Spesheli ya watoto tu. Hasi na chanya

Spesheli ya watoto tu. Hasi na chanya

20221110_223002.jpg
 
Umaskini wa Victoria, 1900. Annie, mwenye umri wa miaka saba, na Nellie mwenye umri wa mwaka mmoja, wameketi kwenye gunia nje ya nyumba yao huko London. Walikuwa miongoni mwa watoto kumi waliozaliwa na mama mmoja Annie Daniels. Ndugu zao watano walikufa wakiwa wachanga.
20221111_164645.jpg
 
Mtoto mchanga wa Kifilipino na familia yake ndani ya mbuga ya wanyama huko New York (Coney Island), Marekani, 1906. Zoo za wanyama za binadamu wakati mmoja zilikuwa za kawaida sana katika ulimwengu wa Magharibi.
20221113_125945.jpg
 
It happened.
It’s terrible.
It’s history and is often uncomfortable.
Own it, learn from it.
Don’t let it happen again!
20221113_130726.jpg
 
 
MAMBO ANAYOTAKIWA KUZINGATIA MZAZI YA KUFANYA MTOTO AKIWA LIKIZO

By sir eliud lusanga


Kipindi hiki watoto wetu wamerudi kwa ajili ya Likizo ni vizuri wazazi kuzingatia haya:

1. Jipe muda wa kuzungumza na MTOTO Kila Siku

2. Muulizie juu ya Changamoto alizokutana nazo akiwa shule

3. kagua vitu anavyovitizama km picha, simu n.k

4.Jadiliana naye kuhusu matokeo yake ya mwaka mzima

5. Kuwa makini sana na aina ya marafiki anaokuwa nao ikiwezekana angalia background ya familia za marafiki zake

6. Mpe muda wa kwenda kwa wazazi wa pande mbili ajifunze mahusiano na familia

7. Hakikisha anapata muda wa kiroho kushiriki ibada na vikundi vya kanisani pia muombe pamoja

8. Usimpe Kila anachotaka mpe kwa sababu ni muhimu

9. Usimdekeze afanye kazi za mikono hata Kama una dada au kaka wa kazi aoshe vyombo, asafishe Nyumba, atandike chumba chake, afue nguo mwenyewe na hata kuhudumia kazi za uzalishaji hapo nyumbani

10. epukeni magomvi ya Mara kwa Mara yatakayomfanya aathirike kisaikologia

11. Kama mmeachana na mzazi mwenzako Hakikisha MTOTO anapata nafasi ya kumsalimia mzazi mwenzako

12.Usiruhusu MTOTO kushinda peke yake chumbani akicheza game mpe nafasi ya kusociliaze lakini kuwe na mipaka

13.Kama Kuna kazi za kijamii kama kutembelea yatima mpe muda afanye charity work itampa tabià ya kujali wengine

14.Epuka Sana kuonyesha kuwa una muogopa na analosema utatekeleza mahali fulani lazima kuwa strictly

15.Mpangie revision kwa kiwango Ili akili ipumzike

16.Anza kujadiliana naye kipawa chake na ndoto zako

17.Mueleze Changamoto zilizopo kama UKIMWI, USHOGA na tabia hatarishi

18.Mfundishe unyenyekevu na kuheshimu wengine

19.Mtie moyo ukimjengea uwezo wa kuwa anaweza

20.Jadiliana naye hali ya uchumi ilivyo katika familia ajue katika maisha Kuna up and down na mfundishe Umuhimu wa kushare Changamoto alizonazo.
 
 
Back
Top Bottom