Spika Bunge la Katiba: Mchuano ni kati ya Sitta na Chenge

Spika Bunge la Katiba: Mchuano ni kati ya Sitta na Chenge

............. KAMA NI KWELI ameangalia alama za nyakati
 
wote hao waliobakia sio watu wazuri, Sitta yule tunayemfahamu kwa misimamo siye tutakaye mshuhudia tena, alionyesha wazi kushabikia serikali 3, na huyo mama ni ndiye tangu mwazo alikuwa anasuka mikakati ya kuhujumu mchakato wa katiba
 
Timu Sitta-- Standard and Speed tunaikumbuka kazi yako... Mungu akusaidie na kukulinda.. Najua mafisadi wanatumia hela kukukwamisha lakini naamini utashinda kwa kishindo...
 
Kama ni kweli, basi yapasa timu ya EL irudi kwenye drawing board vinginevyo standards zitatumika kuhakikisha loopholes za kupata madaraka kijanjakijanja hazipati nafasi
 
kila la kheri wajumbe wa bunge la katiba tunawaomba weledi uwatangulie ili mmpate mwenyekiti bora,na si bora kiongozi
 
kama kweli basi mungu yupo upande wetu,mungu akujalie afya njema, ila awemakin maana anaweza kwenda india kabla kabla hajamaliza kaz yenyewe!!
 
Alafu sipendi mtu akiandika Just 6 ! Muwe na adabu kidogo
 
Kura ya kIITIFAKI INAWEZA KUTUMIKA AGAINST S.S (6). YA BI.KIROBOTO ILIKUWA HIVYOHIVYO NDANI YA CHAMA!Migiro kawekwa hapo kimkakati na watahakikisha inatumika njia yoyote kumweka kuwa mwenyekiti.
Nataka kufahamu, je hakuna utaratibu huru wenye muongozo katika sheria ya mabadiliko ya katiba kuhusu namna ya kumpata Spika bila kufuata taratibu za kichama?kwamba mtu asihitaji ruhusa ya chama chake kugombea bali yeye mwenyewe akijisikia kugombea ndo agombee!!!!!
 
Uchaguzi unafanyika lini? Tunaomba sitta achaguliwe kwa maslahi ya taifa!
 
Siasa ni mchezo mchafu sana,,,,hata sita asipopita ,,mi bado namkubali kuwa sita ni jembe
 
from chanzo cha uwakika ndani ya vyombo vya usalama wa nchi tusubiri tutaona mwisho wa picha hii ya katiba


Andrew Chenge, mbunge wa Bariadi Magharibi na mwanasheria mkuu wa zamani, amejitoa katika kinyang’anyiro cha uenyekiti wa Bunge la Katiba.

Taarifa kutoka ndani ya kinachoitwa, “Kambi ya Edward Lowassa” zinasema, Chenge ameamua kujitoa katika kinyang’anyiro hicho kwa ushauri wa kigogo mmoja mwandamizi katika idara ya usalama wa taifa.

Habari zinasema, sababu ya Chenge kujitoa katika kinyang’anyiro hicho ni kumlinda Lowassa asichafuke.

“Tunataka mgombea wetu Edward (Lowassa) asichafuke. Kumruhusu Chenge kuwa mgombea wa kiti cha uspika (uenyekiti), ni kuhalalisha kuchafuliwa Lowassa,” ameeleza mmoja wa makada wa CCM ambaye yuko karibu na Lowassa.

Amesema, “Tumepima na kugundua kwamba Chenge akiwa mwenyekiti wa Bunge la Katiba, wabaya wa Lowassa baada ya kujadili katiba watamshambulia Chenge na Lowassa. Jambo hili litatugharimu na hivyo tumeona tumuachie mzee Sitta msalaba wake.”
 
Back
Top Bottom