LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Zelensky kaingizwa njini na matapeli US-led NATO
Nchi zote hizo zinapambana na nchi moja tuu?
Hao Nato wamemwinguza cha kike Ukraine sasa wanajitambatamba pembeni
Maafisa wakuu wa Umoja wa Ulaya, akiwemo Borrell mwenyewe, wamekataa wito wa Kiev wa kutaka kujiunga kwa haraka. Hakuna utaratibu wa haraka uliopo na nchi inayotaka kuwa mwanachama lazima ifikie hali tofauti za kisiasa na kiuchumi ili kupewa tu hadhi rasmi ya mgombea.
 
Wameona bora waendelee kula ugali
Screenshot_20220313-134020.jpg
 
Kabisa. Na elimu ya vitu hivyo siku hizi siyo za kujivunia. Maana unaweza kusoma online na ukajua uchumi.

Vitu ambavyo vinahitaji shule ya kweli ni udaktari, uinjinia na mambo ya fananayo na hayo.
Sio kweli Udaktari na uhandisi ndio unahitaji shule,field zote Shule sio lazima.Ukifatilia Historia za wanasayansi wengi wahakuwahi kwenda shule.
Mambo/vitu vingi vilianza kama instincts/imagination.
 
Kichwa champasuka Rais Biden.

Wakati Putin anashambulia vikali Ukraine muda huo huo Kim (North Korea) ametesti makombora ya balistiki ya kuvuka mabara (ICBM) yale ambayo Marekani huyaogopa zaidi ya korona. Marekani yasema North Korea imetesti kisirisiri makombora hayo ya ICBM kwa kuya-control yaruke kwa umbali mdogo.

Mwambieni Rias Biden awe mvumilivu, huo ndio ukubwa
=====
SmartSelect_20220313-134635_Chrome.jpg


 
Kaka unajaribu kufanya mizaha kuhusu mambo ambayo huelewi.
Unajaribu kufanya mzaha kuhusu vita ya nyuklia. Je unajua kama ingetokea, wewe utakufa pia?
Umewahi kukdiria idadi ya silaha za nyuklia zinazopatikana pande zote?? Urusi hapa, Nato (MArekani, Uingereza, Ufaransa) pia?
Umewahi kujifunza kidogo kuhusu mifumo inayoandaliwa tangu miaka 60 jinsi ya kutumia silaha hizo na kujibu kama upande mwingine unaanza kuzitumia?
Umewahi kutumia punje ya akili yako matokeo yatakuwaje?
Neno la "nuclear winter" umewahi kusikia??
Basi endelea na mizaha yako ya kitoto.

Mkuu umepaniki sana umepata lunch tyr?
 
Kichwa champasuka Rais Biden, Putin ashambulia vikali Ukraine na wakati huo huo Kim (North Korea) ametesti makombora ya balistiki ya kuvuka mabara (ICBM) yale ambayo Marekani huyaogopa zaidi ya korona. Marekani yasema Kim ametesti makombora hayo ya ICBM ila alidanganya kwa kuyarusha kwa umbali mdogo.

View attachment 2148877

Ila huyo jamaa wa north Korea anapenda uchokozi sana
 
Kaka unajaribu kufanya mizaha kuhusu mambo ambayo huelewi.
Unajaribu kufanya mzaha kuhusu vita ya nyuklia. Je unajua kama ingetokea, wewe utakufa pia?
Umewahi kukdiria idadi ya silaha za nyuklia zinazopatikana pande zote?? Urusi hapa, Nato (MArekani, Uingereza, Ufaransa) pia?
Umewahi kujifunza kidogo kuhusu mifumo inayoandaliwa tangu miaka 60 jinsi ya kutumia silaha hizo na kujibu kama upande mwingine unaanza kuzitumia?
Umewahi kutumia punje ya akili yako matokeo yatakuwaje?
Neno la "nuclear winter" umewahi kusikia??
Basi endelea na mizaha yako ya kitoto.
Vita hii hata ikitumiwa hizo Nukes hakuna madhara yoyote yataikumba Afrika labda mambo ya kiuchimi tu ila kifo hahaha hiyo hakuna. Likipigwa huko USA ni vipi litarufikia sisi huku kwa Bititi street? Mwanamkiwi acha kuwa mkiwa sana
 
Vita hii hata ikitumiwa hizo Nukes hakuna madhara yoyote yataikumba Afrika labda mambo ya kiuchimi tu ila kifo hahaha hiyo hakuna. Likipigwa huko USA ni vipi litarufikia sisi huku kwa Bititi street? Mwanamkiwi acha kuwa mkiwa sana
Mionzi itakufikia tu japo kidogo.
Usiombe hii vita.

Mrusia akirusha USA naye anarusha yanakutana anga za Afrika. Lazima madhara yakukute.
 
Back
Top Bottom