LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Wakuu nipo kwenye huu uzi nafuatilia kimyakimya... Bado wiki chache sana tuimiliki Ukraine

Taarifa mpya ni kwamba, Marekani inapiga kelele kwa wakazi wa dunia kuwa tuichukie Urusi ila chinichini anaomba kikao cha ngazi ya juu kati yake na Urusi ili wayamalize kikubwa... Bahati mbaya Putin kakataa na kasema lazima akamilishe misheni yake au kibaraka wao ajiuzulu ili Russia ipange serikali upya ndani ya Ukraine.

Tuendelee kula mtori
 
US wants to destabilise Russia by allowing Ukraine to fight for nothing!

US and NATO have no plans to invade or fight Russia, but rather pushing Ukraine to fight.

Ubinafsi mkubwa huu! Leo anatoa vikwazo kwa Venezuela ili apate mafuta, ameona stock na production aliyonayo haitoshi, ataishia kupandisha bei za bidhaa. Biden's miscalculation.
Kwamba unajua kuliko wao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Russia unaemsemea kwamba anafanya biashara na Western ni baada yakuvunjika kwa USSR ndipo sera za kufungua uchumi zilianza miaka ya 90.

Sera za udikteta kwenye uchumi ni kama hizo ulizosikia wanasema eti wata nationalise,mambo kama hayo huwa wawekezaji hawataki lakini jambo kingine na security in large.

Kwa.huu mgogoro ni wazi Russia sio sehemu salama ya kuwekeza kama China nk kwa sababu sera zake za usalama zinalenga kutumia nguvu zaidi mwisho wa siku ni uharibifu na vikwazo.

Kwa mazingira kama haha Russia itasalia Nchi ya hovyo tuu,Nchi kama South Afrika, Nigeria na Egypt zitaifika na kuipita.

Swala la China kuwa neutral ni suala la kupiga hesabu za Uchumi zaidi,China alikuwa na uhusiano mzuri na Nchi zote mbili na juzi tuu hapo katoa msaada wa kibinadamu na infact China inapenda suluhisho la majadiliano zaidi kuliko vita.
Maoni Binafsi sio?
Kwahiyo ulitarajia nini? Kampuni ambazo zimeshiriki kuiwekea vikwazo Nchi, ziendelee kuwepo?
Umeweka mahaba mbele, kiasi kwamba huoni hata Vitu vidogo vilivyo wazi.
 
Na ndivo No Fly Zone ilivo....

Sasa apo si ndo itakua kuingia kwe hyo vita mazima au me ndo sijaelewa [emoji848]
Mwandishi wa habari kamchota akili hapo!

Alimuuliza nini maana ya no fly zone? Jawabu akabaki kimya hajui!

Akamuuliza unataka kulipua ndege za Urusi nchini Ukraine? Akajibu ndiyo! Putin amevuka mipaka.

Mwandishi kamchota akili. Inaonekana hajui anachokizungumzia huyo mwanasiasa.
 
Duh ni atari, sasa najiuliza tena apa kama ni kweli Russia ana Sera za kidikteta kwenye uchumi tfauti na Mchina.

Hayo makampuni yanayojitangaza kila kukicha kujitoa kwenye soko la urusi yalienda kutafuta nini.

Kama Urusi wana sera ya kidikteta kwenye uchumi ilikuaje mmarekani na mataifa ya ulaya yakafanya nae biashara (ambao ndo uchumi wenyewe) tena kwa kui'mports zaidi kutoka Urusi kuliko ya yeye Mrusi anavo'import kutoka kwao...

Na ukiitizama hyo screen shot uliyoiambatanisha apo nazan ni kipengele kiasi katika maelezo yalotolewa na upande wa China.

Hadi sasa taarifa niliyonayo hakuna Rafiki wa Urusi aliye'declare wazi kumuunga mkono kumpiga Ukraine zaidi ya kukaa "Neutral"...

Ni china walogomea Unilateral Sunctions za Mrusi uku wakisema "kua vikwazo sio suluhisho mgogoro" akati huo huo wakikutana na Chancellor wa Germany Rais wa France huyi Malcon kujadili namna gani watalisolve hyo Issue kidiplomasia....

Sasa nirejee tena kwako kwasababu nataka kuelewa zaidi. Udikteta wa kiuchumi ukoje labda au me ndo siujui.
Nakupa mfano mmoja. Kuna oligarch mmoja aliitwa Mikhail Khodorkovsky na alinunua kampuni ya mafuta ya Yukos miaka ile ya 1990s walipofanya ubinafsishaji wa makampuni ya serikali na kuwapa oligarchies kwa mauzo ya chini sana. Baadae mwanzoni mwa miaka ya 2000 huyo bwana akawa mpinzani wa sera za Putin na akajihusisha na siasa, kampuni yake ikatungiwa kesi ya madai ya mabilioni ya kodi. At the time ndio ilikuwa kampuni kubwa ya mafuta Urusi, ikataifishwa yote na yule jamaa akafungwa miaka 10 kisha akaachiwa mwaka 2013 akaenda kuishi uhamishoni Uingereza. Mali za kampuni yake zikataifishwa na kumilikiwa na Rosneft kampuni ya mafuta ya serikali. Ile Yukos ilikuwa na shareholders makampuni tofauti duniani wote wakala hasara. Ni mfano mmojawapo wa sera na sheria za Urusi zisizoeleweka kwa wawekezaji, wanakaa na hofu serikali na viongozi wako juu ya sheria hakuna uhakika wa haki. Mwekezaji hapendi sehemu kama hii.

Huo ndio udikteta wa kiuchumi. Marekani watu kama Trump wametoka kwenye biashara wakagombea siasa na hutokaa usikie mamlaka za mapato nchini kwao zinawatungia kesi za uongo
 
W
Zile ni thermobaric weapons kwenye system ya TOS-1 Buratino. Zinakuzwa uwezo wake kwa kutiwa chumvi kiasi na media, kuna mabomu kama cluster bombs na incendiary explosives kama napalm bombs na white phosphorus hizo ni hatari kupindukia. Ukiona silaha haijapigwa marufuku na mikataba ya kimataifa wakati imetumika muda ujue haina madhara sana, thermobaric weapons hazizuiwi popote.

Huwa TOS-1 inatumika kwenye enemy fortifications kama bunker, tunnels na majengo ambayo adui wamejificha.
Wewe mwanajeshi? Sio kwa kujua huku
 
Russia unaemsemea kwamba anafanya biashara na Western ni baada yakuvunjika kwa USSR ndipo sera za kufungua uchumi zilianza miaka ya 90.

Sera za udikteta kwenye uchumi ni kama hizo ulizosikia wanasema eti wata nationalise,mambo kama hayo huwa wawekezaji hawataki lakini jambo kingine na security in large.

Kwa.huu mgogoro ni wazi Russia sio sehemu salama ya kuwekeza kama China nk kwa sababu sera zake za usalama zinalenga kutumia nguvu zaidi mwisho wa siku ni uharibifu na vikwazo.

Kwa mazingira kama haha Russia itasalia Nchi ya hovyo tuu,Nchi kama South Afrika, Nigeria na Egypt zitaifika na kuipita.

Swala la China kuwa neutral ni suala la kupiga hesabu za Uchumi zaidi,China alikuwa na uhusiano mzuri na Nchi zote mbili na juzi tuu hapo katoa msaada wa kibinadamu na infact China inapenda suluhisho la majadiliano zaidi kuliko vita.
Nakufatilia vyema... Kuna point unazitoa af kuna mahaba pia unayaingiza.

Ukitaka u'judge rationale kwanza uwe huru na hisia zako juu ya jambo lenyewe otherwise unaeza kua na point ya msingi af ukakosa mahala sahihi pa kuiweka.

Uhalisia ulivo nenda karudie kuhusu kuisoma taarifa ya "Nationalising Asset"... Kilichosemwa n tofauti na unachokielezea ila yote nahisi ni kwasabab ya hisia zako hasi kwa upande mmoja.

Sasa em nambie kwa usahihi mpk sasa walioongoza kwa "Seizure" mali tena ambazo sio za Putin bali watu tu walo na mahusiano na Putin n Western Europe kwa UK n US.

Mfano kilichotokea kwa Abrahmovic kinaleta picha gani kwa wageni waliowekeza UK ambao wana mahusiano na Politicians wa nchi walizopo.

Ko siku na wao wakitofautiana mali zao zitachukuliwa vile vile.

Haya hapo naona kuna screenshot umeiweka ikionesha namna wanavoanza kutoka Europe kwenda Dubai kuhifadh fedha zao na mali zao zisije ingizwa kwe sakata la Putin.

Je do you think this is healthy kwa Investors ambao wana mahusiano ya na wana siasa wa Nchi zao?....

Endeleq kupunguza hisia kwa kila upande hivo hivo naamin ntajifunza vitu kutoka kwako.
 
Sasa unajua Russia kuna kampuni ngapi za wawekezaji kutoka west? Nchi zote zilizomwekea Russia vikwazo: Yaani ukijijua umemuwekea Russia vikwazo halafu katika nchi yao una makampuni yako, panga lililopita linalojadiliwa sasa hivi ni kuzi- nationalizing.

Omba wanaolijadili walijadiri kiustaarabu.
 
Nakupa mfano mmoja. Kuna oligarch mmoja aliitwa Mikhail Khodorkovsky na alinunua kampuni ya mafuta ya Yukos miaka ile ya 1990s walipofanya ubinafsishaji wa makampuni ya serikali na kuwapa oligarchies kwa mauzo ya chini sana. Baadae mwanzoni mwa miaka ya 2000 huyo bwana akawa mpinzani wa sera za Putin na akajihusisha na siasa, kampuni yake ikatungiwa kesi ya madai ya mabilioni ya kodi. At the time ndio ilikuwa kampuni kubwa ya mafuta Urusi, ikataifishwa yote na yule jamaa akafungwa miaka 10 kisha akaachiwa mwaka 2013 akaenda kuishi uhamishoni Uingereza. Mali za kampuni yake zikataifishwa na kumilikiwa na Rosneft kampuni ya mafuta ya serikali. Ile Yukos ilikuwa na shareholders makampuni tofauti duniani wote wakala hasara. Ni mfano mmojawapo wa sera na sheria za Urusi zisizoeleweka kwa wawekezaji, wanakaa na hofu serikali na viongozi wako juu ya sheria hakuna uhakika wa haki. Mwekezaji hapendi sehemu kama hii.

Huo ndio udikteta wa kiuchumi. Marekani watu kama Trump wametoka kwenye biashara wakagombea siasa na hutokaa usikie mamlaka za mapato nchini kwao zinawatungia kesi za uongo
Huo sio Udikteta wa kiuchumi T4....
Hizo ni figisu za kisiasa za kawaida.
Mfano Ilivyotokea saiv kwa Ibramovich wa chelsea tutauita udikteta wa kiuchumi?
Kwamba Uingereza hapana uhakika na Uwekezaji wako?
 
The West has made a number of mistakes in its relations with Russia, including the promise of NATO membership to Ukraine - Borrell, head of EU diplomacy.
SmartSelect_20220309-103148_Gallery.jpg
 
Maoni Binafsi sio?
Kwahiyo ulitarajia nini? Kampuni ambazo zimeshiriki kuiwekea vikwazo Nchi, ziendelee kuwepo?
Umeweka mahaba mbele, kiasi kwamba huoni hata Vitu vidogo vilivyo wazi.
Kabisa... Yani ukiwa na mahabba unaeza shusha IQ yako nje ukaonekana Ndezi ila ndani ukijiamini uko sawa...

Kwasababu kila kona utakuwa unatafuta taarifa ya kukufurahisha au kuzimulika hisia zako.

Zikija za kukufurahisha hata kama ni za Uongo utazipa kipaumbele. Na zikija zisizokufurahisha ata kama ni za kweli utaanza kuzitafutia kasoro...

Mahabba na kitu au mtu binafs sipendi na wala staki kuyarejesha tena... Unaeza kua Zuzu wa kujitakia au msukule wa bila ndumba...
 
Mwandishi wa habari kamchota akili hapo!

Alimuuliza nini maana ya no fly zone? Jawabu akabaki kimya hajui!

Akamuuliza unataka kulipua ndege za Urusi nchini Ukraine? Akajibu ndiyo! Putin amevuka mipaka.

Mwandishi kamchota akili. Inaonekana hajui anachokizungumzia huyo mwanasiasa.
Na ajabu sio yeye anayeenda kulipua... Kuna vijana anatuma. Wakifa yeye yupo ofisini ametulia.

Hakuna aina ya watu siwaamini na siwaelewi kabisa ka wanasiasa [emoji706]....

They know little af wana pretend kua much knowers over kila kitu.
 
Af kingine nikusihi uzungumze bila kutukana. No matter who he was... Ni marehem kwa sasa kumuita alikuwa "Fala" kwenye vitu ambavyo mawazo yako na yake hayakufanana si jambo la maana....

Just talk like Adult, matured and well desciplined.
Educate him bro, educate him[emoji123]
 
umeongea meengi ila sidhanii kama yana maana kabla ya huu mgogo haeakuyajua haya uyasemayo
pia unawapangiaje watu chakupenda c wana demoghasia wao
VIVA ROMAN
Huu ndio uhalisia wa ligi ya UK mnayoishangilia bila kujua ushenzi wake, na mgogoro huu haunihusu, ukweli ni kwamba serikali walikuwa wanampa Abromovich nafasi ya kuondoka kiistaraabu, ila hiyo mishabiki imemvurugia...sasa ni kutembeza bakuli kama miaka ya nyuma...
Labda atokee mwarabu awavalishe gauni...
 
Huo sio Udikteta wa kiuchumi T4....
Hizo ni figisu za kisiasa za kawaida.
Mfano Ilivyotokea saiv kwa Ibramovich wa chelsea tutauita udikteta wa kiuchumi?
Kwamba Uingereza hapana uhakika na Uwekezaji wako?
Umeniwah nilichotaka kumuuliza... Ani apa kwasababu sie ni Watanzania yatupasa tubaki na Utanzania kisha tuwajadili wao kama walivo as if tumeletewa kesi mahakamani...

Ani ni kupiga maswali kote kote ili tuupate ukweli. Judge akishrikiana na mtuhumiwa au mtoa tuhuma kesi haita'balance na huenda maamuzi ya mwisho yakawa sio sahihi kwa kias kikubwa.

Ko tuwe huru kuzinyumbua pande zote hakuna malaika apo...
 
Back
Top Bottom