LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Wakuu mbona naanza kuhisi kuna mchezo unachezwa. Nahisi NATO na UN walifanya analysis mapema wakaona Urusi atavamia wakaamua wasubiri wapate justification ya kujibu na wasubiri kuona anaungwa mkono na nani. Sasa Putin yuko na vidagaa vya Chechen na Belarus, hana mbabe yeyote anayeunga mkono. Kwa sasa wanaamua watoe silaha kwa Ukraine.

Au NATO wamejishtukia baada ya kuona Ukraine imegoma kujisalimisha, response ya serikali na raia ni nzuri na wana spirit ya kupambana. Kwahiyo hata wakitoa silaha watumiaji wapo.

Au NATO walikuwa tiyari kuona Luhansk na Donetsk zinaanguka ila hawakujua kama Ukraine nzima itavamiwa. Baada ya kuona Putin anatishia madai mengine na kusemea wanachama wengine wa NATO waliojiunga baadae ikaonekana huyu mtu haaminiki ngoja tuisaidie Ukraine ili aone hatutakubali akija kwa mwanachama halisi.

Kikao cha jana jioni cha NATO plus Finland na Norway kuna siri itakuwa pale imeamuliwa. Naanza kuona response ya kina Biden haikuwa mbaya sana kama nilivyoona mwanzo. Maybe no tunakusubiri upige wee dunia ikuone, alafu tukija utakosa visingizio vya kwamba sisi ndio tulianza
NATO haiwezi mshambulia Puttin sababu ya Eukraine labda tu aiguse nchi mshirika wa NATO. Wasiwasi uliopo ni kuwa Puttin hatabiriki tena. Alisema hatoivamia Eukrain lakini akaivamia. Sasa NATO imeamua kujihami kwa kuhakikisha silaha hazipo mbali na Urusi ikiwa ataamua lolote.
 
NATO na Marekani kama wanaona mbali,Huyu Puttin ni wa kuondolewa madarakani bila kuchelewa vinginevyo kuna siku watajuta.
Hawana uwezo wa kumtoa Putin wale sio nchi za kiafrika
JamiiForums-703077379.jpg
 
Wakuu mbona naanza kuhisi kuna mchezo unachezwa. Nahisi NATO na UN walifanya analysis mapema wakaona Urusi atavamia wakaamua wasubiri wapate justification ya kujibu na wasubiri kuona anaungwa mkono na nani. Sasa Putin yuko na vidagaa vya Chechen na Belarus, hana mbabe yeyote anayeunga mkono. Kwa sasa wanaamua watoe silaha kwa Ukraine.

Au NATO wamejishtukia baada ya kuona Ukraine imegoma kujisalimisha, response ya serikali na raia ni nzuri na wana spirit ya kupambana. Kwahiyo hata wakitoa silaha watumiaji wapo.

Au NATO walikuwa tiyari kuona Luhansk na Donetsk zinaanguka ila hawakujua kama Ukraine nzima itavamiwa. Baada ya kuona Putin anatishia madai mengine na kusemea wanachama wengine wa NATO waliojiunga baadae ikaonekana huyu mtu haaminiki ngoja tuisaidie Ukraine ili aone hatutakubali akija kwa mwanachama halisi.

Kikao cha jana jioni cha NATO plus Finland na Norway kuna siri itakuwa pale imeamuliwa. Naanza kuona response ya kina Biden haikuwa mbaya sana kama nilivyoona mwanzo. Maybe no tunakusubiri upige wee dunia ikuone, alafu tukija utakosa visingizio vya kwamba sisi ndio tulianza
Kuhusu analysis ya uvamizi ilifanyika mapema, definitely! Hata intelligence za US na UK zilisema wazi kabisa kuhusu kuanza kwa uvamizi siku chache zilizopita.

Spirit ya Ukraine katika mapambano ni kubwa sana, so far. Nadhani dunia imeona, hivyo misaada ya kijeshi inayoongezeka si jambo la kushangaza. Silaha za kivita kama anti-tank missiles: British NLAW pamoja na Javelins kutoka Marekani zimesaidia kwa kiasi kikubwa sana kwa sasa dhidi ya vifaru vya Urusi pamoja na helicopters, kulingana na taarifa zilizopo.

Mizinga pamoja na stinger missiles kutoka Czech pamoja na Baltic states pia vimekuwa msaada mkubwa kwao, bila kusahau TB2 drones kutoka Uturuki. Kuna taarifa ya muda si mrefu kuwa nchi takribani 28 zimeridhia na zinapanga kupeleka misaada zaidi zikiwemo silaha.

Kuna taarifa pia kuwa Ukraine imeomba msaada kwa shirika la kimataifa la Msalaba Mwekundu kusaidia kuondoa maelfu ya miili ya wanajeshi wa Urusi kuirudisha nchini Urusi. Kama ni sahihi (kulingana na taarifa ya Naibu Waziri Mkuu), inaonesha resistance iliyofanyika ni kubwa sana.

Hata hivyo, bado ni mapema. Tusubiri tuone kile ambacho kitajiri hapo baadaye!
 
NATO na Marekani kama wanaona mbali,Huyu Puttin ni wa kuondolewa madarakani bila kuchelewa vinginevyo kuna siku watajuta.
Putin ni zaidi ya umjuavyo, Marekani na NATO wanamuelewa vyema zaidi yako. Putin anazungumzwa kuwa hana historia ya kushindwa vita yoyote aliyowahipigana kwa milongo miwili (two decades) aliyokaa madarakani.

 
Askari wa kirusi hawaña motisha ya kupigana kama wenzao na hapo Ndio maelfu ya wanajeshi wao watakufa. Nilitarajia atatumia mbinu kama za Irael za kushambulia Toka mbali. Yeye anakuja kichwakichwa.
Kumbuka lengo lake ni kuonesha mobilization
 
Manina Russia wakutane na Poland ana kwa ana hiyo vita itakuwa sio ya kitoto,Poland wana hasira za kihistoria na Russia,Russian infantry ni wakawaida sana sio kama dunia inavyowapamba kabisa..
Kwanza hadi sasa ni siku ya 4 Russia imeshindwa kuweka No fly zone hapo Kyiv pamoja na Airforce power walionayo,ni kitu cha kushangaza sana.
Yule pilot wa Ukraine wanamuita nickname Ghost of Kyiv ameshaka kula jets 4-6 za Urusi hadi sasa,ikiwemo the most advanced Su-35 ila jamaa anda Mig-29...Jamaa ni mzee tu late 50s...
Vita ni timing na ujanja ujanja
 
Boots on ground ni risky sana hainaga mwenyewe aisee,Na sasa raia karibia 30k wa Kyv tu wana silaha mkononi za kuwaua warusi wakiingia Kyiv,Hata Russia akishinda hii vita atapata tabu sana kuitawala Kyiv.
Alidanganywa anakubalika ndo maana kaingia kichwa kichwa
 
Mbona zipo Cuba na hakuna vurugu
Chanzo cha kuwepo hapo Cuba unajua nini au unaandika tu bila kujua?

Miaka ya 1960 Cuba alihitaji kuondolewa hizo NATO bases ndani ya Cuba na alimwomba RUSSIA msaada kumwondoa USA na RUSSIA alifanikiwa kuondoa NATO ndani ya Cuba.

Hapo ndipo mahusiano mazuri baina ya Russia na Cuba yalipoanzia, ndiyomaana unaona USA hawezi kuleta fyoko fyoko kuhusu hayo majeshi ya Russia huko Cuba
 
Aisee hizi siasa za vita ni ngoma sana. Afu kuna watu mnaishabikia US kama vile ni dini yenu
Kuhusu analysis ya uvamizi ilifanyika mapema, definitely! Hata intelligence za US na UK zilisema wazi kabisa kuhusu kuanza kwa uvamizi siku chache zilizopita.

Spirit ya Ukraine katika mapambano ni kubwa sana, so far. Nadhani dunia imeona, hivyo misaada ya kijeshi inayoongezeka si jambo la kushangaza. Silaha za kivita kama anti-tank missiles: British NLAW pamoja na Javelins kutoka Marekani zimesaidia kwa kiasi kikubwa sana kwa sasa dhidi ya vifaru vya Urusi pamoja na helicopters, kulingana na taarifa zilizopo.

Mizinga pamoja na stinger missiles kutoka Czech pamoja na Baltic states pia vimekuwa msaada mkubwa kwao, bila kusahau TB2 drones kutoka Uturuki. Kuna taarifa ya muda si mrefu kuwa nchi takribani 28 zimeridhia na zinapanga kupeleka misaada zaidi zikiwemo silaha.

Kuna taarifa pia kuwa Ukraine imeomba msaada kwa shirika la kimataifa la Msalaba Mwekundu kusaidia kuondoa maelfu ya miili ya wanajeshi wa Urusi kuirudisha nchini Moscow. Kama ni sahihi (kulingana na taarifa ya Naibu Waziri Mkuu), inaonesha resistance iliyofanyika ni kubwa sana.

Hata hivyo, bado ni mapema. Tusubiri tuone kile ambacho kitajiri hapo baadaye!
 
Too low....
Kwa nnavyoyafahamu maandiko yako humu ndani mkuu, hukupaswa kuandika hivi
Umeandika kishabiki sana.....
Kwakuwa ameandika usichopenda kukisikia ,Mkuu wewe andika hizo facts zako ili tuone tofauti ya "too low" na wewe.
 
Back
Top Bottom