LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Sasa mbona miji hawaikomboi Kama mrusi kakimbia kaacha mitambo

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app

Kwa sasa Mrusi ndiye yupo kwenye offensive, maana kwamba yeye ndiye anashambulia, Ukraine wao wanaendelea kupambana kuhimili mashambulizi yake.

Kihistoria Urusi wakifanya mashambulizi wao hupigana kizalendo na wapo radhi hata kufa mamilioni lakini wafanikishe lengo, ndicho walikifanya kwenye vita vya pili vya dunia, waliuawa mamilioni lakini walisonga mbele kwa mbele mpaka wakaingia Berlin kwa Hittler.
Lakini kwanza huwa mwanzo uwaaminishe kwanini wapigane, kwanini wajitolee kufa, uwachochee na kuwapa mzuka, ila kwenye huu ugomvi Putin kawakanganya kwa kukurupuka, amewatumbukiza kwenye ugomvi ambao hawauhitaji na hawautaki, ukiingia kwenye mitandao ya kijamii kama Quora utaona namna gani Warusi wanapinga hivi vita.

Pia kwao kule wanakamatwa wengi wanaothubutu kufanya maandamano ya kupinga hivi vita vya Putin.
 

WW2 Urusi alikuwa kama Ukraine kwa maana kupambana na kumlinda mvamizi... Germany alikuwa mchokozi kwa kuanza kuivamia Russia..
 
Mrusi kaamua kuutokomeza ubabe wa Kimagharibi. Alichofanya Putin binafsi naona yupo sawa, kwani Magaharibi, hususan USA, wanajifanya wao ndio polisi na wababe wa dunia na wanachotaka wao lazima kiwe. Imefikia mahala, wanakuwa kama wapo Hollywood wanacheza filamu, wanawaonea mataifa madogo, lakini hata hayo mataifa mengine madogo yanawahenyesha sana lakini hawajifunzi wakatia adabu.

USA hawana ujanja wala ari ya kupigana wao wenyewe, wanawasukumizia wengine mizozo yao. Sasa hivi wamemuingiza mkenge Ukraine. Ghuba huko wamemuingiza Mkenge Saudi Arabia na nchi zingine za Kiarabu kuwa ndio "frontline" yao kwa Wa Iran na nchi zingine huko zenye watawala wasikubaliana nao.

Vietnam, waliwahenyesha, Taliban wamewahenyesha mpaka sasa hivi wanaugulia majeraha. Somalia ndio hawana hamu kabisa, wameifanya Kenya kuwa ndio frontline yao, ni heri Tanzania walistuka mapema.

Ukraine haitabaki salama mpaka isalimu amri, Na USA hataki hii vita iishe haraka kwaani ikiisha, front line yao waliokuwa wanaiunda ndio itakuwa imeshasambaratishwa na Warusi wanakuwa karibu zaidi na nchi za NATO, itazimeza moja moja, sio kwa kuzivamia bali kwa zenyewe kutii amri yao wataponyanyuliwa sauti.
 
Yap!....bila Uchumi imara huwezi kuwa na nguvu kubwa za kijeshi.

Nilijua askari wa Urusi wamepata uzoefu sana huko Syria hivyo Ukraine ingetekwa kirahisi lakini mambo ya kijeshi hayapo hivyo.

Vita vya Georgia mwaka 2008 vilionyesha udhaifu mkubwa wa Urusi na wizara yao ya ulinzi iliahidi maboresho makubwa....

Namna walivyoitwaa Crimea mwaka 2014 walionekana bora Sana na hata walivyo 'perform' Syria walikuwa bora zaidi nadhani hawakukutana na upinzani imara ndio maana walionekana bora ila si kwamba wapo imara.
 
Twajua dini yenu ina chuki na USA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Twajua dini yenu ina chuki na USA

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo ndipo ulipoonesha ujinga wako dhahiri shahiri. "Dini yenu" unamaanisha nini? Ina maana "dini yenu" inachuki na Mrusi? hueleweki, usiwe poyoyo.

Huko ndio kujielezea kijinga, funguka tu tukupe Ilm bila khiyana.

Au umemaanisha Uislam? Kama ni hivyo, elewa kuwa Uislam hauna chuki na yeyote duniani. Usome Uislam uuelewe. Wanaousoma Uislam wakauelewa leo hii wanarudi kwenye Uislam makundi kwa makundi.

Hata huko USA leo hii ndio taifa la kwanza duniani kwa watu wengi zaidi kusilimu na kurudi Uislam, kujisalimisha kwa Mola wao muumba wa vyote.

Wengi huko USA wameamua hawataki kubaki kwenye "imani" zinazoongozwa na mashoga na wabakaji wa watoto wadogo. Hulielewi hilo? Vipi wewe, bado upo katika imani inayoongozwa na mashoga na wabakaji wa watoto wadogo? Wamekuacha salama kweli? Au ndio mwenzao? Maana unavyojielezea ni kigasho gasho.
 
Post bora niliyoamka nayo leo.
 
View attachment 2142904

Ukraine Sio Syria huyu ni Major General wa kikosi Cha Russia, kulingana na Taarifa za kiintelejensia za Ukraine ameisha liwa kichwa.


Leo pia nitaendelea kupost mizoga ya Askari wa Russia
Dah!....usituwekee picha za maiti bhana...

Tupostie taarifa nyingine tu kuhusu hii Vita.
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…