LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Sa unafikiri kwa uchumi wako ulio nao utaishije saizi bila kuwategemea hao watu?

Huyo mrusi tu saizi tunamuona gwiji lakini hivyo vikwazo alivypigwa kama vikiendelea lazima atayumba

Dunia ya sasa hivi inataka ushirikiano wa karibu ili uweze kujijenga, ukijetenga au kutengwa ni ngumu sana kutusua
 
Asante Mzee wetu...Mungu akuweke.
 
Namkumbuka kaburu Pick Botha. Alinyosha maelezo kwenye ile hotuba iliyoitwa mbaya wakati ni ukweli mtupu. Labda uwasilishaji wake ndio ulikuwa mbaya.
Wakati huo SA walikuwa kwwnye vikwazo. Na dunia ilikuwa ikijua hivyo. Kwenye ile hotuba akawa anawaambia baraza lake la mawaziri.
Nani ananunua dhahabu yetu? Nani anatusaidia katika miradi yetu ya nyuklia? Nani anafanya biashara na sisi? Ukweli ni kuwa wao ni wetu na sisi ni wao. German, America, Canada na Austria ndio watu wetu.

Kwa kifupi kuna nchi nyingi zinahitaji malighafi toka russia kuendeleza viwanda vyao. India kwa mfano viwanda vya chuma % kubwa ya mali ghafi wanachukua huko russia.
Kwa maoni yangu. Vikwazo vitatikisa tu uchumi wq russia lakini haviwezi kuuwangusha uchumi wenyewe.
 
Huwezi wapangia Ukraine nani awe Rais wao hicho ni kiherehere na ndicho Putin anafanya. Huyo Putin yuko wapi si yuko makazi yake Nova Ogaryovo amejificha na yuko Kremlin na vikao vya kuungwa mkono? Zelensky yuko field anapigana, aliyekwambia wanapigania ofisini mpaka wawe na settings za kurekodi hotuba wamekaa mezani nani. Zelensky is a hero na anaungwa mkono na raia.

Serikali yake aliyoiunda inaungwa mkono na raia zaidi ya sana, kila wizara ya ulinzi inachosema raia wanafuata. Zelensky katangaza Marshal law hakuna aliyepinga, wizara ya ulinzi imezuia wanaume aged 18-60 kuondoka mjini Kyiv hakuna raia aliyepinga wanaume wanasindikiza watoto na wake zao kwenye vituo vya treni wanarudi wenyewe kushika silaha. Wizara ya ulinzi imesema raia watengeneze Molotov cocktails na wamefanya. Mpaka wazee wanaunga mkono wajuu wao wapiganie nchi.

Putin hana uwezo wa kwenda mtaani bila maandalizi wala kukaa na wanajeshi wasio presidential security guards. Zelensky anaenda kukaa na wanajeshi wenye live munitions uko unakoita vichochoroni wakati Putin kawaambia wampindue na hawataki. Wakati huo polisi nchini Urusi wanakamata waandamanaji wanaoipinga vita. Nani anakubalika hapo?
 
Safi sana mkuu...Umeandika vizuri sana.
 
Kwa mtu yeyote anaeweza kunisaidia nn chanzo cha vita inayoendelea kati ya Ukraine na Russia, chimbuko lake hasa limeanzia wapi?
Urusi ilishaonya toka kitambo kwamba haitaruhusu kuona nguvu na ushawishi wa jumuia ya NATO inasogea karibu na mipaka yake !!!
 
It has been said that, Ukrine is the most corrupted country in the world.

lkn pia CIA wanaitumia sana Ukrine kama base yao kuipeleleza RUSSIA sasa Rusia haitaki huo ujinga either UKRINE ibaki na RUSSIA au iungane na USA ipate kichapo kikali.
UKRINE iamue yenyewe hatma yake.
 
Haviwezi kuja endelea... Sababu hizo nchi za ulaya zinategemea uwepo wa Russia ili kufanya uzalishaji katika nchi zao. Urusi si ndio mzalishaji mkubwa wa gesi hapo ulaya..?? Na inasambaa nchi nyingi za ulaya..??
 
Ukraine itakuwa nchi ya mwisho Russia kuishambulia kuhusu mambo ya NATO. NATO naona wamekuja full hapo Poland na nchi za jirani.
NATO wako Poland kuvizia Ndege za Urusi zizakazojichanganya zikaingia Poland. Urusi hataki kuchokoza any NATO affiliate hata Kwa bahat mbaya sababu anajua hapo ndo anapotegewa.

Yeye kaamua ku deal na Ukraine tu ili amalize mambo mapema. Akijichanganya tu Poland au Belarus NATO watafurahi sana, sababu atakua kaingia kwenye 18 zao. Hapo ndo perhaps WW3 itatokea.
 
Mkuu una points. Ila chanzo mgogoro sio Raisi bali mikataba ya nyuma ya kujilinda mara tu baada ya kusambarika kwa USSR.
Sawa nafahamu. Aina ya lugha walizokuwa wakitumia rais wao (ukraine) mabalozi wao huko UN na Washington ndio zilikuwa na ukakasi.
Wqngejaribu kutumia lugha nzuri na ya kushawisha. Wewe unaona kabisa Mpinzani anasogeza majeshi na vifaa vya kijeshi we bado unashupaza shingo.

Acha alipe gharama.
 
Amalizane kwanza na Ukraine ambaye ni weak mbele ya kina Poland na Finland. Russia uwezo wake uko exaggerated tukubali tu, vita atashinda ila weakness ashaonesha.

Ila nadhani inachangiwa na kupigania mjini, uko kwingine aliwashinda walikuwa hawajajipanga na hawakuchukulia serious kama watavamiwa. Haya mambo ya urban warfare Israel ndio wameishi nayo muda mrefu na silaha zao ziko kwa ajili ya urban pamoja na desert warfare. Urusi silaha zake ni za kupigania porini kwenye vast lands maeneo ya Siberia uko. Akitoka hapa atafanya modifications ya silaha na kujipanga dhidi ya vitu kama IEDs vilivyosumbua Wamarekani Uarabuni. Una kifaru kina armour ya kuzuia HEAT shell kikipigwa na rocket kinahimili, ila mpishi wa Ukraine anakirushia chupa ya petrol kinawaka moto, hajatumia hata TSH. 2000.

Kupigana na jeshi linaloungwa mkono na raia ni kazi sana. Kwanza wanoko, ukipitisha vifaru CCTV zao mtaani wanasoma wanawaambia wanajeshi wao mko wapi mnapigwa ambush. Mpaka Urusi baadhi wakavaa sare za Ukraine kufanya infiltration ila mambo magumu bado
 
Kuaminisha watu kuwa kuna saboteur groups kumeleta friendly fire nyingi sana......
Wanaua raia wao wenyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…