LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Hii point Yako hua inanifikirisha sana.Tuliambiwa na
Tunaambiwa Urusi ni nchi maskini,Leo inakuaje nchi zote zinazoitwa matajiri hapa duniani kwa pamoja zinashindwaje kuiadhibu nchi moja TU ambayo ni maskini?
Sio kazi rahisi kumfunga kamba 'kichaa' aliyeshika panga.
 
Mpenda haki hashadadii mbabe anayevuka mpaka wake kwenda kuuwa na kuharibu mali za majirani zake.
Nashindwa kuelewa maana ya neno "kushadidia".
Sijui maana yake.
Ila kitu nilichogundua ni kwamba huenda mjadala huu umeuanzia Hapa.
Kama uliuanzia mwanzo Kuna wadau waliufafanua kwa undani kabisa na kuonesha kua Urusi ana haki ya kuivamia Ukraine baada ya juhudi zote za kidiplomasia kishindikana.
Hata hivyo inategemea na utayari wako kuukubali ukweli.
Lakini uzuri wa mgogoro huu majibu yake yapo wazi kutokana na matukio yaliyokwisha kutokea.
Jibu mojawapo ni hili.
Unafahamu kua USSR ilipeleka makombora ya nyukilia Cuba ?
Je unafahamu ni Kwa sababu Gani USSR iliyapeleka Cuba?
Je unafahamu kua USA ilitaka kuivamia Cuba kwa sababu ya makombora hayo?
Je USA ilikua sahihi kutaka kuvuka mipaka yake na kwenda kuivamia Cuba kitu ambacho kingeharibu Mali za jirani yake Cuba?
 
Sio kazi rahisi kumfunga kamba 'kichaa' aliyeshika panga.
Ukichaa wa Urusi uko wapi hapo?
Mbona mmelewa propaganda kiasi zinawafanya mmekua hamuwezi hataa kuchuja mambo?
Kwamba nchi za west ndio zina akili timamu na nchi za east ndio vichaa?

Maana nchi za east na west zote zina miliki mapanga.
Lkn kwa maelezo yenu nchi za east TU ndio nchi zinazoongozwa na vichaa.
Nyie hupenda kusema Rais wa Korea kaskazini ni kichaa.
Mlikua mkisema Rais wa Korea kaskazini ni kichaa tokea Baba yake Kim Jon UN alipokua Rais. ,akaja uchukua uongozi mtoto mtu Kim Jon Un mwenyewe nae Sasa mnasema ni kichaa.Kwa hiyo ukichaa wa Viongozi wa KK ni wa kurithi?au hua unahama kutoka Kwa baba kwenda kwa mtoto?
Tuambieni basi kua ukoo wa akina Kim Jon Un ni vichaa ili tujue mapema ,maana akifa huyo kiduku Kuna uwezekano akaja Rais kutoka ukoo huohuo.

Sasa tuangalie kichaa ni yupi,Urusi alie na panga halafu hajalitumia? Ama Marekani alie na panga pia lakini keshalitumia?
Yupi ni kichaa hapa?
 
1716106438343.png
 
watu wamekimbia miji ya UKREINE.... Baada ya sheria kupitishwa ya KWENDA MSTARI WA MBELE......
(Narudia tena, hapa kwetu mwaka 1978 kulikuwa na vita vya Kagera watu walikuwa wanasonga wenyewe kwa ajili ya kwenda kwenye mapigano kukomboa nchi yao, wasioweza walikuwa wanachanga NG'OMBE, MBZU, KUKU, MAHINDI, NGANO , SUKARI n.k kwa ajili ya askari wetu walio mstari wa mbele, NAJIVUNIA JESHI LETU.....NAJIVUNIA PIA JESHI LETU LA MGAMBO) VIVA TANZANIA........ VIVAAAAAA!!!!!!

View: https://x.com/Zlatti_71/status/1792088812379607198
 
Back
Top Bottom