu Kyiv rais wa Ukraine Zelensky amelaani kutendo cha viongozi wa Nato cha ' kukataa Ijumaa kuanzisha eneo la anga ambalo ndege hazipai -no-fly-zone juu ya nchi yake.

Zelensky alisema: "Watu wote wanaokufa wanakufa kwasababu yenu, kuanzia leo, watakufa kwasababu yenu. Kwasababu ya udhaifu wenu, kwasababu ya kutoungana."

Aliendelea kusema kuwa: " Mkutano wa Nato ulifanyika leo. Mkutano dhaifu. Mkutano uliokanganyikiwa. Mkutano unaoonyesha kwamba sio kila mtu anayechukulia mapambano kwa ajili ya uhusu kwa Ulaya kuwa lengo namba moja.

"Mashirika yote ya ujasusi yan chi za Nato yanafahamu fika kuhusu mipango ya adui. Walithibitisha kuwa Urusi inataka kuendeleza mashambulizi.

"Kwa makusudi Nato iliamua kutofunga anga juu ya Ukraine. Nchi za Nato zimebuni fikra kwamba kufunga anga za juu ya Ukraine kutakuwqa ni uchokozi wa moja kwa moja dhidi wa Urusi dhidi ya Nato.

“Haya ni mawazo ya kipekee ya wale ambao ni dhaifu, wasio jiamini, licha ya ukweli kwamba wanamiliki silaha silaha ngingi zaidi ya zile tulizo nazo."

Zelensky baadaye aliuhutubia umati mkubwa wa waandamanaji wanaoendelea kuandamana katika mataifa ya Ulaya, akiwaambia waandamanaji : " Iwapo Ukraine haitanusurika, Ulaya yote haitanusurika.

"Kama Ukraine itaanguka, badi Ulaya nzima itaanguka."
Source:BBC
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…