LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
img_1_1646640244185.jpg
 
Na wengi aliowapeleka inaonekana ni kutoka upande wa Mongolia ( wenye asili ya mongolia
Wengine wengi ni kutoka nyanda za milima ya Urals. Nimeshagusia kuwa wamekuwa drafted kwenda jeshini vijana wadogo na experience hawana alafu wanakutana na jeshi la Ukraine linalopigana since 2014. Ni vijana maskini kutoka jamii minorities za Russian Federation, at least Chechens wana uzoefu na kupigana na huwa wanapenda vita na actually kupigana wanaweza sana wale hata ile Chechen war kwenye ile uprising majeshi ya Russia yalipigwa hovyo na vifaru vikaharibiwa hivihivi.

Hao troops walioenda hutowaona Caucasians wengi wale wa Western na miji kama St. Petersburg, utakuta mostly ni from Siberia uko. Labda maofisa na wataalamu. Binafsi Putin huwa naona ana dalili za kuwa na asili ya Eastern part kule kwa kina Mongols
 
Urusi atawaua hao waukraine hata kwa kemikali za sumu ,subiri amalize kwanza kukusanya ushahidi anapopita ili mtu akipigwa kipigo cha mbwa mwizi kusiwepo kelele za tunaonewa. Wanaompa jeuri huyo mchekeshaji ndio watakuja kuona Russia ni makatitli sana.

Maana kama Russia imeona silaha hatari hivyo kwa adui hapo hatakuwa na cha msalia Mtume
Kwenye hiyo kada ya Polonium 210 Russia ndio wanatisha duniani
 
Kuna mamburura humu yamekomalia NATO NA US zimeufyata , wanafikri vita ni movie za Rambo na Anord swazeneger.... Vita ni kifo , wazungu wanauzoefu na vita
Mzungu hahitaji kutanua scale of war , nje watatangaza hawataingilia mzozo , ili eneo la vita libaki kuwa Ukraine hapo hapo , ndani watahusika kimya kimya , now wanademand Sana raia watoke ili Ukraine iwe battle zone endapo Urusi hata kubali kusitisha mapigano ...
Raia wote wa Ukraine wanaotoroka wamepewa ofa ya kuishi ulaya na kufanya kazi , huoni tu hapo kuna kitu ....!!!

Propaganda sasa ni kuonyesha uharibifu anaofanya Russia , huku matamko yakitolewa NATO na US kutoingilia , dunia nzima itaihurumia Ukraine ..kumbe watu Wana mission zao ....leo US wamesema tayar uwezo na nguvu zote za kivita za Russia zipo Ukraine Kwa [emoji817], na wakasema Ukraine bado ipo stable kudefend fiercely airstrike..!!
kwa %100 unatudanganya leta ushahidi
 
Inawezekana jeshi la anga la Urusi wanyonge sana kwa Israel na NATO countries.

Urusi bado wanaendesha operesheni za kijeshi kama enzi za Soviet.
Training ni gharama sana. Tunarudi palepale kuwa bila uchumi ni vigumu kuwa na jeshi kubwa. Injini nyingi za ndege za Urusi nakumbuka hazifiki 70% ya lifespan ya injini za kampuni kama Safran ya Ufaransa, RR ya UK na PW au General Dynamics za Marekani. Ukifanya mazoezi sana unaongeza wear and tear hasa kwa engine parts na landing gear. Bado zile drills zinataka ammunition na fuel. Bado logistics na mambo kibao. Jas-39 Gripen niliyotaja hapo juu ina $7,500 cost per flight hour ni lowest kwenye modern fighters. Hapo tunazungumzia milioni 17 hivi zetu kwa lisaa, wakati kwa mwaka marubani wa Russia huruka angani kwa wastani wa masaa 100. Marekani marubani wao huruka masaa 200 kwa kawaida na huruka 350hrs kwa mwaka kama wako deployed kambini.
 
Habari zenu wanaJF wenzangu.

Ukraine na Urusi wana historia ndefu ambayo wanaulaya wa magharibi wanaitambua lakini nahisi wamarekani hawaitambui vizuri kwa sababu elimu yao haifundishi sana mambo ya dunia nje yao. Wengi wetu kutokana na habari propaganda hatutambui hivi vita havikuanza majuzi na wala si mrusi alienzisha.

Kwa historia ya karibuni - WanaUlaya wa magharibi na wa mashariki walivamiwa na Hitler akiwa na nia tofauti kwao. Nia ya Hitler kwa wanaulaya magharibi ilikuwa kuingiza ufashisti, yeye akiwa ndo mfalme na wajerumani wakiwa ndo binadamu bora kutawala dunia. Kwa wanaulaya wa mashariki, hakuwapenda kabisa, sijui mipango yake ila moja moja kati yao alitaka kuwatekeza wale wazungu wayahudi. Wanaulaya wa mashariki walikuwa waslavic, warusi, na wale waliojiita wayahudi (waashkenazi). Vilikuwa ni vita vya kufa na kupona espesheli kwa sababu Hitler alishawavamia wote na kuteka nchi zao na alikuwa na jeshi moja machachari sana lenye silaha za kisasa enzi zile. Ikumbukwe tayari wanaulaya wa magharibi na wa mashariki walishakuwa wanabaguana kama vile maadui wa kiitikadi na kifilosofia. Vita vya Hitler viliwapa adui mmoja wakapumzisha tofauti zao na kusaidiana kujikomboa. Ukweli mmoja historia haisisitizi, ni majanga kwa wanaulaya mashariki kutoka kwa Hitler. Ndio vita ni vita ila Hitler alikuwa anawateka wanaulaya magharibi kuliko kuwaua, na ilikuwa kinyume kule kwa wanaulaya mashariki. Pamoja na waslavic, mrusi amemwaga damu nyingi sana kujikomboa na kuwakomboa binamu zake waslavic. Alijengewa minara ya kumbukumbu za mashujaa ya kutosha Ukraine, historia haidanganyi na waUkraine waliienzi historia hii.

Wanaulaya kwa Pamoja walimtwanga Hitler hadi chumbani kwake. Yaani vita vinaisha, wanaulaya magharibi wana nusu ya ujerumani, na warusi wana nusu ya ujerumani, yaani hata mji wa Berlin ilikuwa nusu nusu tumekutana. Sasa ile bifu na ule utofauti wao walioweka pembeni ulirudi mezani. Sijui ni uchovu wa vita virefu ila uamuzi ukawa ulichoteka chako na papo hapo ‘vita baridi’ vikaibuka. Hapo ndo pia kuibuka Ujerumani mashariki na Ujerumani magharibi na Berlin mbili. Pia hapa ndo kukaibuka muungano uliounda USSR (urusi kubwa ikiwa na Ukraine ndani yake) na nchi kadhaa huru za kislavic alizokomboa mrusi zikawa marafiki na tegemezi wa mrusi. Sasa kukiwa na vita lazima kuwe na mipaka ya kutovuka na kuwepo na majeshi ya kulinda mipaka hiyo. Hapa ndipo majeshi ya muungano yakaanzishwa - NATO ya wamarekani na wanaulaya magharibi, na WARSAW PACT ya warusi na wenzao waslavic. Umoja wa kirusi ulipovunjika, WARSAW PACT nayo ilivunjika na nchi kadhaa kama Ukraine zikawa huru. waUkraine waliiheshimu historia hii na undugu wao na warusi. Historia inathibitisha enzi hizi za haya majeshi - hakuna damu iliomwagika ulaya.

Historia imenionyesha kwamba hakuna mtu muongo wa ahadi kama mzungu. Anapenda sana kusisitiza tuamini neno lake lakini kwa kweli historia inatuonyesha tena na tena anavowageuka aliowaahidi. Historia pia imenionyesha mzungu akikuchukia atakufanyia vituko hata kukuvamia akikusingizia una makosa aliyoyaeneza yeye. Wazungu wa magharibi waliona upenyo enzi za Gorbachev wakamshangilia wakichochea avunje urusi kubwa awarudishie ujerumani waliyoiteka vitani na awape waslavic uhuru nk wakampa hata Nobel. Wakamu”ahidi” sasa kuna amani hawana haja kutanua mipaka ya NATO na hawatusumbua usalama wa mrusi – tatizo mrusi hakupewa ahadi ya maandishi, kwa mfano ya juzi ya MINSKi. Wanaulaya magharibi wanamruka mrusi eti hawakutoa ahadi hizo ila Imedhihirika kwa taarifa kadhaa kwamba madai ya mrusi ni ya kweli. Pia maraisi wa urusi kuanzia Gorbachev, Yeltsin na Putin wote wamelalamikia kupewa hii ahadi hewa na wameonyesha wapi na lini. Basi imeonekana pia kama mrusi anavodai yote yalikuwa uongo na ahadi hewa kwa sababu kumbe wanaulaya magharibi bifu liko pale pale kwa mrusi na walikuwa wanamezea mate jinsi ya kunyakua maeneo anayoachia.

Wanaulaya magharibi walianza kampeni ya kuchochea nchi za kislavic kumgeuka mrusi na kuanza kutanua mipaka ya NATO. Haikujalisha hata kama nchi bado inakiuka itikadi zao ili mradi tumfikie mrusi, kwa mfano Poland. Nchi za kislavic zilizokataa zinashughulikiwa kiuchumi hata kijeshi. Mfano, NATO walivunja sheria za kimataifa na kuivamia na kuivunja Yugoslavia. Umoja wa Mataifa ukamezea hakuna mashtaka kule Hague. Chombo chao.
Angalia ramani hii hapo chini ya mtanuko wa NATO tokea watoe ahadi hewa...
00B UKRAINE - NATO ILIVOTANUKA BAADA YA USSR.jpg



Tuangalie Ukraine sasa. Hadi miaka ya majuzi waUkraine na warusi walionekana kuheshimiana na kuwa marafiki wanaolewana kimila na kwa vilemba. Hii ni kabla ya kuingia kiongozi ambae warusi wanadai ni kibaraka wa wanaulaya magharibi na aliepindua serikali mwaka 2014. WaUkraine hawakuwa na shida na ishara za kirusi nchini mwao kwa mfano kumbukumbu za vita vya ukombozi wao. Sasa anaingia huyu kiongozi, kunaibuka kundi la waUkraine wengi vijana wenye itikadi wazi ya Hitler na wanaanzisha kundi la kijeshi lenye nembo ya swastika na wanajiita NATIONALIST. Wanaungwa mkono na serikali ya Ukraine kwa sababu hawakemewi. Wanaulaya magharibi wanaliona hili lakini bado wanaingiza pesa na silaha zinazofikia kundi hili. Sasa hawa NATIONALIST Wanaanza kuwa na sauti na uhuru mkubwa kama chombo cha wawakilishi wa Ukraine, na wanaanza kubeza mrusi na kutaka eti “kufuta” historia ya mrusi ndani ya Ukraine. Wanachochea ubomoaji wa minara na ishara za majeshi ya ukombozi ya warusi. Wanachochea na kuvamia kijeshi miji ya wenye asili ya kirusi espesheli ya kule mpakani kama DOMBASS na LUGANSK wakinyanyasa raia tokea 2014. Inasemekana ni wao walivamia kituo cha nyuklia ili wampakazie mrusi. Zipo Habari za wao na ushirika wa serikali kutenda mambo kama haya ili wamsingizie ukatili mrusi Pamoja na porojo propaganda nyingi. Bado kwa ruksa na ushirika wa serikali ya Ukraine, wanavamia na kupiga mabomu kule dombass na Lugansk. Wanaulaya magharibi wanakazana kuwaita wapigania uhuru wakisaidia vita vya Habari porojo propaganda – kwa kweli wanachochea vita kuliko suluhu.


1646689220778.png

00B UKRAINE - JESHI.jpg


Hivi ni vita vya ubaguzi. Cha kusikitisha ni kwamba huu ubaguzi umeota miguu ya pweza. Viongozi wachochezi hawajali raia wa dunia ila wanataka tu kuungwa mkono na upuuzi wao, wakitishia dunia na ubabe wao kwa yule asiwaunga mkono. Poland ambayo majuzi ilijenga ukuta na kutumia risasi kutishia wakimbizi waarabu na Weusi, leo inashangiliwa ni karimu inapokea waUkraine kwa wingi. Taarifa nyingi tayari zimeonyesha ubaguzi katika kuruhusu nani aondoke kwanza na aingie Poland. Wanafunzi wa kiafrika na wengineo wa kigeni na raia wanapata tabu sana za ubaguzi leo hii. Halitangazwi. Ile miji ya warusi inayopigwa mabomu watu kufa na kuumia tokea 2014 hadi leo hii, hawatangazi – hata chupa ikivunjika Ukraine matangazo yanakuzwa. Wamarekani na waisraeli wamevamia sehemu kadhaa na mara nyingi lakini hata siku kupata masanksheni makubwa hivi. Wanamichezo na biashara za warusi zinafungiwa kushiriki duniani chap chap wakati Hitler aliruhusiwa kuwa mwenyeji wa olimpiki na wakashiriki vizuri tu bila kuigomea.

00B UKRAINE - UBAGUZI.jpg

00B UKRAINE - UBAGUZI 2.jpg



Wahenga walisema ukichezea moto utaungua na za mwizi arobaini. Dunia wakati inapitia majanga makubwa kiafya na kiuchumi kutokana na covid, mmarekani anachochea vita vyake vya kibinafsi kutuongezea majanga haya. Sehemu nyingi duniani Pamoja na ulaya na marekani, bei za vitu zilipanda wakati wa covid. Bado raia hatujapona sasa bei ndo zinapanda zaidi kwa sababu ya vita hivi. Nahisi itafika mahali huyu kiongozi mmarekani na wenzake ulaya wataonekana vile wanajali watu wa kawaida, na hizi kero zitawalipukia. Mwanauchumi yeyote atakwambia kufungia urusi biashara na Ukraine kutofanya biashara kutaumiza sisi wote duniani, hata kwao wamarekani na ulaya - sio warusi peke yao. Hili swala wamarekani wameliona ila ujeuri bado unawapelekesha afu wanavunja hata miiko sasa wakitaka mafuta hata kwa adui kama Venezuela. Pia kinachoonekana kama michango ya wanadunia na makampuni kuacha biashara na warusi – kwangu mimi ni uoga kwa sasa, itakapofika pale mahali mifuko haina hela hakuna biashara tutawaona na kuwasikia tena.
00B UKRAINE - ATHARI ZA VITA KIUCHUMI.jpg


00B UKRAINE - ATHARI ZA VITA KIUCHUMI 2.jpg


00B UKRAINE - ATHARI ZA VITA KIUCHUMI 3.jpg



Wamarekani na wenzao wanaulaya magharibi wametumia mbinu zao zile zile za zamani - Ukitaka kuanzisha vita lazima uonyeshe adui, na unaanza kwa kumpakazia mavi afu vita nae. Tatizo ni kwamba dunia ilishastukia staili hii, tunakumbuka Saddam na qadafi, tunachunguza Zaidi. Mjerumani ameamua kutumia akili mapema tu, akijali uchumi wake kuliko upuuzi huu japo hasemi wazi ila kwa vitendo. Nahisi wengi watafuata mkumbo espesheli ulaya pale njaa itakapozidi.

Sijaelewa kwa nini waUkraine wanaamini ghafla wanaulaya magharibi na wenzao wanawapenda baada ya kubaguana kwa miaka mingi. Ningekuwa muUkrainia ningeshatambua hawa jamaa wananichochea nipuuzie maongezi ya amani, nipigane hadi kifo wakinipa silaha LAKINI wananiambia hata nilie vipi niumie vipi hawataniletea majeshi ya kunisaidia vitani - ?sasa Nikiisha mm muukrainia nani anabaki hai kunyakua nchi.

SASA WAAFRIKA, WATANZANIA – HUU NDO MDA WA KUCHEZA MCHEZO WAO WA MIAKA NENDA RUDI – SERIKALI KUTUMIA MAJANGA YAKO KUTAJIRIKA NA PIA KUEPUSHA SISI WANANCHI KUUMIA NAO NDANI YA VITA VYAO VYA KIPUUZI, KWA MFANO NCHI AFRIKA ZENYE MAFUTA ONGEZA MTIRIRIKO NYUMBANI ILI BEI ZIBAKI CHINI – ZINAPANDA KILA SIKU MAGHARIBI NA MASHARIKI. HAMASISHA NA WEZESHA KILIMO CHA TIJA SABABU YA VITA HII, KWA MFANO NGANO ITAKUWA ADIMU KWA SABABU UKRAINE NA URUSI WALIKUWA WAUZAJI WAKUBWA SANA … MASOKO YAKO MENGI KARIBU NA MBALI, NI SISI KUTAMBUA MILA ZA CHAPATI NA MKATE.
 
Mkuu utakuwa mwehu Sana ukilinganisha Russia na Ukraine , Russia kuivamia Ukraine ni kama wewe ukapigane na mtoto w darasa la Kwanza , haijalishi utampiga Kias gan Ila Kwa jinsi atakavyokubishia itashangaza wengi ... Hata hvyo hii vita Russia hashindi , mda ndo mwamuzi
nisuala la muda tu kabla ya RUSSIA kushinda hii vit MKUU
 
Training ni gharama sana. Tunarudi palepale kuwa bila uchumi ni vigumu kuwa na jeshi kubwa. Injini nyingi za ndege za Urusi nakumbuka hazifiki 70% ya lifespan ya injini za kampuni kama Safran ya Ufaransa, RR ya UK na PW au General Dynamics za Marekani. Ukifanya mazoezi sana unaongeza wear and tear hasa kwa engine parts na landing gear. Bado zile drills zinataka ammunition na fuel. Bado logistics na mambo kibao. Jas-39 Gripen niliyotaja hapo juu ina $7,500 cost per flight hour ni lowest kwenye modern fighters. Hapo tunazungumzia milioni 17 hivi zetu kwa lisaa, wakati kwa mwaka marubani wa Russia huruka angani kwa wastani wa masaa 100. Marekani marubani wao huruka masaa 200 kwa kawaida na huruka 350hrs kwa mwaka kama wako deployed kambini.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom